Na Fredy Mgunda,Iringa.


Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dk Pindi Chana amevutiwa na ubunifu na mawazo  mazuri yaliofanywa na Shamba la Serikali Sao hili kwa kuandaa Mashindano ya mbio za Magari katika msitu huo kwani ni fursa kubwa ya kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo kwenye Shamba hilo.


Balozi Dk Chana ameyasema Hayo wakati akizungumza kwa njia ya simu katika Mashindano  Sao Hill Misitu auto Cross Tanzania the Royal Tour kwa kushirikiana Iringa Motorsports club Tanzania kwa ubunifu huo kwani unaumuhimu mkubwa katika masuala mazima ya kutangaza utalii.


" Haya nimaelekezo ya Rais wetu Samia Suluhu Hassan ambaye alituelekeza kuendelea kubuni vyanzo mbalimbali vya utalii kwani ndio chanzo kimoja wapi katika masuala mazima ya utalii wa aina hiyo wa mashindano ya mbio za mahari au Rally katika misitu yetu ambavyo tunaihifadhi mwenye maeneo yetu ." Alisema dk  Balozi Chana



Aidha alieleza Mkakati wa wizara ni kunatukio masuala ya michezo mbalimbali  ambayo utafanyika  katika maeneo ya hifadhi za Serikali ikiwemo msitu katika eneo la Sao hill.


" Ni jambo zuri na tuendelee kuratibu ili liweze kufanyika mara kwa mara  kadiri Kamati ya maandalizi tutakavyo amua I'll kupata washiriki wengi zaidi." Alisema Waziri huyo



Kwa upande wake Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Sao hill Lucas Sabida alisema wameandaa mashindano mafupi ya mbio za mahari lakini wanampango wa kuandaa mashindano makubwa zaidi.


Alisema lengo la mashindano Hayo ni kuendelea kujitangaza kama Shamba la TFS kwa ajili  kutangaza utalii wa ikolojia na nyuki kupitia utalii wa michezo wa mbio za Magari kutokana na mwitikio kuwa mkubwa kwao Wananchi.


Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Saad Mtambule alisema kuwa wilaya hiyo inamisitu Msingi ambapo wanaziadi ya hekta 100,000 ambayo inatumiwa kwa ajili ya uzalishaji wa mbao pamoja na bidhaa zingine kama Marine boad, Mirunda  na nguzo za umeme.


Alisema mazao Hayo wamekuwa wakiyatumia na kuwasaidia kwa uchumi na mapato kwa mustakabali wa jamii  lakini kupitia Program ambayo ilianzishwa na Rais wa Jamhuria ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan  The Royal Tour.


Share To:

JUSLINE

Post A Comment: