Mkuu
 wa Mkoa wa Pwani Aboubakar Kunenge akizungumza na Wananchi wa Vijiji 
vya Manda na Mkange Chalinze Wilayani Bagamoyo leo Agosti 3,2021.
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
MKUU
 wa Mkoa wa Pwani Aboubakar Kunenge amekutana na Wananchi wa  Vijiji vya
 Manda na Mkange Chalinze Wilayani Bagamoyo, ambao wanalalamikia 
kutolipwa Fidia  baada ya kuwepo  Mchakato wa Ujenzi wa Barabara ya 
Afrika Mashariki, Makurunge, Saadani Tanga.
Kunenge
 ameeleza kuwa Awali Tathimini ya Fidia kwa Wanachi hao ilifanyika mwaka
 2019 na malipo yamefanyika kwa Wananchi  Pangani Tanga.
Jambo
 lilowatia hofu Wananchi hao ni kufanyika kwa Tathimini mpya ambayo 
fomula iliyotumika ni tofauti na ya mwaka 2019,hivyo kuwepo kwa 
Tathimini mbili kwenye mradi huo mmoja, na wakati huo huo Wananchi wa 
Vijiji Jirani wamelipwa kwa Tathimini ya awali.
"Mtalipwa
 Fidia kama walivyolipwa wenzenu wa Tanga, kwasababu ya Mazingira ya 
suala lenyewe kwamba Mradi ni mmoja Tathimini ilikwisha fanyika 
kilichofanya msilipwe kipindi hicho ni kukosekana kwa fedha" alisema 
Kunenge.
"Nimelichukua
 tutaenda kushauriana na Wizara fidia zilipwe kupitia vigezo 
walivyotumia kulipa wananchi wa Vijijini Jirani na kama inavyonekana 
kwenye Tathimini ya awali. Tutatumia hekima pia kutafutia ufumbuzi suala
 hilo alieleza Kunenge."vuteni subira suala hili 
tunalishughulikia"alisisitiza Kunenge.
 
Post A Comment: