Mkuu
wa Mkoa wa Pwani Aboubakar Kunenge akizungumza na Wananchi wa Vijiji
vya Manda na Mkange Chalinze Wilayani Bagamoyo leo Agosti 3,2021.
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
MKUU
wa Mkoa wa Pwani Aboubakar Kunenge amekutana na Wananchi wa Vijiji vya
Manda na Mkange Chalinze Wilayani Bagamoyo, ambao wanalalamikia
kutolipwa Fidia baada ya kuwepo Mchakato wa Ujenzi wa Barabara ya
Afrika Mashariki, Makurunge, Saadani Tanga.
Kunenge
ameeleza kuwa Awali Tathimini ya Fidia kwa Wanachi hao ilifanyika mwaka
2019 na malipo yamefanyika kwa Wananchi Pangani Tanga.
Jambo
lilowatia hofu Wananchi hao ni kufanyika kwa Tathimini mpya ambayo
fomula iliyotumika ni tofauti na ya mwaka 2019,hivyo kuwepo kwa
Tathimini mbili kwenye mradi huo mmoja, na wakati huo huo Wananchi wa
Vijiji Jirani wamelipwa kwa Tathimini ya awali.
"Mtalipwa
Fidia kama walivyolipwa wenzenu wa Tanga, kwasababu ya Mazingira ya
suala lenyewe kwamba Mradi ni mmoja Tathimini ilikwisha fanyika
kilichofanya msilipwe kipindi hicho ni kukosekana kwa fedha" alisema
Kunenge.
"Nimelichukua
tutaenda kushauriana na Wizara fidia zilipwe kupitia vigezo
walivyotumia kulipa wananchi wa Vijijini Jirani na kama inavyonekana
kwenye Tathimini ya awali. Tutatumia hekima pia kutafutia ufumbuzi suala
hilo alieleza Kunenge."vuteni subira suala hili
tunalishughulikia"alisisitiza Kunenge.
Post A Comment: