Na Imma Msumba, Arusha

Mkuu wa Mkoa wa Arusha John Mongela amewataka viongozi wa dini kisiasa,machinga,bodaboda na mashirika yasio ya kiserikali kuendeleza ushirikiano wa kwenda kuhamasisha zoezi la sensa ya watu na makazi.

Mongela ameyasema hayo wakati wa Mkutano wake na wadau mbalimbali mkoani hapa walipokutana nao kwa ajili ya kuhamasihsa zoezi la sensa ya watu na makazi kwa mkoa wa Arusha.

Amesema kwamba zoezi la uhamasishaji wa sensa ya watu na makazi limeenda vizuri na kupokelewa vyema na jamii hivyo anaendelea kuwasihi viongozi wote kutoka na kwenda kuongeza hamasa kwa wananchi wanaotunzunguka ili zoezi  liweze kufanikiwa vyema.

“Kwenye madhehebu ya kiislam na mengine tutumie fursa hii pamoja na kazi kubwa iliyofanyika tutoke na twende kuongeza hamasa,basi tuombe kukumbushana ili tujue idadi yetu kwani kazi hii ya mwanzo ilikuwa ya matayarisho ya sensa hivyo twende kwenye kusimamia na kuweka hamasa ili zoezi hili lenyewe lifanikiwe”

Amesema kwamba zoezi la Sensa ya watu na makazi sio la siku litaanza tarehe 23 na litaenda hadi tarehe 29 ya mwezi wa nane,Lakini kuanzia tarehe 30 hadi tarehe 02 mwezi wa tisa ni madodoso na sensa ya jamii kimsingi wananchi watambue kuwa kwenye siku za sensa sio siku za mapumziko kazi zitaendelea kama kawaida.

Awali akiongea katika hafla hiyo ErickSongo Meijo Laigwanan kiongozi Mkuu wa kabila la Wamasai  amesema kwamba Taifa bila kufanya Sensa ni sawasawa na mtu kutembea usiku wa manane bila kuwa na mwanga lazima uwe na mwelekeo hivyo sensa ni dira ya maendeleo.

ErickSongo amesema kwamba sensa ni dira ya kuleta maendeleo ya watu vijijini na mijini hivyo wanahitaji madawa kwa ajili ya mifugo,Elimu,Maji,Barabara na Hospitali sambamba na watumishi  wa kada hizo bila kuhesabiwa hatuwezi kufikia malengo ya kimaendeleo tunayoyahitajia.

Kwa Upande wake Yunis Urasa Naibu Katibu wa Shirikisho la watu wenye Ulemavu Mkoa wa Arusha amesema kwamba wanaishukuru serikali kuweza kuwashirikisha katika uhamasishaji wa zoezi la sensa ya watu na makazi na pia wamepokea zoezi hilo la sensa na kwani watapata takwimu sahihi za watu wenye ulemavu kwa ajili ya maendeleo yao.  

Share To:

Post A Comment: