Meneja wa TARURA Wilaya ya Kilindi Mhandisi Martin Mwashambwa, akisoma bajeti ya TARURA mbele ya Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi. (Picha na Yusuph Mussa).
Mkandarasi akiwa kwenye hatua za mwisho za kukamilisha barabara ya Bokwa -Lengatei kipande cha lami chenye urefu wa mita 400. Barabara hiyo ni ya urefu wa kilomita 5.1 kutoka Kata ya Bokwa Wilaya ya Kilindi hadi Kata ya Lengatei, Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara. Lakini kwa kuanzia wamejenga mita 400 katika Mji wa Songe yalipo Makao Makuu ya Wilaya ya Kilindi. (Picha na Yusuph Mussa).
Hiyo ni barabara inapita kata ya Kilwa vijiji vya Tamota, Kilwa, Majengo, na Kwadundwa. Pia inapita kata ya Lwande vijiji vya Lwande, Lulago na Kwamfyomi katika Wilaya ya Kilindi. Barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 33.7 ambayo imetengenezwa kwa kiwango cha changarawe na TARURA, ni muhimu kwa wakulima na wafanya biashata sababu huko wanalima ndizi, Iriki, pilipili manga, magimbi , karafuu na mahindi, na kusafirishwa Handeni, Korogwe na mikoa ya Dar es salaam, Kilimanjaro na Arusha. (Picha na Yusuph Mussa).
Mahindi na iliki kutoka Kata ya Kilwa na Lwande wilayani Kilindi. (Picha na Yusuph Mussa). |
Na Yusuph Mussa, Kilindi
MADIWANI
wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi mkoani Tanga kwa kauli moja
wamepitisha bajeti ya Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA)
baada ya kuridhika na namna watakavyotengeneza barabara, kuweka
makalavati na madaraja.
Ni
baada ya TARURA Wilaya ya Kilindi kutengewa sh. bilioni 1,039,153,784
kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kwa ajili ya matengenezo ya barabara ya
kawaida, sehemu korofi, muda maalumu na madaraja na kalavati.
Akisoma
bajeti hiyo juzi Februari 2, 2022 kwenye kikao cha Baraza la Madiwani
wa Halmashauri hiyo, Meneja wa TARURA Wilaya ya Kilindi Mhandisi Martin
Mwashambwa alisema fedha za matengenezo ya barabara ya kawaida ni sh.
milioni 91.4, ambazo zinatarajiwa kufanya matengenezo ya kilomita 17.80.
Mhandisi
Mwashambwa alisema matengenezo ya barabara sehemu korofi ni sh.
milioni 342.6 jumla ya kilomita 3.98, matengenezo ya muda maalumu sh.
213,790,000 kilomita 29.70, madaraja mfuto 13 na makalavati mistari 15
zimetengwa sh. 290,720,000, na Usimamizi na Ufuatiliaji ni sh.
100,640,000.
"Pia
sh. 1,381,000,000 (nje ya bajeti) ni za utekelezaji wa Mfuko wa
Barabara miradi ya maendeleo, sh. milioni 500 ni utekelezaji wa barabara
miradi ya maendeleo fedha za nyongeza (Jimbo), na sh. bilioni moja ni
utekelezaji wa barabara miradi ya maendeleo fedha za tozo za mafuta"
alisema Mwashambwa.
Fedha
za Mfuko wa Barabara kwa matengenezo ya kawaida barabara za Mkusanyo,
Muungano- Kilindi- Kimbe kilomita 17 sh. milioni 76.9, Darajani mita 500
sh. milioni 6.5, Kanisa la Pentecoste mita 300 sh. milioni nane (8),
jumla ndogo sh. milioni 91.4.
Matengenezo
Barabara za Mjazo sehemu korofi, Stendi Kwamadoti mita 28 sh. milioni
241.5, Sambuche kilomita moja sh. milioni 22, Sophia mita 500 sh.
milioni 32, na Mtambo kilomita 2.2 sh. milioni 47.1, jumla ndogo sh.
milioni 342.6.
Matengenezo
ya muda maalumu Mafisa- Huyaga 6.2 sh. milioni 28, Muungano- Kimbe-
Tamota- Vyadigwa kilomita 13 sh. milioni 70, Kibirashi- Gombero-
Komhingo kilomita 10 sh. milioni 91.2, na Sekondari ya Mafisa mita 500
sh. milioni 24.5 jumla ndogo sh. 213,790,000.
Mwashambwa
alisema katika ukarabati na ujenzi wa madaraja mfuto, Mafisa- Huyaga
manane (8) sh. milioni 51, Muungano- Kimembe- Tamota- Vyadigwa sita sh.
milioni 114, Kibirashi- Gombero- Komhingo manane (8) sh. milioni 107.72,
na Shule ya Sekondari Mafisa Daraja Mfuto moja sh. milioni 18, jumla
ndogo sh. 290,720,000.
Mhandisi
Mwashambwa alisema kwa mwaka wa fedha 2021/2022, hadi kufikia Desemba
2021, wameweza kupokea sh. 250,174,888 kati ya sh. 1,039,153,784
zilizopangwa sawa na asilimia 24.07 kwa ajili ya matengenezo ya kazi za
barabara kutoka Mfuko wa Barabara. Fedha za tozo wamepokea sh.
83,268,423 kati ya sh. bilioni moja zilizopangwa, hiyo ikiwa ni sawa na
asilimia 8.32. Hakuna fedha ya Jimbo iliyopokelewa hadi Desemba 2021.
Mhandisi
Mwashambwa amebainisha changamoto kadhaa za wilaya hiyo katika
utekelezaji wa miradi. Na hiyo ni kulingana na jiografia ya wilaya hiyo
ambapo barabara nyingi hupita kwenye milima na mabonde makubwa, hivyo
zinahitaji matengenezo makubwa pamoja na ujenzi wa madaraja.
"Moja
ya ya changamoto ni uharibifu wa barabara unaosababishwa na mifugo, hii
inatokana na Wilaya ya Kilindi kuwa na mifugo mingi, na upungufu wa
vitendea kazi hasa magari, kwani mahitaji ni mawili, lakini lililopo
sasa ni moja.
"Katika
utatuzi wa changamoto, ni kuomba fedha kutoka vyanzo vingine vya fedha
mbali na Mfuko wa Barabara ili kutatua changamoto ya baadhi ya barabara
zinazohitaji matengenezo makubwa pamoja na ujenzi wa madaraja, kuendelea
kuiomba wizara kupitia Mfuko wa Barabara kuongeza fedha za bajeti ya
matengenezo ya barabara ili ziendane na hali halisi ya barabara na
urefu wa mtandao wake, kuwaelimisha wananchi kutunza barabara kwa
kutopitisha mifugo, na kuomba kuongezewa magari na vitendea kazi"
alisema Mwashambwa.
Post A Comment: