Na John Walter-Manyara
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa  wilaya ya  Kiteto mkoani Manyara  itawarejeshea kiasi cha shilingi milioni 2,050,000  wananchi wakiwemo wachungaji katika wilaya hiyo, waliotapeliwa na kampuni ya Namaingo Bussiness Agency Ltd iliyowahaidi kutoa mafunzo ya ujasiriamali na haikufanya hivyo tangu mwaka 2016.
Kaimu mkuu wa Takukuru mkoa wa Manyara Isdory Kyando amesema awali walipokea malalamiko ya wananchi 41 juu ya kutapeliwa na mwakilishi wa kampuni hiyo yenye ofisi zake jijini Dar es Salaam, ambaye aliwawahamasisha wananchi hao wajiunge kwenye vikundi kwa ajili ya kupatiwa mafunzo ya ujasiriamali ambapo kila mshiriki alitakiwa kutoa kiingilio cha shilingi 50,000.
Kyando amesema wananchi wote hao walichangia fedha hizo huku wakisubiri mafunzo hayo bila mafanikio ndipo walipoamua kufanya mawasiliano na mwakilishi na mkurugenzi wa kampuni hiyo Bwana Biubwa Ibrahimu bila mafanikio yoyote.
Kaimu mkuu wa Takukuru mkoa wa Manyara Isdory Kyando ameendelea kusema kuwa baada ya watu hao kuona wanapoteza haki zao waliamua kufika ofisi za Takukuru wilayani Kiteto kutoa malalamiko yao dhidi ya Biubwa Ibrahimu ambaye ni mkurugenzi wa Namaingo Business Agency Ltd.
Kyando amesema baada ya kufanya uchunguzi Bwana Biubwa alikiri kuchukua fedha hizo na kuahidi kuzirejesha na alitekeleza ahadi hiyo kwa kurejesha fedha zote shilingi milioni 2,050,000.





Share To:

Post A Comment: