Katibu Mkuu wa CCM mstaafu, Mzee Yusuf Makamba amewaomba wananchi wa Jimbo la  Bumbuli mkoani Tanga kumchagua mgombea urais wa chama hicho, Rais Samia Suluhu Hassan, mgombea ubunge wa jimbo hilo, Mhandisi Ramadhani Singano na madiwani wote wa chama hicho.

Makamba amesema hayo leo Septemba 15, 2025 kwa njia ya simu kwenye mkutano wa kampeni za mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama hicho, Dk Emmanuel Nchimbi uliofanyika Lushoto eneo la Soni.

Mzee makamba amesema anaimani na wagombea wote wa CCM na alipenda kuhudhuria mkutano huo ila tatizo ni changamoto ya afya yake.

Dk Nchimbi alimpigia simu Mzee Makamba akiwa jukwaani ndipo alipozungumza na kuwaombea kura wagombe wote huku akiwaomba wananchi wa mkoa wa Tanga wasimuangushe katika uchaguzi utakaofanyika Oktoba 29, 2025.





 

 

Mratibu wa Mradi, kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Kenneth Hosea, akizungumza wakati wa kumkaribisha Mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa kikao cha Mradi wa HEET

.....

UTEKELEZAJI wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) umefikia asilimia 74.3 tangu uanze kutekelezwa mwaka 2022, hatua iliyotajwa kuwa mafanikio makubwa.

Hayo yameelezwa leo Septemba 15,2025 , katika ukumbi wa Maktaba wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Mratibu wa Mradi  kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Kenneth Hosea, wakati akimkaribisha Mgeni rasmi kufungua kikao cha siku tano cha tathmini ya Mradi, kikihusisha wadau wote muhimu wanaotekeleza Mradi huo.

Dkt. Hosea amesema, juhudi hizi kubwa ni matokeo ya kazi nzuri iliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kwamba Wizara inaendelea kutoa hamasa kwa Taasisi za Elimu ambazo zinatekeleza mradi huu kuendelea kuongeza kasi ili kuhakikisha malengo yanafikiwa katika kipindi kilichopangwa.

Akifungua kikao kazi hicho, mgeni rasmi, Prof. Nelson Boniface, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, akimwakilisha Makamu Mkuu wa Chuo amesema inatia moyo kuona mafanikio makubwa ya Mradi kitaifa na kuwataka washiriki katika kupokea mawasilisho kuwa makini kujifunza na kutumia fursa hiyo kujifunza kutoka kwa wale waliofanikiwa ili kwa pamoja kufikia malengo makubwa kama Taifa. 

“Hii ni fursa kwa Taasisi ambazo bado ziko nyuma kwenye utekelezaji, tuitumie kwa kujifunza wenzetu walikopita wakafanikiwa ili tuongeze juhudi za tufikia malengo yaliyokusudiwa” Alisisitiza.

Katika Mkutano huo, Mratibu msaidizi wa Mradi Chuo Kikuu cha Dodoma, Dkt. Happiness Nnko, amewasilisha taarifa ya maendeleo ya Mradi kwa kueleza baadhi ya Miradi imekamilika kwa asiliamia 100, wakati miradi ya ujenzi ikiendelea kutekelezwa ukiwemo ujenzi wa Maabara ya Sayansi katika Ndaki ya Sayansi Asilia na Hisabati, ambapo ujenzi wake umefika asiliamia 55.3, Ujenzi wa vyumba vya Madarasa Ndaki ya Sayansi za Ardhi ya Uhandisi umefikia asilimia 61, wakati ujenzi wa Kampasi Mpya, Njombe ulioanza mwezi Juni 2025, umefikia asilimia 10.3.

Amesema,kuwa  Menejimenti ya Chuo inaendelea kufuatilia kwa karibu ujenzi unaoendelea ikiwemo vikao vya mara kwa mara na wakandarasi, ili kuhakikisha ujenzi unakamilika kabla Mradi kwisha, Juni 2026. Kwa upande wa mitaala mipya ya elimu, Dkt. Nnko amesema Chuo kimefanikiwa kubuni na kufanya mapitio ya programu 39, na mchakato wa kuzianzisha uko kwenye hatua mbalimbali za mapitio na kupata ithibati.  

“Mbali na mapitio ya programu, pia Chuo kimepeleka Wakufunzi 18 masomoni kwa ngazi mbalimbali za elimu (Masters na PhD), kati yao wanaume wakiwa 13 na wanawake watano(5). Baadhi wanasoma hapa Tanzania na wengine wako nje ya nchi, Ghana, Uganda, Africa Kusini, Uingereza, Japan na Zambia.

Aidha, Chuo kinaendelea na ununuzi wa vifaa na samani vya majengo, ambapo hadi kufika Septemba 15, 2025 tayari manunuzi 23 yameanzishwa, kati ya hayo 11 wazabuni wameshapatikana, huku taratibu za manununi kwa maeneo mengine zikiendelea. 

Mkutano huu umekutanisha Waratibu wa Mradi kutoka kwenye Taasisi zote za Elimu ya Juu nchini zinazotekeleza Mradi wa HEET, waratibu Wasaidizi, Wataalamu wa Maeneo mbalimbali ya Mradi ikiwemo Ufuatiliaji na Udhibiti, Mazingira, Tehama, Mahusiano na Viwanda na Mawasiliano.

,Naibu Makamu Mkuu wa Chuo, Taaluma, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Prof. Nelson Boniface,akifungua Kikao Kazi cha Waratibu na Wasimamizi wa Mradi wa HEET kilichoanza leo Dar es Salaam.

Mratibu wa Mradi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Kenneth Hosea, akizungumza wakati wa kumkaribisha Mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa kikao cha Mradi wa HEET

Mratibu Msadizi wa Mradi wa HEET toka Chuo Kikuu cha Dodoma, Dkt. Happiness Nnko, akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya Mradi kwa UDOM wakati wa Kikao cha Wadau.

Mratibu wa Mradi wa HEET toka Chuo Kikuu cha Dodoma akisikiliza kwa makini wasilisho wakati wa kikao cha wadau kinachoendekea katika ukumbi wa Maktaba, UDSM

Baadhi ya washiriki wa kikao kazi wakifuatilia kwa makini kikao kuhusu maendeleo ya Mradi wa HEET

 


Na Mwandishi Wetu, Muheza


MGOMBEA ubunge Jimbo la Muheza kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Hamisi Mwinjuma maarufu MwanaFA amesema ataendelea kushirikiana na wananchi wa wilaya ya Muheza kuhakikisha changamoto za Jimbo hilo linafanyiwa kazi.


Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika kata ya Mkuzi, MwanaFA alisema kuwa changamoto zote zilizopo wilayani hapa anakwenda kuzifanyia kazi kwakuwa ni kipaumbele chake.

"Napenda niwahakikishie kuwa changamoto zote za wilaya ya Muheza nakwenda kuzifanyia kazi, hakuna jiwe ambalo litaachwa kugeuzwa...Changamoto zilizopo nakwenda kuzifanyia kazi na zitakuwa kipaumbele changu," alisema mgombea huyo.


MwanaFA ambaye ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo aliwataka wananchi waende wakapige kura Oktoba 29 na wakawachague wagombea wa CCM kwakuwa katika kipindi cha miaka mitano wamefanya kazi kubwa ya kutekeleza miradi ya maendeleo.


Alisema Muheza wamejipanga safari hii kuvunja rekodi ya watu waliojiandikisha kupiga kura watoke kwa idadi kubwa kwakuwa Jimbo hilo wameandikishwa watu 168,000.

"Ni uovu mkubwa kama umejiandikisha halafu hukwenda kupiga kura Oktoba 29, nawaomba amkeni asubuhi unamwamsha na jirani yako wale wapiga kura halali mnaenda kuchagua wagombea wa CCM," alisema MwanaFA.


Alisema unapokwenda kupiga kura unakuwa na wajibu wa kuwauliza viongozi wao yale walitoaahidi na Kisha wakashindwa kutatekeleza kwa kuwa umekuwa na uhalali huo kwavile umepiga kura ya kuwachagua.

Akielezea kazi zilizofanyika katika kata ya Mkuzi ambayo imepokea jumla ya shilingi milioni 850 na kwa upande wa elimu ya msingi jumla ya sh. 248,436,056 ambazo zikipelekwa katika shule za msingi Mkuzi, Mafere na Mindu.

Alisema shule ya sekondari Mkuzi ilipata kiasi cha shilingi milioni 146.9 ambazo zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa madarasa, ujenzi wa maabara na matundu ya vyoo.

Hata hivyo, alisema shule nyingi za sekondari wilayani Muheza hazina mabweni ya wanafunzi wanaokaaa mbali waweze kulala akasema kwamba katika ilani ya uchaguzi jumla ya mabweni 15 yatajengwa.


Kwa upande wa afya alisema kuwa kata ya Mkuzi ilipata jumla ya shilingi milioni 280 ambazo zimepelekwa katika kituo cha afya Mkuzi kwa ajili ya kununulia vifaa tiba na majokofu ya kuhifadhia miili ya marehemu.


MwanaFA alisema katika wilaya ya Muheza wakati akiingia kuwa mbunge kulikuwa na kituo cha afya kimoja cha Mkuzi ambapo katika kipindi chake ameweza kufanikisha kupata vituo vya afya vingine ambazo ni za Ubwari ambayo hati katika eneo ilipojengwa haikuwepo na baada ya kupatikana kikapitishwa kuwa kituo cha afya na kuanza kupata mgao.


Kituo kingine cha afya kilichojengwa ni cha tarafa ya Bwembera kilichojengwa Kata ya Kwafungo, kingine ambacho tayari kimeingiziwa pesa kiasi cha shilingi milioni 645 ni kituo cha afya tarafa ya Amani. Kingine ni cha tarafa ya Ngomeni ambacho kinajengwa kata ya Misozwe kimeingiziwa shilingi milioni 250.

MwanaFA aliwaambia Wana Mkuzi kwanini anaomba kura na wanatakiwa kuichagua CCM ni kwasababu Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ameweza kutatua changamoto mbalimbali katika Jimbo hilo hivyo anatakiwa kupata kura za kishindo.


"Mimi nina kimbelembele cha kusemea mahitaji ya Wana Muheza lakini anayetoa fedha ni Dkt Samia Suluhu Hassan  hivyo mnatakiwa msipote kura hata moja katika wilaya yetu," alisema. 


Akizungumza kuhusu maji katika kata hiyo alisema jumla ya shilingi milioni 175 ambazo zimetumika katika miradi mbalimbali katika vijiji vya Mafere, Mkuzi na Mindu.


"Kama tatizo la maji halitakaa liishe Muheza kwa shilingi bilioni 40 tulizopata katika mradi wa miji 28 ambao hapa Mkuzi mtapata, basi halitakaa liishe," alisema Mbunge.


Mgeni rasmi katika mkutano huo Mjumbe wa halmashauri Kuu ya mkoa wa Tanga Faraha Mvumo alimkabidhi ilani mgombea udiwani wa kata hiyo Sharifa Kivugo na Mbunge huyo.


Aliwanadi wagombea hao akiwemo Mgombea Urais Dkt Samia Suluhu Hassan ambapo alisema CCM Ina dhamira ya dhati ya kuwaletea maendeleo Watanzania.

Mwisho

15 Septemba 2025, ARUSHA

Waajiri nchini wametakiwa kuweka utaratibu wa kuwajengea uwezo watumishi wao kwa kuwapatia mafunzo mara kwa mara yatakayowawezesha kuwa na uelewa wa pamoja ili kuepusha migogoro sehemu za kazi.
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MAONESHO ya pili ya Masaki Health Expo yanatarajiwa kufanyika Septemba 21, 2025 katika mtaa wa Twiga 06 Masaki Jijini Dar es Salaam ambalo litakuwa huru kwa wananchi wote na linalenga kutoa maarifa na nyenzo za kuboresha afya ya jamii.

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Monduli mkoani Arusha, Joseph Isack maarufu kwa jina la Kadogoo, ameweka wazi siri ya mafanikio yake ya kisiasa kwa kumshukuru Hayati Edward Lowassa, akisema ndiye aliyemtabiria kuwa siku moja atakuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni yake uliofanyika katika eneo la Esilaley, Mji wa Kigongoni, wilayani Monduli, Kadogoo alisema anatamka kauli hiyo kutoka sakafuni mwa moyo wake, kwani Lowassa ndiye aliyemlea kisiasa na kumpa dira ya maisha ya uongozi.

“Sisi wana Monduli, hasa wanasiasa, hatuwezi kumzungumzia Lowassa kama mtu wa kawaida. Mimi ni zao lake. Yeye ndiye alinitabiria kuwa ipo siku nitakuwa Mbunge wa Monduli. Nikiwa hapa leo, naomba nimtaje hadharani, kwa sababu matunda haya ninayoyaona yametokana na mikono yake,” alisema Kadogoo huku akishangiliwa na umati.

Aliongeza kuwa Hayati Lowassa atabaki kuwa nguzo ya kisiasa ya Monduli na ataendelea kukumbukwa na viongozi mbalimbali aliowahi kuwajenga, kuanzia madiwani, viongozi wa wilaya, mkoa hadi Taifa.

Kadogoo alisema akipata nafasi ya kuliongoza jimbo hilo, atahakikisha anasimama kidete kuendeleza misingi ya maendeleo ambayo Lowassa aliyaacha na kuwaletea heshima wananchi wa Monduli.


 


Mgombea Ubunge wa Jimbo la Rufiji kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Mohamed Mchengerwa amewaahidi wananchi wa Jimbo la Kibiti kuwa, atashirikiana Mgombea Ubunge Jimbo la Kibiti kupitia CCM Bi. Amina Mkumba kuleta maendeleo katika jimbo la Kibiti iwapo wananchi hao watamchagua mgombea huyo wa CCM.

Mchengerwa ametoa ahadi hiyo kwa wananchi wa Kibiti, alipopewa fursa ya kuzungumza na wananchi kwenye wa Uzinduzi wa Kampeni za Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilayani Kibiti. 

“Ninawathibitishia wananchi wa Kibiti kuwa sitomtupa Amina, ni msomi na na mwenye uwezo hivyo nitashirikiana nae bega kwa bega kuwaletea maendeleo hapa kibiti, nawasihi mchagueni kwa maendeleo ya Kibiti,” Mchengerwa amesisitiza.

Mchengerwa amefafanua kuwa, ameamua kushirikiana na Amina Mkumba kuleta maendeleo kwani hali za wananchi wa Kibiti bado ni duni kama ilivyo kwa wananchi wa Rufiji na ameongeza kuwa, CCM pekee ndio inaweza kuwaletea maendeleo wananchi wa Kibiti hivyo wasisite kumchagua Amina Mkumba na wagombea Udiwani kupitia CCM.

Aidha, Mchengerwa amewataka wananchi wa Kibiti kumchagua Mgombea Urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kura nyingi za kishindo kwa ajili ya maendeleo endelevu, amani na utulivu wa taifa letu.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu UWT Bi. Susan Kunambi ambaye alikuwa Mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo wa Kampeni za CCM Kibiti, amesema uzinduzi huo ni sehemu ya mkakati wa CCM kujinadi kwa wananchi na kuwaomba kura za ushindi wa kishindo katika ngazi ya Urais, Ubunge na Udiwani ili CCM ipate fursa ya kutekeleza Ilani itakayowaletea maendeleo wananchi.

 


Jina langu ni David, kijana mwenye umri wa miaka 32. Kutoka nilipoanza kuhitimu chuo kikuu, nilikuwa na ndoto ya kupata mke wa kuoa na kuunda familia yenye amani na furaha. Nilijua kuwa upendo na ndoa ni msingi wa maisha yangu, lakini miaka mitano iliyopita, jitihada zangu za kupata mwanamke wa kuoa hazikuzidi kuwa na matokeo.

Kila mara nilipokutana na wanawake waliokuwa sahihi kiakili na kihisia, mahusiano yetu hayakudumu. Wengine walikuwa tayari kuanzisha familia, lakini walinipata sina uthabiti wa kifamilia au hazina ya maisha ya baadaye.

Nilijaribu njia nyingi: marafiki walinisaidia kutambulishwa na wanawake, nilienda kwenye mikutano ya kijamii, na hata kutumia mitandao ya mahusiano, lakini kila hatua ilikuwa ikishindikana. Miaka mitano ilipita bila kuwa na mtu wa kuoa.

Hali hiyo ilinifanya nijisikie kukata tamaa. Marafiki walikuwa wanapita mbele yangu kwenye familia zao na maisha yao ya ndoa, huku mimi nikiendelea kuwa peke yangu. Nilijikuta nikijiuliza: Je, kweli nitapata mwanamke wangu wa maisha? Je, ndoto yangu ya kuunda familia itatimia?. Soma zaidi hapa 




Na Denis Chambi, Tanga


 KATIKA kuendelea kukabiliana na migogoro baina ya wakulima na wafugaji ambayo imekuwa ikileta athari mbalimbali katika jamii za wananchi wanaoishi wilaya ya Pangani mkoani Tanga shirika lisilo la kiserikali la Pangani Coastal Paralegal 'PACOPA' limeendelea kutoa elimu kwa jamii  kwa lengo la kuleta amani.


Baada  ya PACOPA kutoa elimu kwa makundi hayo na kutoa maadhimio ya kushirikiana  kutokomeza migogoro pamoja na kufuata Sheria ikiwemo ya mpango wa matumizi bora ya ardhi zimeundwa kamati maalumu katika kata ya Bweni ambazo zitasaidia kusuluhisha  migogoro pindi itskapotokea hatua ambayo inakwenda kupunguza  malalamiko ambayo yamekuwa yakipelekwa katika ngazi za Halmashauri ya wilaya ya Pangani.

Elimu hiyo inayotekelezwa kupitia mradi wa Tujenge amani pamoja uliopo chini ya shirika la PACOPA  kwa kushirikiana na  We World pamoja na shirika la Twaweza imeanza kuleta matokeo chanya baada ya jamii hizo za wakulima na wafugaji kukiri mabadiliko waliyonayo sasa baada ya kupatiwa elimu hiyo.


Mathayo Madeleke  pamoja na Saumu Bakari ambao ni wa kulima kutoka katika kata ya Bweni wameeleza manufaa waliyoyapata kupitia elimu hiyo waliyopatiwa  ambapo wameahidi kwenda  kuwa mabalozi kwa wananchi wengine.


Wamelishukuru shirika la PACOPA kwa kushirikiana na  we World pamoja Taweza kuwa kuwafikishia mradi huo wenye lengo la  kutoa elimu ya matumizi bora ya ardhi pamoja na kujenga amani na mshikama o baina yao.

"Tunawashukuru sana wahisani waliotuletea mradi huu tulikuwa tukiingia kwenye migogoro mbalimbali lakini shida ni elimu tuliyokuwa nayo kuhusu Sheria  zinazonekana zimepitwa na muda sana , tulikuwa tunaomba elimu iendelew kutolewa ili tuweze kujenga amani hii tuliyonayo hii itatusaidia kuelimiahana sisi kwa sisi binafsi naahidi kwenda kuwa balozi kwa wengine kuhusu elimu hii nipiyoipata


Alfred Mwalongo ambaye ni mfugaji kutoka kata ya Bweni ameeleza kuwa migogoro mingi inayotokea baina ya jamii hizo imekuwa ikisababishwa na wafugaji kutokana na kutokufuata Sheria zilizopo wengi wakitafuta malisho ya mifugo yao hata maeneo ambayo hayajaruhusiwa jambo ambalo limekuwa likisababisha kutokuolewana baina yao na wakulima.

"Ukweli semina hii imetuelimiaha sehemu kubwa husasani sisi wafugaji  ambao tulikuwa tunaishi kwa mazoea kutokana na  utamaduni ambao tulikuwa nao  tukiamini kuwa popote pale tunaweza kwenda kulisha mifugo yetu, lakini sasa  tunaoaswa kufuata Sheria  bila ya kuwa wakaidi  kwa sababu kwa kufanya hivyo ni kudumaza maendeleo  wakulima na wafugaji tunategemeana Kila siku"."


Mratibu msaidizi wa mradi wa kujenga amani  kutoka shirika la Pangani Coastal Paralegal 'PACOPA' Mwanakuzi Abdillah amesema kuwa  lengo lao ambalo limejikita zaidi katika kuhamasisha wananchi kushiriki Moja kwa moja kwenye utatuzi wa migogoro pale inapotokea kwa kushirikiana na wadau  pamoja na viongozi wa Serikali kuanzia ngazi za vijiji.

Ameongeza kuwa kutokana na elimu waliyoitoa kupitia mradi huo uelewa kwa jamii katika kutatua migogoro baina ya wafugaji na wakulima umeongezeka hatua ambayo inakwenda kuleta mabadiliko kwao na hatimaye kufikia lengo la mradi huo wa kujenga amani na kutokomeza kabisa migogoro.


"Lengo kubwa la mradi huu ni kuongeza ushiriki wa wananchi katika kutatua changamoto zao wenyewe ili kuepusha  migogoro katika mradi huu wa kujenga amani tunaamgalia zaidi ni jinsi Gani wananchi wao wenyewe wanaweza  tutatua migogoro kwa kushirikiana na wadau pamoja na viongozi wa Serikali  zao za vijiji"


"Baada ya kuleta mradi huu tumeona kuwa jamii zimekuwa na uelewa zaidi katika kutatua migogoro hata zile kesi za mapigano Kati ya wakulima na wafugaji zimepungua katika kata ya Bweni wengi wamekuwa wakikimbilia katika Serikali zao za vijiji kurlezea zile changamoto walizonazo na kupata utatuzi"


Mratibu hiyo amebainisha kuwa kumekuwa na uelewa mdogo kwa jamii za wakulima na wafugaji hasa kwa namna ya kusuluhisha na kutatua migogoro yao ambapo wengi wamekuwa wakijichukulia Sheria mkononi lakini baada ya mradi huo  kumekuwa na mabadiliko chanya hasa.

 


Na Mwandishi Wetu, Mbeya


MKUU wa Wilaya ya Mbeya, Solomon Itunda, amezindua rasmi Ofisi mpya ya Umoja wa Waendesha na Wamiliki wa Bajaji katika kanda ya Old Airport jijini Mbeya. 


Hafla hiyo ilihudhuriwa na mamia ya vijana, wajasiriamali, viongozi wa Serikali za mitaa na wadau wa sekta ya usafirishaji, ikiwa ni ishara ya kuimarisha mshikamano na kuchochea maendeleo ya vijana katika jiji hilo.

Katika hotuba yake, DC Itunda aliwataka vijana kutumia fursa zinazotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan hususani mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kwa makundi ya kinamama, vijana, na watu wenye ulemavu.


Ameeleza kuwa kwa mwaka wa Fedha 2024–2025, Halmashauri ya Jiji la Mbeya imefanikiwa kutoa mikopo ya zaidi ya shilingi bilioni 3.2, hatua inayodhihirisha dhamira ya serikali katika kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Mkuu huyo wa Wilaya alimshukuru na kumpongeza Mhe. Rais kwa kuboresha mazingira ya kibiashara, hasa katika sekta ya usafirishaji.


Itunda amebainisha kuwa maboresho ya miundombinu, sera rafiki za kiuchumi, na uwezeshaji wa kifedha vimewapa nguvu vijana wajasiriamali ya kujiendeleza na kuchangia maendeleo ya Taifa. 


Uzinduzi huo umekuwa sehemu ya jukwaa la kujenga mshikamano, kuhamasisha uwajibikaji, na kuendeleza maadili ya kazi na utu akiwahimiza vijana kuendelea kushirikiana, kuwa na nidhamu ya kazi, na kutumia fursa zilizopo kwa manufaa ya muda mrefu. 



Ameisitiza kuwa maendeleo ya kweli hujengwa kwa juhudi za pamoja, mshikamano wa kijamii, na uongozi wenye maono.


Tukio hilo limeacha alama ya matumaini na mwelekeo mpya kwa sekta ya bajaji jijini Mbeya.

Mwisho

14 Septemba 2025, ARUSHA

Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (TUGHE) kimeandaa mafunzo yatakayowakutanisha Wafanyakazi na Waajiri yanayojulikana kama “Semina ya Waajiri na Viongozi wa Matawi ya TUGHE yatakayofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 15-18 Septemba 2025.

  


Kwa muda mrefu maisha yangu yaligeuka kuwa uwanja wa mateso makali. Nilikuwa nikishuhudia mambo ya ajabu ambayo sikuwahi kufikiria yangeweza kunipata. Usiku nilipokuwa nikilala, nilisikia mizigo mizito ikinikandamiza kifua, nikashindwa kupumua na kushindwa hata kupiga kelele kuomba msaada.

Wakati mwingine nilikuwa nikiona vivuli vikizunguka chumbani kwangu, vikicheka kwa sauti ya kutisha, na mara nyingine nilihisi kama kuna mikono isiyoonekana ikinishika shingoni.

Wakati wa mchana hali haikuwa tofauti sana, nilikuwa nikihangaishwa na hofu isiyo na sababu, uchovu uliokithiri na migogoro isiyoisha katika maisha yangu. Nilijua wazi kwamba haya yote yalikuwa matokeo ya uchawi uliokuwa unanifuata kila mahali.

Kazi yangu ilianza kudorora kwa sababu nilikosa nguvu ya kufanya chochote. Ndugu na marafiki walianza kunitazama kama mtu asiye na msaada, na wengine walidhani nimechanganyikiwa. Nilijitahidi kutafuta msaada wa kawaida kwa madaktari na hata kwa maombi yangu ya binafsi, lakini mambo yaliendelea kuwa mabaya zaidi. Soma zaidi hapa 

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela ameendelea na ziara zake katika baadhi ya matawi ya jijini Dar es Salaam kukutana na wateja ikiwa ni siku chache baada ya Benki kukamilisha maboresho makubwa ya mfumo wake mkuu wa utoaji huduma (Core Banking System).

Akiwa katika tawi la CRDB TPA lililopo katika jengo la Bandari jijini Dar es Salaam alikozungumza na mameneja wa matawi ya Kanda ya Dar es Salaam na Pwani pamoja na wanahabari, Nsekela alipata fursa pia ya kuzungumza na wateja waliokuwa wakihudumiwa. Aliwashukuru wateja kwa ushirikiano na uvumilivu wao katika kipindi cha mabadiliko huku akiwahakikishia kuwa huduma za Benki zinaendelea kuimarika kila siku tangu kuanza kutumika kwa mfumo mpya.

“Kuanzia tarehe 8 Septemba tulihamia kwenye mfumo mkuu wa utoaji huduma za benki ambapo, kwa ukubwa wa mabadiliko yaliyofanyika, baadhi ya wateja wetu walipata changamoto katika akaunti zao na baadhi ya miamala kutofanikiwa. Juhudi za wataalamu wetu zimefanyika usiku na mchana, na hadi jana akaunti zilizokuwa na changamoto zilirudi katika hali yake ya kawaida. Aidha, wateja ambao miamala yao ilikwama walirudishiwa fedha katika akaunti zao na miamala kuendelea kufanyika kwa ufanisi,” amesema Nsekela.

Aidha, Nsekela amebainisha kuwa uwekezaji mkubwa uliofanyika katika mfumo huu mpya umezingatia mahitaji ya sasa na ya baadaye ya wateja, na mabadiliko hayo yametekelezwa katika nchi zote ambako Benki ya CRDB inafanya biashara yaani Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) - huduma zinaendelea vizuri. Vilevile, ameongeza kuwa mageuzi hayo yanaweka msingi wa Benki kujitanua kimataifa, ambapo hivi karibuni Benki ya CRDB imepata leseni ya kuanzisha ofisi Dubai.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi Mtendaji amesema kuwa pamoja na mabadiliko yaliyotokea, Benki bado imeendelea kufanya vizuri kibiashara ikithibitisha imani kubwa ya wateja waliyonayo kwa Benki yao. Vilevile ametumia fursa hiyo kuwashukuru wafanyakazi wote kwa kujitoa kwao katika kipindi hiki cha mabadiliko na akawahimiza kuendelea kusimamia weledi katika utoaji huduma ili kuhakikisha mfumo mpya unaleta matokeo yaliyokusudiwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Abdulmajid Nsekela (kushoto) akihudumia na kupokea maoni ya wateja kuhusu maboresho ya mfumo mkuu wa uendeshaji wa huduma yaliyofanyika hivi karibuni katika tawi la Benki ya CRDB TPA lililopo katika Jengo la bandari jijini Dar es Salaam. 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (katikati) akiangalia namna huduma zinavyotolewa kwa wateja kupitia mfumo mkuu wa uendeshaji wa huduma ulioanza kutumika hivi karibuni. Amefanya ukaguzi huo katika tawi la Benki ya CRDB TPA lililopo katika Jengo la bandari jijini Dar es Salaam alikotembelea kusikiliza na kupokea maoni ya wateja kuhusu maboresho ya yaliyofanyika hivi karibuni.
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (kushoto) akimsikiliza Lella Mushi, mmoja wa mawakala wanaotoa huduma za Benki ya CRDB alipomkuta katika tawi la Benki ya CRDB TPA lililopo katika Jengo la bandari jijini Dar es Salaam alikotembelea ili kusikiliza na kupokea maoni ya wateja kuhusu maboresho ya mfumo mkuu wa uendeshaji wa huduma yaliyofanyika hivi karibuni.

 

 

Na Mwandishi Wetu,Korogwe

Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa kupitia Afisa Mwandamizi kutoka Ofisi ya hiyo Bi Edna Assey, amewaasa Viongozi wa Vyama vya siasa vitakavyoshiriki katika uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 2025, kuzingatia Sheria ya Usajili wa Vyama vya siasa na Sheria ya Gharama za Uchaguzi zinazosimamiwa na Ofisi hiyo, hasa katika kipindi hiki cha kampeni za kuelekea Uchaguzi Mkuu.

Pamoja na mambo mengine, Akitolea Ufafanuzi wa Sheria hizo wakati wa Mafunzo kwa Wenyeviti na Makatibu wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, Bi Edna Aliongelea makatazo yaliyopo katika Sheria hizo na adhabu zake akitolea mfano wa matumizi ya maneno ya matusi kashfa na dhihaka yanayoweza kupelekea uvunjifu wa Amani na kuwaasa kunadi Sera za vya vyama kistaarabu kwa wafuasi na wananchi ili kuweza kuchaguliwa.


Mafunzo hayo yaliyohusisha viongozi wa vyama hivyo kutoka Halmashauri ya Mji Korogwe na Korogwe vijijini yamefanyika Tarehe 12 Septemba 20225 mjini Korogwe.


Timu ya watalaamu kutoka TEITI ikitembelea baadhi ya miradi ya CSR, ikiwemo ya elimu katika vijiji vilivyo jirani na mgodi wa North Mara
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Barrick North Mara, Apolinary Lyambiko, akizungumza na watalaamu kutoka TEITI waliotembelea mgodi huo.
**

Na Mwandishi Wetu, Tarime

Timu ya wataalamu wa Taasisi ya Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikali katika Rasilimali za Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) ilitembelea Mgodi wa Dhahabu wa North Mara Septemba 11, 2025 kujionea mchango wake kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

 


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha.Felchesmi Mramba ameeleza kuwa matumizi ya nishati safi ya kupikia nchinj yameongezeka kutoka asilimia  6.9 mwaka 2021 hadi asilimia 20.3 huku lengo likiwa ni kufikia asilimia 80 ndani ya miaka 10, ambapo hadi sasa imebakia miaka 9.

Mha. Mramba ameyasema hayo Septemba 12, 2025 jijini Dar es Salaam wakati akizindua Kongamano la  Nishati Safi ya Kupikia lililoandaliwa na kampuni ya Mwananchi kwa ushirikiano  na Wizara ya Nishati pamoja na wadau mbalimbali likibebwa na kaulimbiu ya  ‘Nishati safi ya Kupikia Okoa Maisha, Linda Mazingira.

Akizungumza  wakati wa uzinduzi huo, Mha. Mramba amesema  “Nishati Safi ya Kupikia siyo jambo la kinadharia bali ni jambo linalohusu maisha, mazingira na uchumi huku msingi wake mkuu ukiwa ni kulinda afya, mazingira pamoja na maendeleo jumuishi.” 

Aidha, Mhandisi Mramba ameendelea kuwahamasisha wananchi kutumia nishati safi ya kupikia akikumbusha kuwa, takwimu zinaonesha kuwa takribani watanzania 33,000 hupoteza maisha kila mwaka kutokana na magonjwa ya mfumo wa kupumua ambayo kwa kiasi kikubwa huchangiwa na uvutaji wa moshi unaotokana na matumizi ya nishati isiyo safi ikiwemo kuni na mkaa.

Ameeleza kuwa kutokana na athari hizo   Serikali chini ya uongozi wa Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan,  imeandaa Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia 2024–2034 uliozinduliwa mwezi Mei 2024 ambao utawezesha asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati safi ya kupikia.

Sanjari na hayo, Mha. Mramba amemshukuru Rais,  Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ni kinara wa nishati safi ya kupikia kitaifa na kimataifa kwa Uongozi wake wa mfano na dhamira yake ya dhati ya kuhakikisha kila Mtanzania anatumia nishati safi, salama na nafuu ya kupikia.