Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akimsikiliza Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein (kulia) wakati akizungumza nae alipomtembelea kumjulia hali nyumbani kwake Kibele, Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini, Zanzibar tarehe 08 Januari, 2026

Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal (kulia) akisisitiza jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) wakati Waziri huyo alipomtembelea nyumbani kwake Mbweni, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini, Zanzibar tarehe 08 Januari, 2026.

Mama Sitti Mwinyi, mke wa Hayati Ali Hassan Mwinyi (kushoto) akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) alipomtembelea nyumbani kwake Nyamanzi, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini, Zanzibar kumjulia hali ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake.

Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein (wa kwanza kulia) akisisitiza jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa pili kutoka kulia) wakati Waziri huyo alipomtembelea nyumbani kwake Nyamanzi, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini, Zanzibar kumjulia hali ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal (kushoto) baada ya kuzungumza nae nyumbani kwake Mbweni, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini, Zanzibar tarehe 08 Januari, 2026.

Mkurugenzi Msaidizi Utawala na Dawati la Viongozi wa Kitaifa Wastaafu, Bi. Nyasinde Mukono (wa kwanza kushoto) akizungumza jambo wakati Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipomtembelea Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal (hayupo pichani). Wengine ni wake wa Dkt. Bilal

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein (katikati) baada ya kuzungumza nae nyumbani kwake Nyamanzi, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini, Zanzibar alipomtembelea kumjulia hali ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Utawala na Dawati la Viongozi wa Kitaifa Wastaafu, Bi. Nyasinde Mukono.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal (watatu kutoka kulia). Wengine ni Wakurugenzi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia) akifurahia jambo na Mama Sitti Mwinyi, mke wa Hayati Ali Hassan Mwinyi (kushoto) baada ya kuzungumza nae alipomtembelea nyumbani kwake Nyamanzi, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini, Zanzibar kumjulia hali ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa tatu kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein (watatu kutoka kulia). Wengine ni Wakurugenzi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mama Sitti Mwinyi (wa tatu kutoka kushoto), mke wa Hayati Ali Hassan Mwinyi wakati Waziri huyo alipomtembelea nyumbani kwake Nyamanzi, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini, Zanzibar kumjulia hali ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake. Wengine ni Wakurugenzi na Maafisa kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI.


Na. Veronica Mwafisi-Zanzibar


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amefikisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Viongozi Wakuu wa Kitaifa Wastaafu ambaye ameahidi kuendelea kuwatunza Viongozi na Wenza wao kwa kuzingatia Katiba, Sheria na Kanuni zilizopo.

Salamu hizo zimefikishwa Januari 8, 2026 kwa nyakati tofauti alipomtembelea Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein nyumbani kwake Kibele Mkoa wa Kusini Unguja, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal nyumbani kwake Mbweni, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini na Mwenza wa Hayati Ali Hassan Mwinyi-Mama Sitti Mwinyi nyumbani kwake Nyamanzi, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini.

Mhe. Kikwete amesema, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ina jukumu la kutunza Viongozi Wakuu Wastaafu Kitaifa na Wenza wao, hivyo yuko tayari kuendelea kutekeleza jukumu hilo alilopewa na Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ufanisi.

Kwa upande wake, Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein amemshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia kwa salaamu na kumpongeza Mhe. Kikwete kwa kupanga ziara ya kuwatembelea Viongozi Wakuu wa Kitaifa Wastaafu. Ziara hiyo inawapa faraja, heshima na inaonesha thamani ya mchango wao kwa taifa.

Aidha, Dkt. Shein ametumia fursa hiyo kutoa rai kwa watumishi wa umma kufanya kazi kwa kupendana, ushirikiano na kuzingatia mipaka ya kazi zao kwa kuwa watumishi hao wanamsaidia Rais ambaye anawajibika kwa wananchi.

Naye, Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal ameishukuru Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora kwa kuwajali na kuwahudumia vyema kwa mujibu wa taratibu


Kwa upande wake, Mama Sitti Mwinyi amemshukuru Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wenza wa Viongozi Wastaafu na ameomba moyo huo uendelee.
8 Januari, 2026

Hayo yamesemwa leo tarehe 08 Januari, 2026 na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu – ADEM Dkt. Maulid J. Maulid alipokuwa akifunga rasmi mafunzo ya Utawala Bora wa Elimu kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa yanayoendeshwa na ADEM kwa Maafisa Elimu Kata 101 wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Picha ya Pamoja ya baadhi ya viongozi watendaji wa Kata na Tarafa, waliohudhuria semina iliyotolewa na Mamlaka  ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, leo Januari 8,2026

.....

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, leo Januari 8,2026 ilitoa elimu kwa watendaji wa Serikali za Mitaa mkoani Njombe kuhusu utaratibu wa kushughulikia malalamiko na migogoro, mchakato wa kupata leseni za kuanzisha vituo vya mafuta vijijini pamoja na matumizi sahihi na salama ya gesi ya kupikia majumbani.

Akizungumza kwa niaba ya Meneja wa Kanda hiyo, Mhandisi Mwandamizi wa Maji na Usafi wa Mazingira kutoka EWURA, Bw. Dikson Semkuyu, alisema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo viongozi hao ili waweze kuwafikishia wananchi elimu sahihi kuhusu huduma zinazodhibitiwa na EWURA.

“Tunatarajia elimu tuliyotoa itawafikia wananchi mnaowaongoza, ikiwemo mwongozo wa kutambua na kuchangamkia fursa mbalimbali za uwekezaji zinazotolewa na EWURA,” alisema Mhandisi Semkuyu.

Kwa upande wake, Katibu Kata wa Idamba, Bw. Ibrahim Ilomo, aliishukuru EWURA kwa kutoa mafunzo hayo, akisema yamewasaidia kufahamu matumizi salama ya gesi ya kupikia na kugundua kuwa zipo fursa za uwekezaji katika vituo vya mafuta vya gharama nafuu vijijini.

Mwakilishi wa Meneja wa EWURA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini ambaye ni Mhandisi Mwandamizi wa Maji na Usafi wa Mazingira, Dickson Semkuyu, akiwasilisha mada juu ya kazi na wajibu wa EWURA.

Ofisa za Huduma kwa Wateja Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Bw. Francis Mhina, akiwasilisha mada ya namna EWURA inavyosikiliza na kutatua migogoro na malalamiko ya wateja kwa watoa huduma zinazodhibitiwa wakati wa semina hiyo leo.

Mhandisi Mwandamizi Mkaguzi wa Mafuta ya Petroli EWURA Nyanda za Juu Kusini, Raphael Nyamamu, akiwasilisha mada wakati wa semina hiyo, leo.

Picha ya Pamoja ya baadhi ya viongozi watendaji wa Kata na Tarafa, waliohudhuria semina iliyotolewa na Mamlaka  ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, leo Januari 8,2026

 

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.

Na.Mwandishi Wetu-MOSHI

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, ameielekeza VETA Moshi kuimarisha ushirikiano na makampuni na viwanda ili kuongeza fursa za ajira kwa wahitimu na kukuza matumizi ya teknolojia mpya, sambamba na uelekeo wa taifa uliobainishwa katika Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, sera za kisekta na miongozo mbalimbali ya kitaifa.

Mhe. Ameir ametoa maelekezo hayo Januari 07, 2026, alipotembelea chuo hicho, amesisitiza kuwa ushirikiano huo unaboresha mafunzo na kulingana na mahitaji ya soko la ajira.

Aidha, amesema kuwa utekelezaji wa mafunzo ya sekta ya madini kupitia programu jumuishi ya ufundi wa teknolojia ya uchimbaji madini kwa kushirikiana na Chemba ya Madini Tanzania utawezesha utoaji wa mafunzo yanayoakisi mahitaji halisi ya sekta hiyo muhimu kwa taifa.

 "Serikali itaendelea kuwekeza katika kuongeza fursa na kuinua ubora wa mafunzo ya ufundi stadi kwa kununua vifaa vya kisasa, kuimarisha miundombinu ya kufundishia na kujifunzia, pamoja na ujenzi wa vyuo vipya vya VETA 64 nchini."amesema Mhe. Ameir 

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Antony Kasore, amesema kuwa  Chuo cha VETA Moshi kimeendelea kuwa mfano wa mafanikio ya elimu ya ufundi stadi kwa kuimarisha ushirikiano na viwanda na migodi, hatua inayowezesha mafunzo yanayotolewa kuendana na mahitaji ya soko.

CPA Kasore amesema  ushirikiano huo umewezesha vijana kupata ajira kwa haraka kutokana na ujuzi wa vitendo wanaopata wakati wa mafunzo, na kwamba baadhi ya wahitimu kutoka VETA Moshi wamefanikiwa kupata ajira nje ya nchi, jambo lililosaidia kuboresha uchumi wa familia zao na kuchangia pato la taifa.

Katika kuunga mkono juhudi za Serikali, zinazotekelezwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na wadau katika kuimarisha Elimu Amali, Mbunge wa Moshi Mjini, Mhe. Ibrahim Shayo, ameahidi kufadhili masomo ya vijana 10 kila mwaka katika Chuo cha VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akipata maelezo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi mara baada ya kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir,akizungumza mara baada ya  kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.

Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA Antony Kasore,akielezea mafanikio yaliyopatikana katika Chuo cha VETA Moshi mara baada ya Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, kutembelea  Chuo cha  VETA Moshi.

 

 



Na Oscar Assenga,TANGA

BILIONI 10 zimelipwa kama sehemu ya fidia kwa wananchi ambao wameweza kupisha maeneo yao kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya Bomba la Mafuta Ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongeleani Tanga,Tanzania.


Hayo yalibainishwa na Naibu Waziri wa Nishati Salome Makamba wakati wa ziara ambayo aliambatana na Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini wa Uganda, Dkt. Ruth Nankabirwa ya kujionea hatua ambayo imefikiwa ya ujenzi wa mradi huo katika eneo la Chongoleani Jijini Tanga.

Ambapo pia katika mradi huo zaidi ya wananchi 9800 waliopo katika mkoa wa Tanga wameweza kushiriki kwenye shughuli za ujenzi wa bomba la mafuta ghafi.

Naibu Waziri huyo alisema mradi huo kwa upande wa Tanzania umeweza kufikia asilimia 86 ya utekelezaji wake ukihusisha maeneo ya ulazaji wa mabomba,ujenzi wa matankiya kuhifadhia mafuta ghafi sambamba na eneo la gati ya kushushia mafuta hayo.


Aidha alisema kuwa mpaka sasa mradi huo upo katika hatua nzuri ya utekelezaji wake na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Julai mwaka huu.

Makamba alisema kuwa mradi huo utaongeza usambazaji wa mafuta nchini na kupunguza gharama za usafirishaji, na kuufanya uwe na tija kwa wananchi wa mkoa wa Tanga na Tanzania kwa ujumla.



Mradi huu umewanufaisha kwa kiasi kikubwa wananchi wa Tanzania tofauti na wenzetu wa uganda kutokana na eneo kubwa kuwa upande wa nchi yetu"alisema Naibu Waziri Makamba.


Hata hivyo Makamba alisema kwamba dhamira ya dhati ya Rais Dkt Samia Suluhu na Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni imewezesha utekelezaji mzuri wa mradi huo unaotarajiwa kuleta mabadiliko makubwa katika Nyanja za kiuchumi ,kijami,ajira na uboreshaji wa huduma za jamii


Kwa upande wake Waziri wa Uganda Nankabirwa alisema kuwa mradi huo umeweza tekelezwa katika viwango bora vya usalama huku ukizingatia ulinzi wa athari za kimazingira


"Tayari wananchi wetu wameweza wameweza kunufaika na sehemu ya kurudisha kwa jamii kwa kuwekewa miundombinu ya maji safi,ujenzi w barabara sambamba na shughuli za michezo kwa wananchi wanaoishi karibu na maeneo ya mradi huo"alisema Waziri huyo.

Aidha aliwataka wananchi wa nchi hizo mbili kuutunza na kuulinda mradi huo kwani utakapoanza kazi utaweza kuketa manufaa makubwa ya kiuchumi baina ya nchi hizi mbili.


Ziara hiyo ililenga kuona hatua za utekelezaji wa mradi huo na kuhakikisha kuwa unatekelezwa kwa viwango vya juu vya ubora na usalama.



 


Watoto waliokinzana na sheria na kupelekwa katika Shule ya Maadilisho ya Irambo iliyopo Wilaya ya Mbeya Vijijini mkoani Mbeya wamehimizwa kujutia makosa yao, kubadili mienendo na kuishi kwa utii na maadili mema mara baada ya kumaliza adhabu na kurejea katika jamii walizotoka.

Ushauri huo umetolewa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum , Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi wakati wa ziara yake ya kutembelea na kukagua shule hiyo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali katika kuhakikisha watoto waliokinzana na sheria wanarekebishwa kimaadili na kisaikolojia.

“Hii ni fursa ya pili mliyopewa na Serikali itumieni kujitathmini, kujutia makosa na kuamua kubadilika ili mtakaporejea katika jamii muwe mfano wa kuigwa maana mnajua kabisa kutowasikiliza wazazi na jamii kumewasababisha wengi wenu kujiingiza katika vitendo vinavyopingana na sheria na hatimaye kujikuta mmefikishwa katika shule hii na naamini ndani ya miaka hiyo uliyopangiwa na Serikali naamini itawasaidia kubadilika” amesema Mhe. Mahundi.

Aidha, aliwasisitiza watoto hao kuwa utii, nidhamu na maadili mema ni nguzo muhimu zitakazowawezesha kujenga maisha bora na kuepuka kurudia makosa ya awali, huku akiahidi kuwa Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya malezi katika shule za maadilisho nchini.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini, Mhe. Patali Shida Patali, ameishukuru Serikali kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika eneo hilo, pia kukifanya kituo hicho kuwa katika jimbo lao ambapo kinasaidia watoto wa vijiji vyao na Tanzania nzima.

“Mheshimiwa Naibu Waziri kuwepo kwa kituo hiki sisi Mbeya Vijijini tunanufaika kwani tuna mahusianao mazuri na kituo hiki kwa kuwa kinatunufaisha katika masuala mbalimbali ikiwemo maji tunapata kwao, elimu za mashamba darasa tunazipata hapa pamoja na huduma za afya wanakijiji hutumia zahanati ya shule hii” amesema Mhe. Patali.

Awali akisoma taarifa ya shule hiyo, Meneja wa Shule ya Maadilisho Irambo John Meshack amesema kuwa, shule hiyo kwa sasa inahudumia watoto 28 wa kiume waliotoka maeneo mbalimbali ya Tanzania Bara na watoto hao wanapatiwa huduma muhimu ikiwemo elimu ya msingi, afya, stadi za maisha, malezi na michezo kwa lengo la kuwabadilisha tabia na kuwaandaa kurejea katika jamii wakiwa raia wema. 

Ziara ya Naibu Waziri Mahundi inalenga kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali, viongozi wa kisiasa na taasisi za malezi katika kuhakikisha watoto waliokinzana na sheria wanapata marekebisho stahiki na kurejeshwa salama katika jamii.