Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Leonard Mahenda Qwihaya akikabidhiwa cheti cha pongezi kwa ushindi alioupata kutoka kwa Mkuu wa mkoa wa Iringa Halima Dendego wakati wa sherehe za pongezi

Na Fredy Mgunda, Iringa.


Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Leonard Mahenda Qwihaya amesema ataweka taa ili kuondoa giza kwenye Kituo Cha Mabasi cha Mji wa Mafinga, Wilayani Mufindi.


Qwihaya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Makampuni  ya Qwihaya amesema kwa hadhi ya mji huo hautakiwi kuwa stendi yenye  giza.


"Kwa Tanzania, mji wa Mafinga unaweza kuwa wa kwanza au wa pili kwa mapato kwa hiyo ni aibu kukosa taa za babarani kwa hiyo nitaweka  taa kwenye  stendi yote,"  amesema Qwihaya.


Qwihaya alitoa ahadi hiyo katika hafla ya pongezi iliyokuwa imeandaliwa na wananchi wa Mufindi kwa lengo la kuwapongeza viongozi wa CCM wa ngazi ya Mkoa na Taifa walio chaguliwa kutoka katika Wilaya hiyo.

Share To:

mwangaza wa hbari

Post A Comment: