Mamia ya washiriki wa Mkutano wa Mawaziri wa sekta ya Mazingira, Maliasili na Utalii kutoka nchi za SADC wamewasili katika Ukumbi wa Mikutano wa kimataifa Arusha (AICC) tayari kuanza mkutano huo ambao unatarajiwa kuhudhuriwa na Mawaziri wa sekta husika, wataalamu pamoja na wadau mbalimbali.

Mkutano ambao utafunguliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Tayari baadhi ya Mawaziri wameanza kuwasili akiwepo Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Hamis Kigwangalla, Naibu Waziri wa Wizara hiyo Constantine Kanyasu, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mussa Sima, pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara zinazohusika na mkutano huo.





Share To:

msumbanews

Post A Comment: