Mnufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Said Kiwamba kutoka Kitongoji cha Chahua ambaye anafuga kuku wa kienyeji akiwaingiza kuku kwenye banda lao.
Mnufaika Said Kiwamba wa Kitongoji cha Chahua ambaye anafuga kukuwa kienyeji akiwa mbele ya nyumba yake.
Mume wa Mnufaika wa TASAF, Saina Rufubwa akiwa kwenye genge lao ambalo wanauza bidhaa mbalimbali baada ya kuwezeshwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii.
Mnufaika wa TASAF,  Fatuma Mohamed Pononga ambaye ni mfugaji wa kuku akiwahudumia kuku wake.
Mnufaika wa TASAF,  Fatuma Mohamed Pononga ambaye ni mfugaji wa kuku akiwaangalia kuku wake.
Bibi Mwajabu Mrisho mnufaika wa TASAF wa Kijiji cha Saleni ambaye anajishughulisha na ufugaji wa mbuzi akiwaangalia mbuzi wake bandani.
Bibi Mwajabu Mrisho mnufaika wa TASAF wa Kijiji cha Saleni ambaye anajishughulisha na ufugaji wa mbuzi akiwahudumia mbuzi wake.

 Bibi Mwajabu Mrisho mnufaika wa TASAF wa Kijijicha Saleni ambaye anajishughulisha na ufugaji wa mbuzi akiwa mbele ya nyumba yake. 

Na Dotto Mwaibale, Chalinze, Pwani

JUMLA ya Kaya nne katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze mkoani Pwani zimepata matokeo chanya baada ya kuwezeshwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwa kupewa Sh.Milioni 2 kwa ajili ya ufugaji wa kuku na kufanya biashara ndogondogo.

Wanufaika wa mfuko huo watatu kutoka Kitongoji cha Chahua na mmoja wa Kijiji cha Saleni wakizungumza kwa nyakati tofauti leo Novemba 2, 2022 walielekeza shukurani zao kwa Rais Samia Suluhu Hassan na TASAF katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze kwa msaada huo mkubwa uliobadilisha maisha yao.

Mnufaika Said Kiwamba wa Kitongoji cha Chahua ambaye anafuga kuku wa kienyeji anasema anamatarajio makubwa baada ya kuwezeshwa Sh.250,000 kwa awamu ya kwanza ambapo alinunua kuku 20 ambao wamekuwa vizuri na sasa wameanza kutaga mayai.

"Nategemea kupiga hatua kubwa ya maendeleo kwani matunda ambayo yametokana na fedha za awali Sh.250,000 nilizopewa na TASAF nimeyaona na siku mbili zilizopita nimepewa tena Sh.250,000 jumla ni Sh.500,000 fedha hizi zinanipeleka katika maendeleo mengine zaidi nashukuru sana TASAF" alisema Kiwamba.

Kiwamba anasema kutokana na fedha alizozizalisha kwa ufugaji zinamsaidia kusomesha watoto na matarajio yake ni kuendelea kufuga kuku wengi ili aweze kubadilisha maisha yake kwa kujenga nyumba ya kisasa.

Mnufaika mwingine wa kitongoji hicho Zaina Rufubwa ambaye anafanya biashara ya genge anasema sijui hali ya maisha na familia yake yangekuwaje bila uwezeshaji huo wa TASAF kwani imewabadikisha mno kupitia fedha walizopewa kupitia Rais Samia Suluhu Hassan.

"Famailia yetu imekuwa na furaha sana na ari ya kukuza genge letu lenye bidhaa mbalimbali ambalo linatoa huduma kwa jamii iliyopo katika kitongoji hiki" alisema Rufubwa.

Rufubwa alisema matarajio yao ni kukuza mtaji waliopewa ili wawe na duka badala ya genge kwa kuwa tayari tena wamepokea Sh.250,000 kutoka TASAF na kuwa hivi sasa hata uhakika wa kupata chakula, mavazi na mahitaji mengine ni mkubwa mno ukilinganisha na hapo awali.

Mnufaika wa TASAF wa kitongoji hicho Fatuma  Pononga alisema ndoto zake ni kuendeleza ufugaji hadi awe mfugaji mkubwa na baada ya hapo ajenga nyumba kubwa ya kisasa na kununua gari litakalokuwa likimrahisishia kazi katika shughuli yake ya ufugaji.

Bibi Mwajabu Mrisho mnufaika wa TASAF wa Kijiji cha Saleni ambaye anajishughulisha na ufugaji wa mbuzi baada ya kupewa Sh. 216,000 awamu ya kwanza ambapo alinunua mbuzi wanne anasema licha ya ufugaji huo kuwa na changamoto za hapa na pale hawezi kuacha kwa sababu matunda yake ameyaona.

"Naishukuru sana TASAF na Rais Samia, mwanzo nilikuwa na mbuzi niliokuwa nawafuga baada ya kuwezeshwa na wadau wengine nikiwa na wenzangu kutokana na ujane wetu lakini TASAF ndio walikuja kuniongezea nguvu kwa kunipa fedha hizo na kuongeza mbuzi wanne" alisema Bibi Yusuph.

Alisema matamanio yake ni kuona anakuwa mfugaji mkubwa wa mbuzi ndani ya kijiji hicho na nje na kuwa amekuwa akitembelewa  na jamii ya wafugaji wa kimasai ambao wanampa mbinu mbalimbali akiwepo mwangalizi wake ambaye ni mratibu na mshauri wa masuala ya ufugaji kutoka Ofisi ya Afisa Mtendaji wa Kata  ya Lugoba.

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: