Na Denis Chambi,Tanga.
Naibu waziri wa ujenzi na uchukuzi Atupele Mwakibete ameliagiza shirika la Reli Tanzania mkoa wa Tanga kuhakikisha ikarabati kipande cha reli kinachotoka kituo kikubwa cha Mkwakwani hadi bandari ya Tanga hii ikilenga hasa kuongeza kasi ya usafirishaji wa mizigo inayotoka na kuingia katika bandari hiyo.
Alitoa
 maagizo hayo  april 1,2023 mara baada ya kutembelea   mradi wa ukarabati katika bandari hiyo  ambapo kwa sasa umefikia  asilimia 98.9  katika utekelezaji wake 
ikiwa ni uboreshaji wa gati  2 kutoka urefu wa kilomita   1.7 hadi 
kilomita 450 pamoja na kuongeza kina cha bandari kutoka mita 3 hadi 13 
mradi wote ukigharimu jumla ya shilingi Billion 429.1 zilizotolewa na 
serikali.
Mamlaka ya 
Bandari ambayo ilikiri kupokea mapendekezo hayo ya ukarabati wa kipande 
hicho cha reli hivi karibuni kutoka shiria la reli ilieleza mbele ya naibu waziri kuwa itakaa na ndani ya 
wiki moja na kutoa  majibu ya  ukarabati huo huku Naibu waziri 
akizipunguza siku hizo na kuwaagiza ndani ya siku tatu kuja na majibu 
kamili ya nini kifanyike ili kuweza kukamilisha mradi huo. 
Hata
 hivyo shirika la reli ambalo limeshapeleka mapendekezo ya gharama 
kwaajili ukarabati wa kipande cha reli hiyo kinachotoka kituo kikubwa 
hadi bandarini hapo   tayari  TPA wameshatenga kiasi cha shilingi 
Million 500 kwaajili ya kazi hiyo.
"Nimewapa
 maelekezo watu wa Reli kwamba walichelewa kuleta mapendekezo kwa 
mamlaka ya Bandari na Mamlaka ya Bandari wana fedha kwaajili ya zoezi 
hilo na wamesema ndani ya wiki moja watakuwa  wameshazipitia ili  watu 
wa reli waanze kufanya hiyo kazi na mimi nimesema sio wiki moja,  wiki 
moja ni mbali fanyeni ndani ya siku tatu muwe mmeshawarudishia majibu 
watu wa reli ili waanze  kuihuisha reli iliyokuwepo zamani ndani ya 
bandari hii ya Tanga" alisema Mwakibete.
Uboreshaji
 wa bandari hiyo umeanza kuzaa matunda kwani kwa kipindi cha mwezi 
january hadi march 2023  wamefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi 
billion 5 ikivunja rekodi zaidi ya kupokea meli kubwa  ambapo hivi 
karibuni ilipokea Meli Metsovo  iliyotokea nchini Marekani yenye ukubwa 
wa Mita 189.9 ikiwa imebeba malighafi zinazotumika viwandani pamoja na 
meli nyingine mbili ambapo awali hazikuweza kufika kutokana na kina 
kidogo cha Bandari hiyo.
Awali akizungumza Mhandisi kutoka shirika la Reli "TRC' Patience Karumuna
alisema
 kuwa mara baada ya kupokea maagizo kutoka kwa Makamu wa Rais Philipo 
Mpango mwishoni mwa Mwaka jana walifanya  usanifu wa kujua mahitaji  ya 
kipande hicho kinachoenda bandarini ambapo walifanikiwa kukamilisha na 
kuikabidhi mamlaka ya Bandari ya Tanga.
"
 Baada ha kupokea maagizo kutoka kwa makamu wa Rais ilikuwa mwezi 
December upande wa shirika tukishirikiana na  TPA hatua za  kwanza 
kabisa tulizofanya ni kurudishia miundombinu ya reli upande wa stesheni 
na tumekamilisha ,   kwa upande wa  Bandari tumeleta wasanifu wakaja  
tukaangalia mahitaji yaliyopo kwa sasa hivi   tukatengeneza makisio ya 
gharama ambalo nalo tumelikamilisha tumeikabidhi  mamlaka ya Bandari 
'TPA' kwaajili ya wao  waweze kulipitia "alisema Karumuna
Akizungumza
 kaimu Meneja wa bandari ya Tanga Petter Milanzi aliishukuru serikali 
kwa uwekezaji na maboresho makubwa hayo yaliyofanyikia ambayo sasa 
matunda yake yanaonekana huku akiwakaribisha wadau na wafanyabiashara wa
 ndani na nje ya nchi kuitumia bandari hiyo.
"Sisi
 kama  Bandari tunatoa wito kwa wadau wetu wote na watumiaji wa bandari 
kwamba bandari ya Tanga imeshafunguka tupo tayari kuwahudumia na kutoa 
huduma bora ,  tumeshajiandaa kukabiliana na ushindani ili kuweza 
kuwahudumia wateja wetu vizuri,  tunajua serikali imewekeza fedha nyingi
 kwahiyo fedha zile zilizowekezwa lazima zitoe faida hivyo sisi kama 
bandari ya Tanga lazima tutoe uhakika kuwa tupo tayari kufanya kazi ili 
bandari hii iwe inaleta faida kubwa kadiri ya kilichowekezwa" alissma 
Milanzi.
 Kaimu meneja wa bandari  Tanga Petter Milanzi akitoa maelezo kwa Naibu waziri wa ujenzi na uchukuzi Atupele Mwakibete wakati alipofanya ziara ya yake ya  siku moja kutembelea mradi unaoendelea katika bandari hiyo april 1,2023.
 Naibu waziri wa ujenzi na uchukuzi Atupele Mwakibete akipata maelezo kutoka kwa mhandishi wa shirika la Reli Patience Karumuna kuhusu miundombinu ya reli ambayo inatakiwa kufika bandarini hapo ili kuzidi kurahisisha usafirishaji.
 Naibu waziri wa ujenzi na uchukuzi Atupele Mwakibete akipata maelezo kutoka kwa meneja wa mradi wa Rafael Angulo Niras Resident wanaotekeleza mradi katika bandari ya Tanga ambao mpaka sasa wamefikisha asilimia 98.9.
Post A Comment: