Tangu wiki iliyopita zimesambaa taarifa za Hamisa Mobetto kuchezea kipigo cha ‘Mbwa Koko’ kutoka kwa mama yake Diamond – Hata hivyo ukweli wa taarifa hizo haukuwezekana kufahamika mpaka sasa.
Lakini Diamond ameonekana kuibua upya suala hilo huku akionekana kutoa jibu la tukio hilo lakini kwa kutumia njia ya mafumbo.
Msanii huyo wa WCB, amecomment kwenye video ya mama yake ambayo ameiweka kwenye mtandao wa Instagram kwa kumfananisha mama huyo na bondia aliyekuwa hatari zaidi ulingoni, Mike Tyson.
“Tysoooooooon!!!!😅,” amecomment Diamond kwenye video hiyo.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: