Mhaidrolojia wa Bodi ya Maji Bonde la Rufiji (RBWB), Ally Diwani akiwaelezea waandishi wa habari namna wanavyopima kiwango cha maji kwenye bonde hilo.

Na Selemani Msuya, Iringa

BODI   ya   Maji   Bonde   la   Rufiji   (RBWB)   imesema   ilikuhakikisha uwekezaji mkubwa wa miradi mbalimbali yauzalishaji  inakuwa endelevu wanatarajia  kuajiri walinzi50 ambao watalinda vyanzo mbalimbali vinavyotiririshamaji eneo hilo. 

Hayo   yamesemwa   na   Mkurugenzi   Mkuu   wa   RBWB,Florence   Mahay   wakati   akizungumza   na   waandishi   wahabari   kutoka   katika   vyombo   vya   habari   mbalimbaliambao wapo kwenye ziara ya kutembelea bodi hiyo.

Mahay alisema bonde hilo  linapokea  maji   kutoka  mitomikubwa   minne   ambayo   ni   Ruaha   Mkuu,   Kilombero,Luwegu na Rufiji.Mkurugenzi   huyo   amesema   kutokana   na   faida   ambazozimeonekana   na   zinaendelea   kuonekana   wamejipangakuongeza   ulinzi   kwenye   bonde   hilo   ambapo   katikamwaka   wa   bajeti   wa   2023/2024   wanatarajia   kuajiriwalinzi 50 ambao watalinda vyanzo vilivyopo.

Amesema   wamejipanga   kulinda   vyanzo   vya   majivinavyoingiza   maji   katika   bonde   hilo,   ili   kuhakikisha shughuli za kiuchumi zilizopo zinakuwa endelevu, kwakuwa zinachangia ukuaji wa uchumi.

Mahay   amesema   bodi   hiyo   ina   kazi   moja   kuu   yausimamizi   wa   rasilimali   za   maji,   kwa   kuhakikishawanatambua kiasi cha rasalimali maji kwenye bonde hilo,kugawa   maji,   kutunza   vyanzo   vya   maji   na   kuzuiauchafuzi.

Mkurugenzi   huyo   amesema   wamelazimika   kuwapitishawaandishi wa habari katika maeneo ya Bonde la Rufiji, ilikuhakikisha umma unapata taarifa sahihi katika eneo hilo.

“Serikali imewekeza katika Bonde la Rufiji kwa kujuengamiradi   ya   kuzalisha   umeme,   kama   Bwawa   la   Mtera,Kidatu   na   Kihansi   na   kwa   sasa   Mradi   wa   UzalishajiUmeme wa Mwalimu Nyerere (JNHPP). Miradi yote hiyoina   mchango   katika   uchumi   wa   nchi   kama   unavyoonaasilimia 80 ya umeme wa maji unatokea hapo.Lakini pia ukubwa wa bonde hili unachangia asilimia 50 ya miradi kilimo cha umwagiliaji, kama chai na sukari,hivyo tunakuwa na usalama wa chakula na tuna mbuga zawanyama takribani sita,” amesema.

Mahay amesema kwa sasa Bonde la Rufiji lina maji yakutosha ambapo kuna mita za ujazo bilioni 40, mita za ujazo bilioni 31 juu ya ardhi na bilioni 9 ni chini ya ardhi,huku   maji   yanatumika kwa kutolewa vibali ni mita zaujazo bilioni 2.4.

Amesema kwa sasa bodi hiyo imesitisha utoaji wa vibalivya maji ikiwa ni maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan,ili kuhakikisha maji yanajaa kwenye Bwawa la Nyerereambalo linatarajiwa kuzalisha megawati 2,115.

Mahay   amesema   bodi   hiyo   haitasita   kubomoamiundombinu ya wale ambao watabainika kutumia majibila kupewa vibali, hivyo wataka wananchi hasa jumuiyaza watumiaji maji kutoa taarifa pale wanapobaina.“Naomba   nisisitize   kuwa   bodi   hii   haitamvumilia   mtu yoyote   anashiriki   kutumia   maji   bila   kibali,   jumuiya   zawatumia maji tunaziomba ziendelee kutoa ushirikiano, ilikuhakikisha uwekezaji unaofanywa na serikali unakuwaendelevu,” amesema.

Kwa upande wake Mhaidrolojia wa RBWD Ally Diwani,amesema kitengo chao kina vituo 137 ambapo vituo 59vinapima maji juu ya ardhi, 29 chini ya ardhi na 49 vyahali ya hewa.Amesema katika eneo hilo wana changamoto ya uharibifuwa vituo, wizi na uvunjaji wa vifaa vinasaidia kuchukua takwimu kwa ajili ya tathminj ya rasilimali maji kwenyebonde.

Naye   Msimamizi   wa   Kitengo   cha   Ugawaji   RasilimaliMaji wa Bodi, Mhandisi Gallus Ndunguru amesema hadisasa wametoa vibali 2005 kwa watumiaji maji mbalimbaliwalioko katika eneo la bonde.“

Pia   tumetoa   vibali   10   vya   kutiririsha   maji   taka   kwataasisi   mbalimbali   ambao   wanatoa   huduma   zao   kwakutumia maji. Ila kwa sasa tumesitisha kutoa vibali vyawawekezaji   wakubwa   hasa   katika   maeneo   ambayoyameathirika,” amesema.

Ofisa   Maendeleo   ya   Jamii   RBWB,   Upendo   Lugallaamesema   katika   kuhakikisha   bonde   hilo   linakuwaendelevu wanataerajia kupata miti 200,000 rafiki na maji.Amesema   pia   kupitia   idara   yao   wamefanikiwa   kuundajumuiya 42 za watumiaji maji ambao wanashiriki kulindavyanzo vya maji katika bonde hilo. 


Mhandisi wa Maji, Bodi ya Maji Bonde la Rufiji (RBWB), Gallus Ndunguru,  akiwaelezea waandishi wa habari namna wanavyotoa vibali vya maji kwenye bonde hilo.
Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Maji Bonde la  Rufiji (RBWB), Florence Mahay akifafua jambo mbele ya waandishi wa habari waliotembeleofisi za bonde hilo mkoani Iringa.
Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Maji Bonde la Rufiji (RBWB), Florence Mahay akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mikakati yao ya kulinda bonde hilo, ili liwe endelevu.
Ofisa Maendeleo ya Jamii wa Bodi ya Maji Bonde la Rufiji (RBWB), Upendo Lugalla akielezea namna idara yao inavyotoa elimu ya utunzaji rasilimali maji
 

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: