Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa (USEMI), Mhe. Abdallah Chaurembo akizungumza na walengwa wa TASAF wa Shehia ya Piki wakati wa ziara ya kikazi ya kamati yake iliyolenga kukagua utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ya kujenga uzio, kukarabati madarasa na ofisi katika Skuli ya Sekondari ya Piki Pemba.
Baadhi ya walengwa wa TASAF wa Shehia ya Piki wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa (USEMI), Mhe. Abdallah Chaurembo (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa ziara ya kikazi ya kamati hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ya kujenga uzio, kukarabati madarasa na ofisi katika Skuli ya Sekondari ya Piki Pemba.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa (USEMI), Mhe. Abdallah Chaurembo kuzungumza na walengwa wa TASAF wa Shehia ya Piki wakati ziara ya kikazi ya kamati hiyo Pemba.Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Sera, Uratibu na Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Hamza Juma akitoa akieleza manufaa ya mradi wa ujenzi wa uzio na ukarabati wa madarasa katika Skuli ya Piki kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa (USEMI) wakati wa ziara ya kikazi ya kamati hiyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ya kuboresha miundombinu ya skuli hiyo iliyopo Shehia ya Piki Pemba.
Mwonekano wa baadhi ya madarasa yanayokarabatiwa na TASAF katika skuli ya Piki, ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ya kuboresha miundombinu ya skuli hiyo iliyopo Shehia ya Piki Pemba.
Na Ahmed Mahmoud
Mhe. Chaurembo amesema
hayo wakati wa ziara ya kikazi ya kamati yake iliyolenga kukagua utekelezaji wa
maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mhe. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.
Dkt. Hussein Mwinyi ya kujenga uzio, kukarabati madarasa na ofisi katika Skuli
ya Sekondari ya Piki Pemba.
“Mama yetu Samia
Suluhu Hassan na Dkt. Hussein Mwinyi ndio walioielekeza TASAF kujenga uzio, kukarabati
madarasa, ofisi na stoo katika skuli hii ya Piki ili kuweka mazingira rafiki
kwa wanafunzi kupata elimu bora, hivyo kamati yangu imekuja kukagua utekelezaji
wa maelekezo hayo na imeridhika na hatua iliyofikiwa,” Mhe. Chaurembo
amefafanua.
Mhe. Chaurembo
ameongeza kuwa, kamati yake iliidhinisha nyongeza ya fedha kwa TASAF baada ya
Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kuelekeza madarasa ya Skuli ya Piki kukarabatiwa
ambaye amedhamiria kuboresha miundombinu ya sekta ya elimu nchini.
Akiainisha kiasi cha
fedha kilichotengwa na kuidhinishwa kwa ajili ya utekelezaji wa maelekezo ya
Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, Mhe. Chaurembo amesema kiasi ya shilingi milioni
328 kimetolewa na Serikali kupitia TASAF na mpaka sasa ujenzi wa mradi uko
katika hatua nzuri kwani umefikia asilimia 85.
Kwa upande wake,
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Mhe. Deogratius Ndejembi amesema kuwa mradi wa ujenzi wa uzio na madarasa
katika Skuli ya Piki ni faida mojawapo ya muungano kati ya Tanzania Bara na
Zanzibar kwa sababu Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ni matunda ya muungano
na ndio maana ameambatana na kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali
za Mitaa (USEMI) kwa ajili ya ukaguzi wa mradi huo ambao Mhe. Rais ameelekeza
utekelezwe.
“Uwepo wa kamati hii
ya USEMI katika Shehia ya Piki ni taswira ya umoja wa taifa letu, ni taswira
ambayo inalindwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu
Hassan na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi
ambao wanapigania utekelezaji wa miradi ya muungano na taifa kwa ujumla,” Mhe.
Ndejembi amesisitiza.
Naye, Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Sera, Uratibu na Baraza la Wawakilishi
Zanzibar, Mhe. Hamza Juma amesema mradi huo wa ujenzi wa uzio na ukarabati wa
madarasa katika Skuli ya Piki ni matunda ya Muungano hivyo wanaoubeza Muungano
wanabeza maendeleo katika sekta ya elimu.
Mhe. Juma amesema
licha ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutekeleza miradi ya maendeleo
kupitia fedha zake, lakini inatekeleza miradi yenye sura ya muungano kwa
kutumia fedha zinazotoka kwenye bajeti ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania ukiwemo mradi huo wa ujenzi wa uzio na madarasa katika Skuli ya Piki
Pemba.
Wajumbe Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa (USEMI) imehitimisha ziara yake
yake ya kikazi ya siku moja mjini Pemba, iliyolenga kukagua utekelezaji wa maelekezo
ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF)
katika Shehia ya Piki na Kendwa.
Post A Comment: