Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga Charles Makoga akifunga kikao cha kupitisha bajeti ya Halmashauri
Madiwani wa Halmashauri ya Mji Mafinga wakipitia makisio ya bajeti kwenye kikao 


Baraza la madiwani la Halmashauri ya Mji Mafinga  mkoani  Iringa  limeidhinisha  makisio  ya bajeti ya shilingi milioni 24.9 kwa  mwaka  2020/2021  kwa  ajili ya  matumizi ya  mishahara  miradi mbali  mbali ya  kimaendeleo ikiwemo ya ujenzi wa barabara za  kiwango cha lami katika mitaa ya mji  wa Mafinga .

Kaimu afisa mipango wa Halmashauri   ya Mji Mafinga  Mashaka Mkongwa  akisoma  makisio ya bajeti  hiyo kwenye  kikao cha kuidhinisha bajeti    cha baraza la madiwani ya Mji Mafinga  jana  alisema  kuwa   kati ya  fedha   hizo mapato ya  ndani ya shilingi 4,613,800.100 makisia ya mapato  ya ndani  ni zaidi ya shilingi 638,721,000 ambayo ni sawa na asilimia 16.00  ukilinganisha  na makisio ya mwaka 2019/2020  ya  shilingi 3,975,079.100.

Pia  kwenye  mapato  hayo kiasi cha shilingi 798,493,500 ni mapato ya  vyanzo  fungiwa   katika idara ya afya  na elimu  sekondari  hivyo  kufanya mapato  halisia   kuwa ni  shilingi 3,815,315,306.600.

Hata  hivyo  alisema  kwa mwaka 2020/2021 jumla ya  shilingi 18,428,460.00  zimeombwa    kwa  ajili ya matumizi ya kwaida  na mishahara ,kati ya fedha  hizo  kiasi cha shilingi 14,757,136,020.00 ni kwa  ajili ya mishahara    na shilingi 3671,602,440.00 ni kwa ajili ya matumizi  mengineyo  na chanzo cha fedha   hizo ni makusanyo ya mapato ya ndani  na  serikali kuu  .

Aidha  alisema   katika mpango wa bajeti ya maendeleo  ya mwaka 2020/2021  Halmashauri  ya Mji Mafinga  inatarajia  kukusanya na kutumia kiasi cha shilingi 6,537,959,035.16 kwa  ajili ya  kutekeleza miradi ya maendeleo   fedha  zitakazotokana na vyanzo mbali mbali  na kati ya fedha   hizo  shilingi 4,431,302,708.16  ni toka  ruzuku  ya  serikali kuu ,wahisani ni shilingi 580,533,687 na  Halmashauri  itachangia  kiasi cha shilingi 1,526,122,640,00 sawa na asilimia 40 ya mapato halisi ya ndani .

Alisema  kuwa  kwa mwaka wa  fedha  2019/2020  Halmashauri  hiyo   iliidhinishiwa    kukusanya na  kutumia  kiasi cha shilingi 23,752,127 ikiwa shilingi  12,654,625,953.00 ni  za mishahara   ,kiasi cha shilingi 1,060,615,016.00 ni matumizi ya  kawaida   na kiasi cha shilingi 6,246,137,825.66 kwa  ajili ya miradi ya  maendeleo  kutoka  serikali  kuu na wafadhili .

Pia  kati ya fedha  hizo  Halmashauri  iliidhinishiwa  kukusanya na  kutumia  kiasi cha shilingi 3,975,079,100.00  kutoka   makusanyo ya mapato ya ndani  ambapo  kiasi cha shilingi 2,022,395,460 ni  kwa  ajili ya  matumizi ya  kawaida  sawa na asilimia 60 na kiasi cha shilingi 1,348,240 ni kwa  ajili  ya miradi ya  kawaida   sawa na asilimia 40 na kiasi cha shilingi  604,420,000.00 ni  mapato fungiwa .

Hata  hivyo  alisema hadi kufikia  Desemba 31 2019  jumla ya  shilingi 8,273 ,101,339.83  zimetumika sawa na asilimia 92.68 ya fedha zilizopokelewa  kwa  ajili ya matumizi  ya wakawaida ,mishahara  na miradi ya maendeleo  kuwa  kati ya  fedha  zilizotumika kiasi cha shilingi 5,759,191,620  ni  kwa  ajili ya mishahara  ,shilingi 431,411,732.43 ni matumizi mengineyo  na shilingi 818,155,448.49 ni miradi ya maendeleo .

Pia  alisema   wadau na wananchi    walichangia  kiasi cha shilingi 56,870,654.88 katika miradi   ya maendeleo  fedha  ambazo ziliweza kutekeleza miradi  mbali mbali na  wananchi  wenyewe .

Kupitia  bajeti  hiyo  wameweza  kuongeza ufaulu wa wanafunzi wa darasa la saba  umefikia asilimia 93 ambapo  wamekuwa  wa  pili  kimkoa na 17  kitaifa kwa  mwaka 2019 ,ujenzi wa jengo la utawala umekamilika  na kukamilika kwa   jengo hilo kutaboresha  utoaji wa huduma   za  kiutawala  kwa  wananchi .

Mkongwa  alisema kuwa  kumekuwepo na mafanikio makubwa  katika  utekelezaji wa  bajeti  kwa  mwaka 2019/2020  kwa  kipindi cha nusu mwaka  kwa maana ya Julai -Desemba 2019.

Akitolea  mfano wa mafanikio hayo alisema ni pamoja na  upatikanaji wa dawa  .vifaa tiba na vitendanishi  umeimarika  na kufikia asilimia 100 kwenye zahanati na vituo vya afya  na asilimia 97 kwa Hospitali .

Pia  Halmashauri  imeendelea  kufanya vizuri  katika   kusimamia ukusanyaji wa mapato ya ndani  kwa  kufikia asilimia 56 katika  kipindi cha nusu mwaka , hali ya  usafi wa  mazingira  katika Mji  imeboreshwa  na Halmashauri  imekuwa ya  mshindi wa  tatu  kitaifa  katika mashindano ya usafi wa mazingira .

Aidha  ujenzi wa  shule mpya ya sekondari  ya kata ya  Upendo umekamilika  na imepokea wanafunzi wa  kidato cha  kwanza mwaka2020  na imepata usajili  tayari ,ujenzi wa  soko la kuuzia mboga na matunda  lililopo  uwanja wa Mashujaa limepauliwa na linatumika  na  kiasi cha shilingi  161,093,599.94 zimetolewa na Halmashauri  kwa  ajili ya kuanza  mchakato wa  kukopesha vikundi  vya vijana ,wanawake  na walemavu sawa na asilimia 47.7 ya lengo  la kukopesha kiasi cha shilingi 337,065,910

Alisema  changamoto  kubwa  iliyojitokeza katika utekelezaji wa  bajeti   hiyo  ilikuwa ni  upungufu wa  watumishi  katika  idara  mbali mbali ,upungufu wa vitendea kazi  kama magari ,vifaa vya tiba ,samani  kuhusu magari  alisema magari mengi yaliyopo  ni chakavu na hayatoshelezi  idara  zote .

Akizungumza  baada ya  kupitisha  makisio hayo ya bajeti,mwenyekiti  wa Halmashauri ya  Mji Mafinga  Charles Makoga   alisema  kuwa  fedha   hizo zilizopitishwa zitaendelea  kuleta kasi kubwa ya maendeleo katika Halmashauri hiyo .

Huku  akiwataka  watumishi  wa umma katika halmashauri  hiyo  kwenda  kufanya kazi kuwatumikia  wananchi  ili  kufanikisha malengo ya Halmashauri  hiyo  badala ya kwenda kufanya kazi ya  siasa na kutaka  kuwakwamisha   wanasiasa  ili  wasichaguliwe  kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika  octoba  mwaka huu .



Share To:

Francis Godwin Mzee wa matukiodaima

Post A Comment: