IGP ERNEST MAGU KUKABIDHIWA SARPCCO.

 

Inspekta Jenerali wa Polisi IGP Ernest Mangu  anatarajia kukabidhiwa uenyekiti wa shirikisho la wakuu wa majeshi ya polisi  kusini mwa Afrika (SARPCCO) katika mkutano unaotarajiwa kufanyika  sept. 16 jijini Arusha.

Akizungumza  jana na waandishi wa habari jijini  hapo msemaji wa jeshi la polisi  kamishna Msaidizi wa polisi Advera Bulimba alisema Mangu atakabidhiwa uwenyekiti huo kutoka kwa Mkuu wa jeshi  la polisi wa nchi ya Msumbiji ambapo atadumu katika nafasi hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Bulimba alisema mkutano huo utatanguliwa  na mkutano wa kamati tendaji za SARPCCO ambazo zitakutana sept. 14  na sept. 15  ili kuandaa ajenda na mapendekezo ambayo yatawasilishwa katika mkutano  wa  wakuu wa polisi ambao unatarajiwa kufunguliwa  na Makamu wa Rais Samia  Suluhu Hassan.

" Mambo mbalimbali yakiwemo ya kukabiliana na uhalifu  wa kuvuka mipaka yatajadiliwa  pamoja na kuweka mikakati na maazimio ya kufanya Operesheni za pamoja zinazojumuisha nchi zinazounda shirikisho hilo" alisema.

Aliongeza kuwa pamoja na majadiliano mbalimbali pia  mkutano huo utajadili kwa kina utekelezaji wa maazimio mbalimbali kupitia kamati tendaji za wakurugenzi wa upelelezi kamati tendaji ya sheria, kamati tendaji ya Mafunzo.

Pia  kamati tendaji ya mtandao wa polisi wanawake itajadili suala la michezo baina  ya majeshi ya polisi kwa nchi wanachama.

Hata hivyo alisema SARPCCO iliundwa  mwaka 1995 kwalengo la kuimarisha ushirikiano wamajeshi ya polisi kwa nchi za  kusini mwa Afrika katika kukabiliana na uhalifu.

"Mpaka hivi sasa umoja huo unaundwa na  nchi   15  ambazo ni Tanzania, Angola, Botswana, Malawi, Lesoto, Mauritius na Demokrasia ya Kongo (DRC)

Nyingine ni Namibia, Afrika Kusini, Zambia, Zimbabwe, Swaziland, Madagascar na Shelisheli

 

Share To:

msumbanews

Post A Comment: