Na  Denis Chambi, Tanga

Wanafunzi , walimu pamoja na waumini wa dini ya Kiislamu zaidi ya 130 kutoka Taasisi ya Bilal Muslim Mission of Tanzania tawi la Tanga wameshiriki kikamilifu katika zoezi la uchangiaji wa damu salama katika hospotal ya rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo ikiwa ni maadhimisho ya mwaka mpya wa kiislamu ukiambatana na kukumbuka kifo cha mjukuu wa Mtume (S. A .W) Imamu Houssein Ally.

Akizungumza mara baada ya tukio hilo Mkuu wa shule ya wasichana katika taasisi hiyo Sheikh Sajad Hassan amesema kuwa uchangiaji wa damu katika hospitali hiyo kawaida yao ya  kila mwaka ikiwa ni ishara ya kuonesha moyo wa kujitolea  wahitaji mbalimbali hususani watoto na mama wajawazito waliopo hospital wanaohitaji kuongezewa damu.

"Lengo la kuja kuchangia damu hapa hospital ni kujitolea sadaka,  tunaifungamanisha sadaka yetu na tukio la kuwawa kwa mjukuu wa bwana mtume (S.A .W) Hussein Bin Allyy aliyeuwawa mwaka 61 Hijiria huko Irak aliyekuwa wakiipigania dini kwa lengo la kukemea mabaya na kuamrisha mema,  aliyetoka kutetea wanyonge  na wale waliodhurumiwa" 

"Na sisi taasisi ya Al Bilal Muslim hili ni zoezi ambalo  tunalifanya kila mwaka tukija kuchangia damu katika maeneo tofauti tofauti lengo na sisi ni kuonyesha kwamba tumesimama pamoja na mjukuu wa bwana mtume (S.A.W) katika kutetea wanyonge,  damu itasaidia wanyonge,  pia tunasimama na kukemea dhuruma zozote  zinazoendelea ulimwenguni" alisema Sheikh Hassan.

Kwa upande wake mkuu wa  idara ya maabara ya damu katika hospital ya rufaa ya mkoa wa Tanga Bombo ,  Sinde Ntobu ameishukuru na kuipongeza  taaisisi hiyo kwa kuona  kuwa wanayo nafasi kubwa kuokoa maisha ya watu wanaofika hospitalini hapo kupatiwa  huduma ikiwemo kuongezewa damu.

Alisema uhitaji wa damu kwa mwezi katika hospital hiyo ni mkubwa tofauti na ile inayochangiwa ambapo uhitaji wao  unafikia lita 500 hadi 600 wakiwa na upungufu wa damu kwa Unit 250 hadi 300 hivyo kuziomba taasisi na watu binafsi kuona umuhimu wa kuchangia damu ili kuokoa maisha ya watu.

"Tunashukuru  sana siku ya leo tupo na wenzetu wa taasisi ya Bilal Muslim ambao kila mwaka huwa wanakuja kuchangia damu salama kwaajili ya wagonjwa wenye uhitaji wa damu tunawashukuru sana kwasababu kila mwaka wana tukio kama hili tunawapongeza kwa moyo wao huo wa kuweka katika kalenda yao" alisema Ntobu.

" Sisi kama hospital kwa wastani kwa mwezi tunatumia  chupa za damu 500 mpaka 600 lakini uwezo wa kuchangia damu ambayo inapatikana  mara nyingi  tunapata unit 250 mpaka 300 kwahiyo uhitaji wa damu kwa wagonjwa ni mkubwa ,  kikubwa niiase jamii kwa sababu damu ni huduma ambayo hainunuliwi mahali popote bali inatoka kwa wananchi kwenye jamii  tunahitaji jamii ijitolee damu kwa hiari lakini muamko wa jamii katika zoezi hili ni mdogo" alisisitiza.

Mbali na uchangiaji wa damu taasisi ya Al Bilal Musilim Mission of Tanzania pia iliweza kuchangia vitu mbalimbali ambavyo ni mahitaji kwa wakinamama wanaojifungua katika hospital hiyo.
 
 
Mkuu wa shule ya wasichana wa taasisi ya Bilal Muslim Mission of Tanzania tawi la Tanga , Sheikh Sajad Hassan akishiriki katika zoezi la uchangiaji wa damu salama lililofanyika july 27 katika hospital ya rufaa ya mkoa wa Tanga Bombo.

Damu salama iliyokwisha kuchangiwa na walimu , wanafunzi na waumini wa dini ya kiislamu kutoka katika  taasisi ya Bilal Muslim Mission of Tanzania tawi la Tanga , Sheikh Sajad Hassan akishiriki katika zoezi la uchangiaji wa damu salama lililofanyika july 27 katika hospital ya rufaa ya mkoa wa Tanga Bombo.

Baadhi ya vitu mbalimbali ikiwemo sabuni vilivyotolewa kwa wazazi waliopo katika hospital ya rufaa ya mkoa wa Tanga Bombo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho yanayofanywa kila mwaka na taasisi ya Bilal Muslim Mission of Tanzania tawi la Tanga.


Share To:

Post A Comment: