Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida Mhe. Aysharose Mattembe ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo yalifanyika kimkoa wilayani Ikungi, akivikwa skafu na wanafunzi mara baada ya kuwasili viwanja vya Shule ya Msingi Mchanganyiko ya Ikungi kwa ajili ya kukabidhi zawadi mbalimbali na kuzungumza na wanafunzi hao ikiwa ni moja ya shughuli walioifanya kusherehekea Sikukuu hiyo jana.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida Mhe.Aysharose Mattembe akihutubia kwenye sherehe hiyo.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida  Mhe.Aysharose Mattembe (kulia) Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Mhe. Miraji Mtaturu (kushoto) na Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Mhe. Dorothy Mwaluko wakimkabidhi zawadi mwanafunzi wa shule hiyo.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida Mhe. Aysharose Mattembe (wa nne kutoka kushoto waliosimama ) akiwa katika picha ya pamoja na wanawake wenzake wakati wa maadhimisho hayo.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida Mhe. Aysharose Mattembe akiwa na Katibu Tawala  Mkoa wa Singida Mhe. Dorothy Mwaluko kwenye maadhimisho hayo.
Zawadi kwa wanafunzi zikitolewa.
Furaha kwenye maadhimisho hayo ikitamalaki.
Wanafunzi wakiwa kwenye sherehe hizo.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida  Mhe Aysharose Mattembe akikagua bidhaa za wajasiriamali alipotembelea mabanda yao kwenye sherehe hizo.
Ukaguzi wa bidhaa za wajasiriamali ukiendelea.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida Mhe.Aysharose Mattembe akiendeleakukagua bidhaa za wajasiriamali.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida Mhe. Aysharose Mattembe na Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Miraji Mtaturu wakikagua bidhaa za wajasiriamali walipotembeleanda yao.

 

Na Dotto Mwaibale, Singida

 

MBUNGE wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida Mhe. Aysharose Mattembe amewataka Viongozi Wanawake na wanawake wote wa mkoa huo  kuendelea kusimama imara, kujiamini kufanya kazi kwa bidii na weledi mkubwa ili  kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan ambaye anachapa kazi kwa bidii na kuonesha uwezo  mkubwa wa kuingoza nchi. 

Mattembe alisema hayo jana katika maadhimisho ya sikukuu ya Wanawake Duniani ambapo kimkoa yalifanyika Wilaya ya Ikungi. 

Mhe.Mattembe ambaye alikuwa mgeni Rasmi alisema Sikukuu hiyo  ni siku muhimu sana kwa kuwa ni mahususi kwa kutafakari, kutathmini, kutambua na kuthamini mchango mkubwa wa mwanamke katika nyanja mbalimbali hasa za maendeleo ya Taifa letu na dunia kwa ujumla. 

" Dhamira ya Rais wetu Samia Suluhu Hassan ni kutuletea maendeleo, kutuinua kiuchumi na  kuhamasisha wawanamke kuwa mstari wa mbele katika ujenzi wa Taifa letu" alisema Mattembe. 

Alisema Rais Samia Suluhu Hassana amefungua milango kwa Wanawake wengi akiwemo Dk.Tulia Ackson ambaye anaweka rekodi ya kuwa mwanamke wa pili kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Dk. Stegomena Tax ambaye anaweka rekodi ya kuwa Waziri wa kwanza  Mwanamke wa Wizara ya Ulinzi. 

Mhe. Mattembe alisema Watanzania tuna kila sababu ya kumuunga mkono na kamwe tusimuangushe na kuwa fursa alizotufungulia tuzitumie vizuri na kufanya kazi kwa uaminifu mkubwa. 

Awali sherehe hizo zilitanguliwa na kupokea mchango na zawadi zilizotolewa na wadau mbalimbali kwa ajili ya kuwachangia watoto wenye mahitaji maalum wa Shule ya Msingi Ikungi Mchanganyiko. 

Akikabidhi michango hiyo Mhe. Mattembe   aliwashukuru wote waliochangia na kuwataka waendelee na moyo huo huo ambao ni Kampuni ya Shanta Mining, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Kanisa la Kiinjili la  Kilutheri Tanzania (KKKT) la Ikungi, AMREF, Halmashauri ya wilaya ya Ikungi, UN Women na Ofisi ya Mbunge Aysharose Mattembe. 

Pia katika sherehe hizo Mhe. Mattembe alitembelea mabanda ya wajasiriamali na mengine na kujionea bidhaa zinazozalishwa ambalo aliahidi kushirikiana nao na kuwatafutia masoko. 

Kwenye sherehe hizo baadhi ya viongozi mbalimbali walihudhuria walikuwepo wa Chama na Serikali akiwepo Mbunge wa Jimbo la Singida  Mashariki Mhe.Miraji Mtaturu, Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida (RAS) Doroth Mwaluko, Katiba wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa  wa Singida Lucy Shee, Katibu wa CCM Wilaya  ya Ikungi Stamili Dendego,  Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Jonathan Semmit, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ally Mwanga, Diwani wa Kata ya Ikungi Abel Nkuhwi, Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Ikungi Haika Masawe, Katibu Tawala wa wilaya hiyo Winfrida Funto na madiwani wa Viti Maalumu wa wilaya hiyo.

 

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: