WAENDESHA pikipiki maarufu kama bodaboda na Bajaji Manispaa ya Morogoro wamefanya maandamano ya amani lenye lengo la kuhamasisha sensa ya watu na makazi katika  kuunga mkono juhudi za Serikali za kutambua idadi ya watanzania ili kuongeza maendeleo nchini.

 

Akizungumza katika tamasha hilo katibu wa kamati ya maandalizi ya tamasha la sensa  Bernad  Msangiya  amesema tamasha lina lengo la kuhamasisha jamii kuhusu sensa na kuwaomba wananchi na  watanzania wote kwa ujumla kuona umuhimu  wa sensa katika nchi  pia  kuweka uhusiano mzuri kati ya serikali, vyombo vya Dola na wananchi ili  kutambua bodaboda na bajaji ni usafiri Salam na wanapaswa kuaminiwa . 


Mratibu wa sensa ya watu na makazi Manispaa ya Morogoro Frank Ugwelo amesema kuwa  sensa itafanyika Kwa siku sita baada ya kuzinduliwa tareh 23 mwezi 8 Hivyo amewaomba wananchi kujiandaa kuhesabiwa na kutoa  ushirikiano  mzuri kwa makarani wa sensa.


Naye Mbunge wa Jimbo la Morogoro mjini Abdulaziz Abood amewapongeza bodaboda na bajaji Kwa kufanya tamasha la kuhamasisha wananchi kuhesabiwa pia amewaomba kuendelea kutunza amani na  kuendelea kushirikiana na serikali , vyombo vya Dola ili kutunza amani ya nchi.


Pia ameeleza kuwa sensa ina lengo la kutambua idadi ya watu , makazi ,Hali ya uchumi, jinsia , umri, ambapo itasadia serikali kufanya mipango ya kiuchumi itakayo inua uchumi wa wananchi na kuboresha huduma za kijamii. 


Naye Ally machela Mkurugenz manispaa ya Morogoro amewataka wananchi kujitokeza kuhesabiwa kwani sensa ya watu itasadia kuongeza maendeleo katika manispaa na kuwezesha  serikali  kuongeza huduma muhimu  zitakazo saidia wananchi. 


Pia amasema kama manispaa  imejianda kuhesabiwa kwani hamasa zimefanyika  na kuwaomba wananchi wote kushiriki katika sensa ya watu na makazi.


Hivyo katika kuazimisha tamasha  lenye kauli mbiu bodaboda na bajaji usafiri Salama tuko tayari kuhesabiwa  viongozi mbalimbali walishiriki ili kuunga mkono  katika kuhamasisha wananchi kuhesabiwa hapo agosti 23 mwaka huu.

Share To:

Post A Comment: