Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Evamaria Semakafu akizungumza wakati wa kufunga mkutano la wadau wa Elimu ya Ualimu kuhusu usimamizi na uendeshaji bora wa Elimu ya Ualimu uliofanyika Jijini Dar es Salaam.
Wadau wa Elimu ya Ualimu wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Evamaria Semakafu wakati akifunga mkutano wa wadau hao uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Mafunzo ya Ualimu Augusta Lupokela akizungumza wakati wa Mkutano wa Wadau wa Elimu ya Ualimu ambapo amesema matokeo ya Mkutano huo yatasaidia katika maandalizi ya mpango mkakati wa maboresho ya usimamizi wa mafunzo ya ualim uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Wamiliki wa Vyuo Binafsi Mahmood Mringo akitoa neno la wa Mkutano wa Wadau wa Elimu ya Ualimu kuhusiana uwepo na ushirikishwaji wa sekta ya elimu kwa maendeleo ya Taifa uliofanyika jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Evamaria Semakafu akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa mkutano wa wadau wa elimu ya ualimu baada ya kufungua mkutano huo jijini Dar es Salaam.
SERIKALI imesema kuwa walimu wa somo la Fizikia ni wachache na kutaka vyuo vya ualimu kuandaa walimu hao katika kwenda sambamba na malengo ya ya serikali.
Hayo ameseyasema Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolijia Dkt. Evamaria Semakafu wakati wa kufunga ya kuwa na mkutano wa Wadau wa Elimu ya Ualimu lililofanyika jijini Dar es salaam,amesema kuwa walimu wa hisabati na Kemia hakuna tatizo lilopo ni walimu wa somo la Fizikia.
Amesema kuwa serikali inafanya mikakati mbalimbali katika kuhakikisha suala elimu linakwenda kutokana na mdau kutambua nafasi yake kutekeleza sekta ya elimu nchini.
Dkt.Semakafu anasema kuwa serikali iko katika mchakato wa kuwa na bodi ya walimu ambao watakuwa wasimamizi maadili na weledi wa kufanya kazi hata ikitokea kuna ukiukaji wa weledi huo kuweza kuchukuliwa hatua.
“Kuwepo kwa bodi itaondoa wale wanaokiuka maadili kutoendelea na kazi kwani wengi wamekuwa wakiuka na wakati mwingine anakwenda kuajiriwa sehemu nyingine au shule ya jirani sasa bodi itafanya kazi hiyo ni suala la muda tu na sheria katika hatua mbalimbali”amesema Semakafu.
Amesema wadau wa elimu kila mtu kutumia nafasi yake katika kupeana taarifa na sio taarifa zinaonekana mitandaoni kwa vitu ambavyo vinaweza kuzungumzika na serikal ikachukua hatua na kumaliza changamoto ambazo ziko katrika sekta ya elimu.
Aidha amesema kongamano hilo linafungua kwenda kuongeza ufanisi wa elimu katika maeneo yao ya kazi huku serikali ikichukua mapendekezo ya michango ya utoaji wa elimu kwa wanafunzi.
Amesema ADEM ifanye jukumu lao la msingi kwani wanatoka na kufanya majukumu mengine hivyo ni bora warudi kama ilivyokuwa dhamira ya uanzishaji wa hiyo ADEM.
Mwenyeki wa mkutano huo Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi Rais -Tawala Mitaa na Tawala za Mikoa Tamisemi) George Jidamva amesema kuwa wakiwa wasimamizielimu watafanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na wajumbe wa mkutano huo.
Amesema katika mkutano huo wamejifunza vitu mbalimbali kwani pasipo kuwepo na mikutono hiyo kuna baadhi ya vitu vinaweza visiende sawa.
Nae Mwenyekiti wa Wamiliki wa Vyuo Binafsi Mahmood Mringo amesema sekta ya elimu inazungumzwa na watu wasio wadau hivyo kila mtu atumie nafasi ya kuzungumza suala la elimu na sio watu wengine.
Amesema kuwa ukurasa mpya umfunguliwa katika hivyo na kuongeza nguvu katika kusukuma gurudumu la elimu.
Post A Comment: