
Mabalozi
 wanaoiwakilisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nje ya Nchi 
wameelekezwa kujipanga, kushiriki na kutafuta fursa zitakazowezesha 
bidhaa mbalimbali za Tanzania kupata masoko ya uhakika katika nchi 
walizopo.
Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na 
Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi wakati 
akizungumza na mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi na kuongeza
 kuwa , Ilani ya Chama cha Mapinduzi inatamka bayana juu ya diplomasia 
ya uchumi sambamba na kuimarisha sauti ya Tanzania na taswira yake 
katika medani ya uhusiano wa kikanda na kimataifa. 
Prof. Kabudi 
ameongeza kuwa ili kufanikisha hilo Balozi zinapaswa kuimarisha ushiriki
 wa Tanzania katika jumuiya nyingine za kimataifa zikiwemo, Indian Ocean
 Rim Association, Indian Ocean Tuna Commission, South South Commission, 
South West Indian Ocean Fisheries Commission.
Aidha amewataka 
Mabalozi hao kuzingatia maelekezo ya Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi,
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi aliyoyatoa wakati
 akizundua Baraza la Wawakilishi ya kutaka Uchumi wa Bluu kupitia uvuvi 
wa Bahari Kuu unakuwa na manufaa kwa Wananchi hususani katika kuongeza 
mapato, ajira na kukuza uchumi kwa kuzingatia kuwa Wizara ya Mambo ya 
Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ni ya Muungano. 
Pia Prof.
 Kabudi amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango unaotolewa na 
Watanzania waishio nje ya nchi (Diaspora) katika maendeleo ya Taifa na 
kuzielekeza Balozi zianze na ziboreshe kanzi data ya Diapora ikiwa ni 
pamoja na kuwahimiza kuanzisha Jumuiya zao. 
“Natambua kazi hiyo 
inaendelea na kwa sasa tuna data za diaspora takriban 98,658 na kuna 
jumuiya 77 za diaspora. Nichukue fursa kusisitiza umuhimu wa Balozi zetu
 kuboresha na kuharakisha zoezi hili kwa kubuni njia mbalimbali za 
kuwaandikisha”. Amesema Prof. Kabudi
Mkutano huo wa Prof. 
Palamagamba John Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
 Mashariki na mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi umehudhuriwa
 pia na Naibu Waziri, Mhe William Tate Ole Nasha, Katibu Mkuu Brigedia 
Jenerali Wilbert Ibuge, Wakurugenzi na Wakuu wa Idara na Vitengo wa 
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Home
KIMATAIFA
Kitaifa
Mabalozi Wanaoiwakilisha Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Nje Ya Nchi Wahimizwa Kuongeza Juhudi Za Kufuta Masoko 
Post A Comment: