Watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma nchini ambayo kila mwaka hufanyika kuanzia tarehe 16 -23 Juni, Leo Juni 21,2022 wamejotokeza kuchangia damu na kufanya usafi katika Hospitali ya Uhuru iliyopo katika Wilayani Chamwino mkoani Dodoma.
Watumishi mbalimbali wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi,wakichangia damnu katika Benki ya Mpango wa Taifa wa Damu Salama katika Hospitali ya Uhuru iliyopo Chamwino Mkoani Dodoma ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma nchini ambayo kila mwaka hufanyika kuanzia tarehe 16 -23 Juni. 
Mbali na uchangiaji Damu katika Benki ya damu ya Mpango wa Taifa wa Damu Salama watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wameshiriki kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Uhuru iliyopo Chamwino Mkoani Dodoma, 
 ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma nchini ambayo kila mwaka hufanyika kuanzia tarehe 16 -23 Juni. 
Watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakishiriki kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Uhuru iliyopo Chamwino Mkoani Dodoma,  ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma nchini ambayo kila mwaka hufanyika kuanzia tarehe 16 -23 Juni. 

Watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakishiriki kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Uhuru iliyopo Chamwino Mkoani Dodoma,  ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma nchini ambayo kila mwaka hufanyika kuanzia tarehe 16 -23 Juni. 

Na Mwandishi Wetu

KATIKA kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma nchini ambayo kila mwaka hufanyika kuanzia tarehe 16 -23 Juni, Tume ya Taifa ya Uchaguzi imechangia damu na kufanya usafi katika Hospitali ya Uhuru iliyopo katika wilayani Chamwino mkoani Dodoma.

Watumishi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi wameshiriki utoaji wa damu ikiwa ni kuunga mkono jitihada za kuchangia damu ili kuokoa maisha ya wagonjwa, akina mama wajawazito na watoto.

Akizungumza mara baada ya kukamilika kwa zoezi hilo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Chamwino, Dkt. Abdul Pumzi amesema uhitaji wa damu katika hospitali zetu nchini ni mkubwa mno, hivyo amewapongeza watumishi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kujitoa kwao kwa kuchangia damu kama sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma.
Share To:

Post A Comment: