Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametoa wito kwa wafanyabiashara wote nchini ambao wanahitaji mahindi kufika haraka katika mkoa wa Rukwa kununua zao hilo kwani kumekuwa na ziada ambayo wananchi wanahitaji kuuza lakini soko hakuna.

Amesema kuwa katika wilaya ya Nkasi pekee kuna zaidi ya tani 23,000 za chakula ambacho ni ziada ya wilaya na imekosa wanunuzi na kumuagiza katibu tawala wa Mkoa kuhakikisha anafanya mawasiliano na mikoa mingine ambayo ina upungufu wa chakula ili kuja kununua ziada hiyo ambayo wananchi wamekuwa wakilalamika kukosa soko. 

Pia, amemuagiza katibu tawala wa Mkoa kuhakikisha kuwa kunakuwa na mratibu wa mahindi katika kila wilaya ili kuwasaidia wafanyabiashara wa mahindi kutoka nje ya mkoa kupata urahisi wa kununua mahindi na kuwaepusha na utapeli. 

 “Tani zaidi ya 23,000 ipo kwenye wilaya moja tu, hii ni fursa kwa wafanyabiashara waliopo kwenye mikoa ambayo ina upungufu wa chakula kuja kununua mahindi na kuyapeleka huko wankoyahitaji, hivyo nakuagiza katibu tawala kuhakikisha kuwa unafanya mawasiliano na mikoa na ambayo ina upungufu pamoja na wafanyabishara wenye kuhitaji ili tuweze kuwasaidia wananchi wetu lakini kuwe na mratibu wa kuweza kusimamia hili ili wafanyabiashara hao wasipate tabu,”

Ameyasema hayo baada ya kusomewa taarifa ya wilaya ya Nkasi iliyobainisha uwepo wa ziada ya tani 23,000 za mahindi kwaajili ya kuuza ambapo wakulima wa wilaya hiyo na kwengineko Mkoani humo wamekuwa wakilalamikia soko la zao hilo. 

Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala wa wilaya ya Nkasi Mwanaisha Luhaga alipokuwa akisoma taarifa hiyo alisema kuwa changamoto kubwa inayowakabili hivi sasa ni upatikanaji wa mbolea kwa wananchi ambapo mpaka sasa wilaya imepokea tani 20 tu kati ya 850. 

Share To:

msumbanews

Post A Comment: