NA DENIS CHAMBI,  TANGA

TAASISI ya Tanga Youth Tallent Association (TAYOTA) imefanikiwa kutoa elimu ya ukatili kwa watoto  wapatao elfu sitini (60,000) wa shule 108 za msingi na sekondari zilizopo katika halmashauri ya jiji la Tanga hii ikiwa ni jitihada za kuendelea kupambana na kutokomeza ukatili wa kijinsia  ambao unaendelea kushamiri katika jamii mbalimbali hapa nchini.

Hayo yameelezwa na mkurugenzi wa taasisis hiyo ya TAYOTA  George Bwire wakati akizungumza kwenye semina ya waandishi wa habari wa mkoa waa Tanga inayolenga kuwajengea uwezo wa kuandika na kuripoti habari bazihusu maswala ya jinsia katika jamii semina ambayo pia ilihudhuriwa na  wawakilishi kutoka mahakama, vyama vya siasa, jeshi la Polisi, TAKUKURU,viongozi wa dini, jeshi la Magereza na maendeleo ya jamii kujadili pia namna jnsi ya kupambana na vitendo vya ki ukatili.

Bwire amesema kuwa dhamira ya semina hiyo ni katika kutekeleza mradi wao unaolenga kutokomeza visa vya ukatili kwa watoto na vijana waliopo katika rika balehe ndani ya jiji la Tanga mradi ambao  unafadhiliwa na shirika la Bortner Foundation ambapo wamevipa kipaumbele vyombo vya habari kama nyenzo sahihi ya kupeleka ujumbe kwa jamii juu ya mikakati wanayoenelea nayo ya kumbana na kutokomeza ukatili  katika jamii katika kutoa elimu na hamasa kwa nia hiyo.

“Moja wapo ya vitu ambayo tulitegemea kuvifanya katika huu mradi ni kujengea uwezo vyombo vyetu vya habari kushiriki kikubwa ni kutoa elimu kwa jamii na watoto  na shule zetu za msingi na sekondari ili waweze kupata ulekewa juu ya ukatili ni nini kwa sababu kuna wengine hawalewei hat, tumeoata nafasi ya kutoa elimu kwa shule zote za serikali za msingi na sekondari  zilizopo ndani ya jiji la Tanga  na tumeweza kuafikia wanafunzi Zaidi ya elfu sitini na shule 108” alisema Bwire

Alisema kufwatia mradi huo mara baada ya kufanya ufwatiliaji katika jamii imeonekana wazazi wamekuwa wakishiriki kwa kiasi kikubwa kuchochea ukatili kwa watoto baadhi yao wakiwashinikiza wanafunzi wa kike wasifaulu mitihani yao ili waweze kuwaozesha hali ambayo inaweza kupelekea skuzima ndoto ao kielimu.

“Kabla ya mradi tulianza kutaka kujua hali ya ukatili katika jamii ndani ya jiji la Tanga ipoje na hali tulitoipata ni kwamba hali yenyewe sio nzuri watoto wengi wanapitia  kwenye ukatili na hasa watoto 16 ambao walishafanya mtihani wa darasa la saba wanasema hawako tayari kwa sababu wameshaposwa wazazi wao wamewaambia maksudi wasifanye vizuri katika mitihani yao ili waweze kuolewa  na wengi wanaowafanyia ni ndugu wa karibu , wapo walimu pia wanatemnea na wanafunzi hizi taarifa” aliongeza.

Alisema bado katika jamii kuna visa vingi vya ukatili havijaripotiwa mahali husika hivyo kupitia wanahabari itkuwa ni njia moja wapo ya kuweza kuviibua na kuvitafutia ufumbuzi ili sheia ziweza kuchukuwa mkondo wake na kunusuru kundi kubwa watoto ambao ni kizazi kijacho.

Akifungua semina hiyo itakayofanyika kwa siku nne mstahiki meya wa jiji la Tanga  Abdurhaman Shillow amewahimiza wazazi kujua na kutmbua majukumu yao katika malezi ya watoto kila siku kujenga ukaribu baina yao na wazazi ili iwe rhisi kutambua matatizo wanayokumbana nayo na kuyapatia ufumbuzi mapema

Aidha amewataka waaandishi wa habari kutumia taaluma zao katika kuuga mkono jitihada za serikali kupitia wadau mbalimbali  kuweza kupambana na vitendo vya ukatili kwa kutoa taarifa kwenye vyombo vinavyohusika ili sheria ziweza kuchukuliwa kwa wale wote wanaootekeleza vitendo hivyo

“Mkikaa kwenye semina hii vaeni viatu vya matatizo yanayoikumba jamii kuna vishawishi vingi vijatumika kuwapelekea watoto wetu kuingia katika ukatili wa kijinsia kuna watu sasa hivi wanajirahisisha sana na wanapenda vitu vya bure  ikiwemo hali ngumu ya kiuchumi  matokeo yake matukio ya ukatili yamezoeleka na yamekuwa kama ni kitu cha kawaida  kitu kingine ni utandawazi ambao ukiutumia vibaya utakuangusha sasa tujitafakari na kuwaelimisha watu”

“Ni lazima wazazi wawe na wasiwasi na watoto wao wasiwaache tu kama kondoo wasio na mchungaji ni lazima wawe makini wafwatilie mienendo  na kujua marafiki wa  watoto wao kila siku  lakini wachukue tahadhari kwa mienendo na hulka za watoto wao, lakini pia wazazi  tuache vitisho kwa watoto wetu mtoto naweza akashindwa kukuambia vitu vingine lakini kwa sababu umemtisha anashishwa kuja kukuambia sasa ni lazima kuwa karibu kwa kujenga urafiki na watoto wetu” alisema Shillow.

Akizungumza mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Tanga Lulu George ametaja maendeleo ya teknolojia kuwa chanzo mojawapo kinachochangia kwa kasi kukithiri kwa vitendo vya ukatili wakijinsia katika jamii akiwataka waandaandshi wa habari kuzidi kusimama imara katika tathnia yao pamoja na kuandika taarifa zenye weledi ili kuweza kusaidia kupunguza na kuondoa kabisa ukatili wa kijinsia huku akiwaomba wadau na serikali kwa ujumla kutokulisahau kundi hilo katika Nyanja zote za kimaendeleo kwa aajili ya maslahi mapana ya Taifa.

“Hali mbaya zaidi inazidi sasa hivi tunapoona teknolojia imebadilika japo kuwa inaleta maendeleo kwa jamii lakini kwa kasi kubwa inazidisha mmomomyoko wa maadili na mwenye jukumu kubwa la kukemea hili ni sisi waandishi wa habari kwa kutumia vyombo vyetu vya habari kwahiyo tujione kuwa ni sehemu ya jamii ambayo tunapaswa na tunahuska kuleta mabadiliko tusimame katika nafasi zetu, lakini naomba waandishi wa habari,  tusiachwe nyumba kwaajili ya mabadiliko yanayohusu ndani ya jiji la tanga  kuwe na ushirikishwaji ili wote kwa pamoja tuweze kushirkiiana na kuleta yale mabadiliko chanya kwa maslahi mapana ya jiji letu la Tanga na mkoa wetu kwa ujumla”

 

 

 

 

Share To:

Post A Comment: