MENEJIMENTI
ya mkali wa Rhumba Afrika, Fally Ipupa imetangaza kuahirisha Matamasha
mawili ya msanii huyo yaliyokua yafanyike Ijumaa ya Julai 23 na Jumamosi
ya Julai 24 mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyoolewa na
uongozi wa msanii huo kampuni ya Prime Time Promotions inasema ahirisho
la matamasha hayo mawili yaliyokua yafanyike jijini Dar es Salaam katika
Hoteli ya Serena na jijini Mwanza katika Hotel ya Elevate Malaika
yameahirishwa kutokana na changamoto zilizoshindwa kuepukika.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Maandalizi ya matamasha hayo, Edward Lusala ameomba radhi
kwa mashabiki wa muziki na msanii huyo nchini huku akieleza kuwa
utaratibu kwa walionunua tiketi tayari utatolewa.
" Menejimenti
ya Fally Ipupa, Prime Time Promotion na Clouds Media Group inachukua
nafasi hii kuomba radhi kwa wale wote ambao walikua wametenga ratiba yao
ili kuwa sehemu ya matukio haya. Tarehe mpya za show zitatangazwa
baadae.
Utaratibu kwa walionunua tiketi na kufanya booking ya
meza utafafanuliwa kwa mawasiliano kati yao na kamati husika," Amesema
Lusala.
Post A Comment: