Mbunge wa Jimbo la Chalinze ambaye pia ni Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti na Utumishi wa Umma Ridhiwani Kikwete, amekabidhi msaada kutoka Serikali ya wanafunzi wa IFM kupitia kamati ya Charity 2023 ambao ni matundu 20 ya choo kwa ajili ya wanafunzi na walimu, taulo za kike katika shule ya Msingi Miono, baiskeli nne kwa ajili ya watoto wenye ulemavu, bima za afya kwa watoto 40 wenye mahitaji maalum katika kituo cha Hope disability centre. 

Msaada huo umetolewa wakati IFM Charity inatimiza miaka 10 tokea wameanza kutoa msaada ambayo imeendana na maadhimisho ya miaka 10 ya IFM Charity







Share To:

Post A Comment: