NA HERI SHABAN

JUKWAA la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Kata yaKipawa lina idadi ya Wanawake 2000  walojiunga na jukwaa hilo

Akizungumza katika uzinduzi wa jukwaa la Uwezeshaji wananchi kiuchumi  Kata ya Kipawa Manispaa ya Ilala Mwenyekiti wa Jukwaa hilo Zipporah  Simwanza   baadhi yao wameunda vikundi.

Simwanza alisema katika Wanawake 2000 ambao wamejiunga Jukwaa baadhi yao walifanikiwa  kuunda vikundi 90 vilivyopo hai vyenye jumla ya Wanawake 1697 ambapo wameungana na kuunda vikundi vya watu watano mpaka hadi 30.

"Kata ya Kipawa ina Jukwaa la Wanawake 2000 Vikundi vikivyosajiliwa 90 wanawake ,1697,vikivyopata mkopo  31.vilivyojaza fomu 19  ambavyo havijaomba mkopo vikundi 40 wasiona vikundi Wanawake 300" alisema Simwanza .


Aidha alisema upatikanaji wa mikopo katika kata hiyo wanawake wengi wanakusudia kukuza mitaji yao wanakata tamaa .

Pia alisema wanakabiliwa na ukosefu wa elimu wameomba halmashauri ya Ilala iwaweze  kuwapatia shilingi milioni 40   kugharamia mafunzo  ya wajasiriamali zaidi ya 200 kwa kutumia watalaam wa SIDO,TFDA na TBS   ili kuwajengea uwezo.

Alisema katika fedha hiyo walioomba itakayobaki watanunua mashine  za kukoboa na kusaga pamoja na mashine za kutengeneza mifuko mbadala.


Akielezea changamoto nyingine katika kata ya Kipawa  alisema kata hiyo ina mitaa sita,Kipunguni,Stakishari,Mogo,Mji mpya,Kalakata na Uwanja Ndege aina eneo la soko tunaiomba halmashauri iweze kutupatia eneo  la soko pindi tunapozalisha bidhaa zetu tujue tunapeleka wapi kata yote aina soko.

Kwa upande wake mgeni rasmi, Katibu wa Jukwaa Mkoa Dar es Saalam Husna
Shechonge aliwapongeza Wanawake wa Kipawa kwa uzinduzi wa Jukwaa hilo watumie nafasi hiyo kuzitangaza fursa za biashara zao na kutafuta masoko.

Husna aliwataka viongozi waliosimikwa katika jukwaa hilo kuwa chachu ya maendeleo katika kushirikiana na wanawake wa kipawa kuakikisha  wanaunga mkono  juhudi za serikali kwa lengo la kumkomboa mwanamke kiuchumi .

Husna pia alitoa elimu ya Jukwaa kwa Wanawake alisema  Majukwaa ya Wanawake hayana fedha dhumuni lake kutambua nafasi zao walizonazo .

Husna alisema majukwaa ya wanawake yote
 ameadhishwa sio kwa ajili ya dhumuni la mikopo majukwaa ya uwezeshaji Wanawake Kiuchumi hayana mikopo

Naye Makamu  Mwenyekiti wa Jukwaa Wilaya ya Ilala Sauda Addey amewataka Wanawake kushirikiana kwa pamoja  katika shughuli zao za kiuchumi waache maisha tegemezi.

Sauda alisema  imefikia Wanawake kujishughulisha wainuke kiuchumi  kuunga mkono juhudi za Rais wa awamu ya tano  wasiweke chuki katika vikundi waheshimu viongozi waliochaguliwa  kwa ajili ya kuwaongoza.
Mwisho
Share To:

msumbanews

Post A Comment: