Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge akimjulia hali jana Mwanahamisi Shabani ambaye ni mjamzito mmoja wa wananchi ambaye amelazwa Hospitali ya Mkoa wa Singida akipatiwa matibabu akidhaniwa kula chakula kinachodhaniwa kuwa na sumu.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge akimjulia hali na kuzungumza na Sheikh wa Kata ya Unyambwa, Ramadhani Yusuf  (kulia) ambaye amelazwa  katika Hospitali hiyo akipatiwa matibabu akidhaniwa kula chakula kinachodhaniwa kuwa na sumu. Katikati ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishna Msaidizi (ASP) Stella Mutabihirwa.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge akiwajulia hali  wahanga wa tukio hilo alipo watembelea jana kabla ya kuruhusiwa..

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge akiwajulia hali  wahanga wa tukio hilo alipo watembelea jana kabla ya kuruhusiwa..

Wahanga wa tukio hilo wakiwa hospitalini hapo kabla ya kuruhusiwa.
Wahanga wa tukio hilo wakiwa hospitalini hapo kabla ya kuruhusiwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishna Msaidizi (ASP) Stella Mutabihirwa, akizungumza na madaktari wa Hospitali wakati mkuu wa mkoa alipo watembelea wahanga wa tukio hilo. 


Na Dotto Mwaibale, Singida 


WATU 50 waliokuwa wamelazwa Hospitali ya Mkoa wa Singida wakipatiwa matibabu baada ya kunusurika kufa baada ya kula chakula kinachodhaniwa kuwa na sumu wameruhusiwa kurudi nyumbani baada ya afya zao kuhimarika.

Akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge alipowatembelea wananchi hao jana Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Banuba Deogratius alisema juzi walipokea juzi jumla ya wagonjwa 50, Wanawake 34 na Wanaume 16 ambapo hali hadi jana hali zao zilikuwa zikiendelea vizuri na baadhi yao wameanza kuwaruhusu kurudi nyumbani kuendelea na majukumu yao ya ujenzi wa Taifa.

Banuba alisema wakazi hao wa Kata ya Unyambwa Kijiji cha Kisasida katika Manispaa ya Singida mkoani hapa walifikishwa hospitalini hapo  baada ya hali zao kuwa mbaya kutokana na kula chakula kilichoandaliwa katika shughuli za ufunguzi wa Madrasa moja Katika kijiji hicho.

Akipokea taarifa hiyo  Mkuu wa Mkoa Singida Dkt Bilinith Mahenge aliwapongeza madaktari wa Hospitali hiyo kwa jitihada walizozifanya za kuhakikisha wananusuru maisha ya wananchi hao ambapo kwa sasa hali zao zinaendelea vizuri na kuipongeza Serikali kwa kuweka miundombinu mizuri ya huduma katika sekta ya afya.

Alitoa wito kwa viongozi wa Serikali na Dini kuwajibika kikamilifu katika kutoa elimu ya namna ya kuandaa chakula pamoja na kusimamia inapotokea sherehe mbalimbali kwenye maeneo yao ili kuepuka madhara ya namna hiyo yasije kutokea tena.

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishna Msaidizi (ASP) Stella Mutabihirwa alisema wanawashikilia watu saba kuhusika na tukio hilo.

" Tuna walishiriki watu saba ambao waliandaa chakula hicho na  uchunguzi ukikamilika tutatoa taarifa kamili kwa sasa tayari tumechukua mabaki ya chakula hicho kwa ajili ya kuyachunguza," alisema Mutabihirwa.

Alisema katika tukio hilo  mtoto mmoja mwenye umri wa miaka (7) aliye mtaja kwa jina la Fahad Masoud alifariki dunia kabla ya kufikishwa hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: