WAFANYABIASHARA DODOMA KUIJENGA DODOMA .

 

MKUU wa wilaya ya Dodoma mjini Christina Mndeme amewataka wafanyabiashara waliomo mkoani humo  kuijenga makao makuu ya nchi  kwa kuwekeza katika maeneo mbalimbali ya biashara kama nyumba za makazi vikiwemo viwanda na mashamba badala ya kusubiri watu kutoka nje kuja kuwasaidia kuwekeza

Mkuu wa wilaya aliitoa kauli hiyo wakati  alipokuwa akiongea na wafanyabiashara wa viwandani na mashambani walio na wasiokuwa  ndani ya [TCCIA] waliokuwa wamekutana kwa lengo la kuzijadili fulsa na changamoto zitakazokuwepo kutokana na serikali kuhamia mkoani Dodoma linalotokana na tamko la hayati Julias Kambarage Nyerere alilolitoa mwaka 1972 kuwa makao makuu ya nchi yahamishiwe mkoani humo

Mndeme alizitaja Fulsa zinazotokana na ujio wa makao makuu mkoani humo kuwa ni ujenzi wa nyumba za makazi, jengo la kisasa la biashara ambalo litakuwa na gorofa 5 litakalojengwa eneo lilipo soko la sabasaba na kituo cha biashara kinachotarajiwa kujengwa Ihumwa ambako patajengwa bandari kavu na tayari hekari 500 zimetengwa

Pia kijijini hapo pametengwa hakari 217,000 kwa ajili ya ujenzi wa  reli ya kisasa yenye standard Gage pia stendi kuu ya mabasi ya kwenda mikoani ambayo itajengwa katika eneo linalotazamana na viwanja vya maonyesho ya nane nane wanasubiliwa  wawekezaji ambao watajenga vibanda vya biashara, migahawa na maduka makubwa, huku viwanja hivyo vya nanenane vikitakiwa kuboreshwa ili shughuli za kibiashara ziweze kufanyika mwaka mzima tofauti na sasa ambapo baada ya maonyesho ni magereza na JKT pekee hubakia wakifanya shuhuli zao

Alisema katika eneo la uwekezaji la Njedengwa patajengwa Kiwanda cha kusindika zabibu kwa ajili ya kutengeneza Mvinyo, Juice ikiwa ni pamoja na kuzikausha kunakoambatana na eneo la kilimo cha zao hilo kutengwa katika kijiji cha Gawaye kwa jumla ya heka 600, pia ujenzi wa kiwanda cha kusindika mazao ya mifugo yakiwemo maziwa fresh, mtindi na hata soseji ambazo zitakuwa zikitokea Dodoma na kusambaa nchi nzima na hata nje ya nchi

“sasa hivi tuna wakazi 410,000 na baada ya makao makuu kukamilika idadi ya watu itaongezeka hivyo tumieni fulsa hii kuwekeza ninyi wafanyabiashara wa hapa kwa kile mnachokiweza ili isijefikia wakati ambapo wanaweza kuwekeza watu kutoka nje halafu mkabaki kulalamika kwa nini nisingekuwa mimi na hapo utakuwa umechelewa”, alisema

Awali kwa upande wake Mwenyekiti wa Chemba ya wafanyabiashara wa viwandani na mashambani [TCCIA] Deus Nyabiri alisema kinachotakiwa ni woa kuwekewa mazingira mazuru kama wafanyabiashara huku kila kitu kikiwa kimewekwa wazi yakiwemo maeneo ya uwekezaj
Share To:

msumbanews

Post A Comment: