Na John Mapepele


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amekutana na msanii nguli kutoka Nigeria Jim  Iyke na kufanya mazungumzo ya mashirikiano katika kuandaa filamu za kimkakati za pamoja baina ya Tanzania na Nigeria 

Mazungumzo haya yamefanyika leo Juni 14, 2022 jijini Dodoma  ambapo wamekubaliana  kuwa na mashirikiano  kwenye filamu za kimkakati kwa faida za pande zote mbili.

Aidha,  Mhe. Mchengerwa amesema mashirikiano hayo yataifanya Tanzania kunufaika zaidi kwa kufanya kazi na manguli wa filamu wa Nigeria ambao wanawapenzi  wengi duniani.

Waziri Mchengerwa ametumia fursa hiyo kuwakaribisha watu mbalimbali duniani kuja kuwekeza  kwenye sekta ya Sanaa na Michezo.

Ameongeza kuwa kwa sasa  tayari imeshusha kodi ya zuio katika biashara ya filamu kutoka asilimia 15 hadi 10 ili kuyapa unafu
Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: