NA DENIS CHAMBI, TANGA.

MWENYEKITI wa chama cha  waandishi wa habari mkoa wa Tanga, Tanga Pres Club(TPC) Bi Lulu George amewaasa wanahabari  kujikita katika uandishi wa habari za kiuchunguzi na za  kijamii hasa zile zinazohusu kundi la watoto hii ikiwa ni pamoja  na kuibua matukio ya ki ukatili yanayotokea  katika jamii ili kuunga mkono kampeni ya serikali na wadau mbalimbali wa maendeleo hapa nchini  ya  kupinga na kutokomeza ukatili dhidi yao.

Ametoa wito huo November 5,2022 wakati wa semina iliyoandaliwa na taasisi ya Tanga Youth Talent Association (TAYOTA) kwa waandishi wa habari yenye lengo la  kuwajengea uwezo na ulewa wa kuripoti taarifa zinazohusu ukatili dhidi ya watoto na vijana wa kundi balehe zinazotokea katika jamii ambapo amesema kuwa  bado yapo matukio mengi ya ukatili yanatokea na hayatolewi taarifa hivyo ni vyema wanahabari   wakajua kuwa wanahusika moja kwa moja katika kupiga na kutokomeza ukatili ambao unazidi kushamiri kwenye maeneo mbalimbali.

“Suala la uandishi wa habari za kiuchunguzi hatuwezi kulikwepa  hili jukumu ni letu  na ndio litaleta hasa maana halisi ya  kile tunachokiandika ambapo  kitakuwa na tija kwa jamii  niwaombe sana tuone kuwa sisi ni sehemu na daraja katika suala la  kupinga na kutokomeza ukatili kwa maslahi mapana ya Umma” alisema Lulu,

Amesema kuwa mwandishi wa habari hapaswi kufungamana na upande wowote pale anapohitaji kutolea taarifa zinazohusu ukatili wa mtoto kwenye jamii badala yake asimamie maadili  taratibu na kanuni zinazomuongoza katika taaluma yake huku akiwataka kupenda kujifunza na kusoma kwa kina sheria zinazomlinda mtoto ili ziweze kuwarahishia wakati wanapohitaji kuchunguza matukio ya ukatili yanayotokea kwenye maeneo mbalimbali.

“Na kama tunataka kuandika maswala ya watoto kwa kina  ni lazima tuepushe uharaka tusome sheria na majarida mbalimbali  inahitaji utulivu na niwatoe hofu kwamba uandishi wa habari za kiuchunguzi sio kuandika  kila kinachosemwa peke yake bali tupende kujifunza kwa kina sheria zinazomlinda mtoto na sasa hivi teknolojia imekuwa ni rahisi na nyepesi sana kwetu ni suala la sisi kujua na kupenda kile kinachozungumzwa tunakifwatilia kwa namna gani”aliongeza



Akizungumza katika semina hiyo Afisa vijana kutoka halmashauri ya jiji la Tanga Fadhili Secha amesema kuwa lipo wimbi kubwa la vijana na watoto wanaojishughulisha na biashara za uuzaji wa kahawa, karanga na mayai ambao kwa umri wao wanapaswa kuwepo shuleni hivyo ni vyema waandishi wakafanya uchunguzi kujua  sababu zinazopelekea kuongezekwa kwa kundi hilo ambao licha ya kujihusisha katika biashara hizo zipo adha mbalimbali wanazokutana nazo.

“Vipo visa vya watoto wanaofanya baiahara za uuzaji wa karanga mayai na kahawa lakini wengine wanatoka katika mazingira magumu, ukweli ni kwamba wanakutana na changamoto nyingi sana hili ni kundi ambalo lintakiwa liangaliwe  hivyo waandisi wa habari tunatakiwa tusiwe waoga au tusiache kuripoti taarifa kama hizo” alisema Secha

Aliongeza kuwa zipo jitihada mbalimbali zinazofanywa na halmashauri ya jiji la Tanga katika  kuhakikisha kundi la vijana wasio na ajira mtaani linapungua au kuondoka kabisa ambapo wanaendelea kutoa mikopo ya asilimia 10  isiyo na riba kwa kundi hilo hivyo kuwaomba waandishi wa habari kutumia weledi wao kuelimisha jamii hasa vijana kujiunga katika vikundi mbalimbali vitakavyowawezesha kupata mikopo hiyo ili iweze kuwaletea maendeleo na hatimaye kuepuka kujihusisha na makundi hatarishi .

“Hili kundi la vijana linataabika sana na mambo mengi , wengi wanahangaika kwaajili ya kupata namna ya kujitegemea katika maisha na wengine ni suala la   kukosa mitaji lakini serikali kwa namana walivyotengeneza kuna fursa za utoaji wa mikopo  ile mikopo ipo tena ni mikopo ambayo ina masharti nafuu  niwakumbushe waandishi wa habari sehemu ambayo tutakuwa tunapita tuwakumbushe vijana waje kwenye halmashauri zao  kuja kuchukuwa mikopo hiyo wakiwa kwenye vikundi vyao”.

“Lakini pia Tarehe 14 October mwaka huu tulipokea muongozo mpya kutoka wizara ajira vijana na watu wenye ulemavu iliyompa fursa kijana mmoja mmoja kuweza kukopeshwa na hii ni mikopo kutoka wizarani hivyo kijana anaweza akaja akajaza fomu tukazituma Dodoma na hatimaye akapata fedha zake” alisema

Kwa upande wao baadhi ya  wadau walioshiriki semina hiyo wameipongeza taasisi ya Tanga Youth Association (TAYOTA) kuwa kulitambua kundi la wanahabari katika jitihada zao za kupambana na vitendo vya ukatili huku wakiwaomba kupelekaa semina hiyo kwa makundi mengine wakiwemo wazazi ili kuzidi kupanua wigo na kuongeza elimu kwa jamii katika kupiga vita ukatili hususani  kwa watoto na vijana waliop0 kwenye kundi balehe.

 

Share To:

Post A Comment: