Makamu Mkuu wa Chuo Mipango, Fedha na Utawala  wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania  (TIA)  Dkt. Modest Assenga, akisoma taarifa ya utekelezaji wa mipango na bajeti ya taasisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2021/2022 katika kikao cha tatu cha baraza kuu la nne la wafanyakazi wa taasisi hiyo kilichofanyika jana ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine  (SUA) mkoani Morogoro.

Meneja wa TIA Kampasi ya Mtwara, Criph Swallo, akichangia jambo kwenye kikao hicho.
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi (RAAWU) Mkoa wa Mbeya Martin Mnyili, akichangia jambo kwenye kikao hicho.
Picha ya pamoja ya washiriki wote wa kikao hicho.
 


Na Dotto Mwaibale, Morogoro


TAASISI ya Uhasibu Tanzania  (TIA) inaomba kuidhinishiwa  bajeti ya Sh.Bilioni 46.4 kwa mwaka wa fedha 2021/ 2022 ili iweze kutekeleza mipango yake.

Hayo yamebainishwa na Makamu Mkuu wa Chuo Mipango, Fedha na Utawala Dkt. Modest Assenga wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa mipango na bajeti ya taasisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Taarifa hiyo alikuwa akiitoa katika kikao cha tatu cha baraza kuu la nne la wafanyakazi wa taasisi hiyo kilichofanyika jana ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine  (SUA) mkoani Morogoro.

Dkt.Assenga alisema pamoja na mambo mengine kupitia bajeti hiyo wamepanga kuongeza udahili wa wanafunzi 24,866 ambapo katika kozi za cheti watakuwa 5,413, Diploma 9,267, Shahada 10,145 na kozi za Stashahada 40 jumla yao ikiwa ni 24,866.

" Mwaka huu wa fedha 2021/2022 TIA tumedhamiria kuendelea kuboresha utoaji wa elimu bora kwa kuajiri walimu wenye sifa, kuboresha huduma ya mtandao ili kuwawezesha wanafunzi kujipatia "study materials" mbalimbali, kuboresha huduma za maktaba, kuwapatia wanafunzi mazoezi, majaribio na mitihani pamoja na kuwadhamini wahadhiri wanaojiunga na kozi za "PhD." alisema Assenga.

Dkt.Assenga alitaja maboresho mengine kuwa ni kuongeza vifaa vya kufundishia, kuimarisha kitengo cha utafiti, ushauri na machapisho, kuunga ushirikiano wa kimataifa na kukuza uhusiano na taasisi zingine ili kuongeza maendeleo katika masomo, utafiti na ushauri na kuboresha na kuimarisha kitengo cha ICT na Takwimu kwa kuboresha huduma za ICT.

Assenga alisema katika mwaka  wa fedha wa 2021/2022 TIA imejipanga kukusanya jumla ya Sh.30,968,287,171 kutoka vyanzo vyake vya ndani na St.14,292,406,574.00 ikiwa ni ruzuku kutoka Serikalini, ambapo Sh.11,292,406,574.00 ni kwa ajili ya mshahara na Sh.3,000,000,000 ikiwa ni ruzuku kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Share To:

Post A Comment: