NA DENIS CHAMBI, TANGA.

Wakala wa vipimo Tanzania ‘WMA’ mkoa wa Tanga imewataka wauzaji na wasambazaji wa mitungi ya gas ya kupikia  ya  jumla na reja reja kuhakikisha kuwa ujazo wa mitungi wanayowauzia wananchi inakuwa sahihi  na kuepukana na udanganyifu wa aina yeyote ile ili kujipatia faida zaidi kinyume cha sheria na taratibu zilizowekwa.

Wito huo umetolewa na  Afisa mwandamizi wa wakala wa vipimo Tanzania ‘WMA’ mkoa wa Tanga Ally Mtowa wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye maonyesho ya 10 ya  biashara na utalii  yanayoendelea katika viwanja vya Mwahako ambapo alisema katika kuwadhibiti wauaji wote wa mitungi ya gas ofisi hiyo imekuwa na utaratibu wa kutoa elimu kwa wafanyabaishara wote.

“Tumeshafanya semina kwa wadau ambao wanafanya biashara za kuuza gas  wakiwemo wale wanaojaza mitungi  viwandani pamoja na wale wauzaji wa jumla na reja reja wamepewa elimu  ya namna gani wahakikishe mitungi inakuwa na ujazo sahihi na anatakiwa wawe na mzani ambao umehakikiwa na wakala wa vipimo na apime ule mtungi wa gas kama una ujazo sahihi  kabla hajaanza kumuuzia mwananchi”

Aidha amewataka wafanyabiashara na wamiliki wa vituo vya mafuta kutokuchezea mizani wakati wa kuwahudumia wateja  akisema kuwa yapo  baadhi ya malalamiko kutoka kwa wateja wakiwemo wamiliki na madereva wa  vyombo vya usafiri wakilalamika juu ya changamoto hiyo ambayo inaenda kinyume cha sheria zilizowekwa .

Hata hivyo Mtowa alisema katika kutua changamoto  licha ya kuendelea kuwabana na kuwachukulia sheria wamiliki na wafanya biashara wa vituo vya mafuta  ofisi ya wakala wa vipimo mkoa wa Tanga imekuwa ikitoa elimu kwa wananchi mara kwa mara ili kuwa na uelewa pale wanapoenda kupata huduma hiyo huku akiwataka kutoa taarifa pindi wanapo baini udanganyifu wa aina yeyot. 

“Majukumu yetu zaidi ni kumlinda mlaji  na madhara yatokanayo na vipimo ambavo havina usahihi mfano katika vituo vya  kujazia mafuta tunahakikisha kipimo kinatoa mafuta kwa usahihi sheria zipo ambazo zinawaongoza na kuwabana wamiliki na wafanyabiashara wote wanaouza mafuta wapo ambao tumeshawachukulia  hatua ikiwemo kupigwa faini na kama kosa litajirudia rudia wanaweza kufikishwa mahakamani , nawaomba wawe waadilifu kuweza kuhudumia wananchi na wahakikishe kwamba muda wote vipimo vyao vinakuwa sahihi” alisema afisa huyo.

Pamoja na hayo alisistiza zaidi kwa wafanyabiashara wadogo wadogo wanaouza vyakula na vitu vya majumbani kuhakikisha kuwa mizani zao wanazotumia kupimia zinakuwa na ubora na zilizo hakikiwa n a ofisi ya wakala wa vipimo kadiri ya utaratibu uliowekwa hii ikilenga kutoa huduma zaidi kwa wananchi na kuwalinda na madhara ambayo yanaweza kujitokeza.

 “Tumekuwa tukitoa elimu mara kwa mara kwa wananchi kwahiyo tunajitahidi kwa kiasi kikubwa kuhakikisha kwamba tunamlinda mwananchi kwenye vipimo , tuna kaguzi za m iani ambazo zinafanywa na watendaji katika serikali za mitaa lakini na wao wafanyabishara wenyewe tunawaelimisha jinsi ya kutumia mizani na kama ni mwananchi wa kawaida uzingatia vitu gani na pindi unapoona kuna udanganyifu wa vipimo usisite kufika ofisni ili tuweze kuchukua  hatua zaidi” aliongeza.

Maonyesho ya biashara na utalii  ambayo hufanyika kila mwaka jijini Tanga yakihusisha makampuni na taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali mwaka huu  yakiwa ni ya 10 yamebebwa na kauli mbiu ya ‘Kilimo , viwanda utalii na madini ndio msingi wa maendeleo ya kiuchumi’
 
Afisa mwandamizi wa wakala wa vipimo Tanzania ‘WMA’ mkoa wa Tanga Ally Mtowa akizungumza na waandishi wa habari wakati wa maonyesho ya 10 ya biashara na utalii yanayoendelea katika viwanja vya mwahako jijini Tanga.
 
Share To:

Post A Comment: