Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii Mhe. Ally Makoa (MB) wakati akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Chabima Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro.


Mwenyekiti wa kamati ya Maliasili ya Kijiji cha Chabima Bwana Iddy Tangula akifafanua kwa Wabunge ramani ya matumizi bora ya ardhi ya Kijiji, Vitalu vya uvunaji na namna utaratibu wa uvunaji unavyofanyika.
Mkurugenzi Msaidizi wa Shirika la Kuhifadhi Misitu ya asili Tanzania (TFCG) bwana Charles Lyimo akieleza namna vijiji pia vinavyoweza kunufaika na uuzaji ya hea ya Kaboni.

  1. Meneja wa Mradi Mradi wa kuleta mageuzi katika ya mkaa Tanzania (TTCS) Charles Leonard akitoa maelezo kwa Wabunge wakiwa kwenye moja ya Kitalu cha Uvunaji.
Afisa Ulaghabishi wa Mtandao wa Jamii wa usimamizi wa Misitu Tanzania (MJUMITA) Bi. Elida Fundi akimpa akifafanua jambo kwa  Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii Mhe. Ally Makoa.
  1. Afisa habari na Mawasiliano wa Shirika la kuhifadhi Misitu ya asili Tanzania (TFCG) Bettie Luwuge akitoa ufafanuzi mbele ya kamati ya Bunge walipotembelea mradi huo.
Wananchi wakiwa kwenye ziara hiyo,
Ziara ikiendelea.
Ziara ikiendelea.
Wananchiwakiwa kwenye ziara hiyo.
 Matukio mbalimbali wakati wa ziara hiyo ya  Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii kijijini hapo.

Na Calvin Gwabara, Kilosa 

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii imewataka Wananchi kwenye vijiji Vinavyotekeleza Mradi wa Usimamizi shirikishi wa Misitu ya Vijiji kuunga Mkono kwa dhati jitihada za Mashirika ya TFCG na MJUMITA kwa kukomesha kabisa vitendo vya Uchomaji misitu ya vijiji ili waweze kuendelea kunufaika na rasilimali hizo vizazi na vizazi.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii Mhe. Ally Makoa (MB) wakati akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Chabima Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro wakati wa ziara ya kamati hiyo ilipotembelea na kujionea na kujifunza namna Shirika la kuhifadhi misitu ya asili Tanzania (TFCG) na Mtandao wa jamii wa usimamizi wa Misitu Tanzania (MJUMITA) Wanavyotekeleza Mradi wa Usimamizi shirikishi wa misitu ya Jamii (USMJ) chini ya Mradi wa kuleta mageuzi katika ya mkaa Tanzania (TTCS) inavyofanya kazi na kulinda misitu huku ikinufaisha jamii.

“Tumeona kazi kubwa ya kutoa elimu ya utunzaji na usimamizi wa misitu ya jamii iliyofanywa na wadau hawa lakini kiukweli bado kuna wimbi kubwa sana uchomaji wa misitu katika wilaya ya kilosa kwenye njia ambayo tumepita tukija kijijini kwenu, Miradi hii itakuwa na maana zaidi kama Wananchi mtashiriki kikamilifu katika kuzuia mioto hii tuliyoiona njia nzima maana inaharibu kabisa malengo ya Mradi na Serikali katika kutunza misitu hii muhimu kwa ustawi wa Taifa letu”alisema Mhe. Makoa.

Amesema kwakuwa wanatambua kuwa Wafugaji ndio wanaochoma moto ameitaka kamati ya Maliasili ya Kijiji kuongeza juhudi katika kufanya doria za kila mara na kila siku kwakuwa fedha zinazopatikana katika biashara ya misitu inatoa fedha za ulinzi kwa kamati kutekeleza majukumu yake vizuri hivyo nao wafanye kazi zaidi ili kutokomeza kabisa changamoto hiyo.

Akizungumzia faida ya kuwa na misitu hiyo ya vijiji amesema kuwa inachangia wao kupata hewa safi, Mvua ambayo inawezesha wakulima kulima lakini pia mbao na mazao mengine ya misitu yaliyovunwa kwa njia endelevu yanachngia katika kuboresha huduma muhimu za jamii inayozunguka misitu hiyo.

Akileza mbinu hiyo inavyofanya kazi huku akijibu baadhi ya maswali ya Wabunge Meneja wa Mradi huo Charles Leonard mfumu huo unatelezwa baada ya tafiti nyingi zilizofanywa kwenye nchi mbalimbali na kuonekana kufanya vizuri nchini Zambia ambapo jamii zimeweza kutunza misitu baada ya kupata faida kwa mtu binafasi,Vijiji na Serikali na tofauti na maeneo mengine ambayo jamii inaona misitu ni mali ya serikali tu.

Akijibu swali la uwekano wa uchipuaji wa miti ianyokatwa amesema mfumo huo unafanya vizuri kwenye miti jamii ya Miyombo na huchipua kwa haraka katika maeneo matatu ambayo ni kupitia pembeni mwa kisiki,Misizi na mbegu kuota baada ya miti mikubwa iliyokatwa kuondoa kimvuli na kuruhusu mwanga wa mbegu kuota.

Bwana Leonard amesema Mradi hauishii kwenye kutekeleza kwa maneno tuu bali una programu nzuri ya ufuatiliaji wa uchipuaji wa miti hiyo kwenye vijiji vyote 41 ambayo inafanywa kwa kushirikiana na watafiti Kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha kilimo SUA kupitia Ndaki yake ya Misitu pamoja na Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania TAFORI ambao hutoa mapendekezo na ushauri wa namna bora ya utekelezaji na uboresjhaji wa mfumo huo ingawa takwimu za mwaka jana zimeonesha zaidi ya asilimia 88 mfumo umefanya vizuri.

Kwa upande wake Mkurugenzi msaidizi wa TFCG bwana Charles Lyimo amesema Vijiji hivyo havitaishia kunufaika na Mkaa,Mbao na mazao mengine lakini pia vitaweza kupata faida kwenye uuzaji wa hewa ya kaboni kwakuwa miti mipya inayochipua itakuwa na uwezo zaidi wa kuvuta hewa hiyo kuliko miti ya miaka mingi iliyozeeka.

“Mwaka 2008 tulikuwa tunatekeleza miradi 9 ya MKUHUMI kwenye Wilaya takribani 7 kuliwezesha taifa kujiandaa kunufaika na uuzaji wa hewa ya Ukaa na badae mkutano mmoja wa COP mataifa kadhaa yalishindwa kukubaiana katika ununuzi wa hewa hiyo na kupelekea changamoto na kushuka kwa progamu hiyo lakini kupitia Kaboni Tanzania ikaja ya Kiteto a Rukwa na Katavi na sasa Serikali imetengenza kanuni ambazo sasa hata vijiji hivi vitanufaika” alifafanua Bwana Leonard.

Wakieleza namna walivyonufaika na Mradi huo Afisa mtendaji wa Kijiji kwa niaba ya Wananchi wa Kijiji cha Chabima Bi Marrygoleth Mlengeni amesema Mradi ulianza mwaka 2017 lakini awali mwaka 2011 mradi wa MKUHUMI uliwezesha  kutengeneza mpango wa matumizi bora ya ardhi katika Kijiji chao kwa kupanga maeneo ya mkazi,Kilimo,Misitu,ufugaji na hivyo kusaidia katika usimamizi wa ardhi.

Amesema kupitia Mradi wa Mkaa endelevu wameweza kusimamia vyema misitu ya vijiji na kuwezesha kununua vifaa kama vile Pikipiki kwaajili ya kufanya doria huku Fedha hizo zikisaidia kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kijijini hapo ikimo Zahanati,Uchimbaji wa Choo cha Hospitali na kulipia bima ya fya CHF Iliyoboreshwa kwa watu 100 kijijini hapo.

“Changmoto kubwa tunayokumbana nayo katika kuteleza mradi huu ni namna ya kudhibiti moto kichaa unaochoma misitu ya hifadhi ya vijiji, Mifugo kwenye misitu tunayoihifadhi na changamoto za migogoro ya Wakulima na wafugaji” alifafanua Bi. Mlengele.

Shirika la kuhifadhi Misitu ya asili Tanzania (TFCG) na Mtandao wa jamii wa usimamizi wa Misitu Tanzania (MJUMITA) kwa pamoja Wanavyotekeleza Mradi wa Usimamizi shirikishi wa misitu ya Jamii (USMJ) chini ya Mradi wa kuleta mageuzi katika ya mkaa Tanzania (TTCS) kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la uswiss (SDC).

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: