Msanii wa vichekesho, Idris Sultan leo Ijumaa Novemba 1, 2019 saa 2 asubuhi ameripoti Kituo cha Polisi ‘Central’ jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya masharti ya dhamana aliyopatiwa jana October 31, 2019.

Idriss alitakiwa kwenda polisi baada ya kuweka picha yenye sura yake huku akiwa ameketi katika kiti chenye nembo ya Taifa na kuambiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuripoti kituo chochote cha Polisi.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: