DENIS CHAMBI, MARA.

KILIMO kinalipa! ndicho unachoweza kusema unapotaka kumzungumzia  Nyihita Wilfred mwekezaji mzawa aliyejikita kwenye sekta ya kilimo kupitia zao la Alizeti  katika Kijiji Nyanchabakenye Wilaya ya Rorya mkoani Mara ambapo sasa amekuwa mwarobaini kwa wakulima wengine ambao wamepata soko la kuweza kuuza mazao yao baada ya kuanzisha kiwanda cha kuchakata zao hilo la mafuta Nyihita  Sunflower Cooking oil Production.

Mbali na mapinduzi ya kiwanda hicho alichokijenga kwaajili ya kuchakata zao hilo na kuwa mzalishaji mkubwa wa mafuta yayokanayo na Alizeti lakini pia ameweza kufungua na kutoa ajira kwa vijana hatua ambayo ni ya kujivunia kwa wana Mara ambao hujipatia kipato chao kutokana na uwekezaji huo.

Mwekezaji huyo anasema aliigeuza changamoto na kuwa fursa kwake hii ni kutokana na kukosekana kwa kiwanda cha zao la Alizeti ndani ya mkoa huo  na hivyo kupata wazo la kuja na sasa ana miliki kiwanda cha kuzalisha mafuta ya kula yatokanayo na zao hilo alichokipa jina lake la Nyihita Sunflower Cooking oil Production.

"Nilipata wazo la kuja kufanya  uwekezaji wa kilimo cha Alizeti  ndani ya mkoa wa Mara  ikiwa ni eneo ambalo halikiwahi kuwa na historia ya kilimo cha Alizeti na niliamini kwamba malighafi zinapatikana kijijini na maendeleo makubwa na mapinduzi ya viwanda yanafanyika  vijijini."

"Nialiamua kuja vijijini ambako niliamini ninaweza kuja kuwashawishi wakulima ambao mashamba yapo ili waweze kulima na ni kweli wazo hili lilifanikiwa kwa asilimia 100 kwani wakulima walijitokeza na kuanza kulima kilimo cha Alizeti mwaka 2019, na ilipofika 2020 wakulima walianza kujiuliza maswali mara baada ya kulima mazao tutauza wapi nikapata wazo kwa kutafuta wazo la soko na kujenga kiwanda  baada ya kuanza ujenzi huo kiwanda hiki kilizinfuliwa rasmi 2021 na  kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa  na ndio kikaanza kufanya kazi mpaka sasa" alisema 

Anasema anajivunia kuwa mwekezaji mzawa na mmoja wa watanzania ambao wanaweza kuzalisha fursa za ajira kwa wananchi wanaozunguka eneo hilo sambamba na kuwapatia soko la uhakika  wakulima hatua ambayo imekuja kuleta mwamko wa wakulima wengi kujikita shambani tofauti na ilivyokuwa awali.

"Pamoja na hayo uwepo wa kiwanda hiki kimeweza kutengeneza fursa za ajira  kwa vijana wetu wa kitanzania  lakini pia kuongeza  uchumi wa mtu mmoja mmoja kwahiyo tumeongeza wigo mpana kwa ndugu zetu wa Mara  kuweza kuongeza pato lao kupitia kiwanda hiki na wakulima kuweza kupata soko la uhakika na kuuza malighafi zao hapa na pia kiwanda hiki kimeweza kuwa faida kwa nchi yetu ya Tanzania kwani tunalipa kodi na  zinasaidia kuleta maendeleo kwenye Taifa letu" aliongeza mwekezaji huyo.

"Ni wito wangu kwa watanzania na wana Mara kujikita kwenye kilimo cha Alizeti wakitumie kama fursa  na kuhakikisha tunasaidia kuinua uchumi wa Taifa letu lakini pia kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja  ndani ya Tanzania kwa ujumla" alisisitiza.

Nyihita anasema ukubwa wa kiwanda hicho hauendani sawa na mali ghafi inayozalishwa mashambani ambayo imekuwa ni mdogo  hatua ambayo amewaasa wananchi kuendelea kujikita katika kilimo hicho kwani tayari uhakika wa wapi watauza mazao yao upo ni suala tu la kuongeza uzalishaji.

"Uwezo wa kiwanda ni mkubwa  tofauti na Malighafi inayoweza kupatikana, kwa misingi hiyo basi tunahitaji wakulima wajitokeze kwa wingi kulima  wakijua kwamba fursa ya soko la uhakika ipo ili waweze kusaidia kiwanda kuweza kuzalisha kwa wingi na kupata ukamilifu wa uhitaji wa mali ghafi"

"Sasa hivi wizara ya kilimo  imeanzisha kilimo biashara wazo hili linasaidia vijana wakitanzania na watanzania kwa ujumla kuweza kujikita  kwenye kilimo kwahiyo kupitia wazo hili la kilimo biashara litasaidia watanzania kujiwekeza  ni matumaini yangu kwamba kupitia kilimo biashara vijana wengi watajitokeza  kulima zao hili ambalo litasaidia  kuongeza utoshelevu wa uhitaji wa malighafi"

Meneja wa kiwanda hicho cha  Nyihika Sunflower Cooking oil Production  Happiness Masunga  alisema wakiwa na uwezo wa kuajiri watu mbalimbali kwa siku kina uwezo wa kuchakata tani 24 lakini kutokana na changamoto ya upatikanaji wa  malighafi kwa sasa wanazalisha chini ya kiwango  hado  asilimia tano kwa siku.

"Mchakato wa Kiwanda hiki ulianzia mwaka 2019 kama sehemu ya uhamasishaji wa kilimo uwezo soko Ia  Alizeti  kwa wakulima  wa Mara  na ilipelekea kuanzishwa kwa kiwanda hiki 2021 na sasa kinatambulika na serikali na kuajiri watu mbalimbali, kiwanda hiki kwa siku kina  uwezo kuchata hadi tani 24  lakini kutokana na  ukosefu wa malighafi za kutosha sasa hivi uchakataji  wake  umeshuka sana hadi asilimia tano" alibainisha meneja huyo.

Mariam Hamis ni miongoni mwa waajiriwa wa kiwanda hicho anasema "Vijana wengi tunafaidika na kunufaika na uwepo wa kiwanda hiki kutupatia ajira ambapo watu waliosoma na wasio soma wameweza kuajiriwa katika kiwanda cha Nyihita Sunflower Cooking oil Production na kimeweza kupunguza upungufu wa ajira ambalo ni tatizo bado katika nchi yetu, uwepo wa kiwanda hiki umekuwa na manufaa kwa wananchi  wengi".
Mkurugenzi wa kiwanda cha Nyahita Sunflower Coking Oil Production Nyihita Wilfred (watatu kulia ) akiwa a wageni mbali mbali pamoja na waandishi wa habari waliombelea kiwandani hapo hivi karibuni
Mkurugenzi wa kiwanda cha Nyahita Sunflower Coking Oil Production Nyihita Wilfred akimkabidhi mafuta ya Alizeti mwandishi wa habari Ibrahim Kunoga wakati  alipomtembelea katika kiwanda chake kujifunza namna jinsi kiwanda hicho kinavyofanya kazi.

Meneja wa kiwanda hicho cha  Nyihika Sunflower Cooking oil Production  Happiness Masunga  akiwaongoza wageni waliotembelea kiwandani hapo  kujua na kujifunza namna jinsi kinavyofanya kazi ya uzalishaji wa mafuta ya kupikia yatokanayo na zao la Alizeti.
 

Share To:

Post A Comment: