Watendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) na wenzao wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), leo 23 Desemba 2025, wamekutana na kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano wa utendaji hususani katika usimamizi wa masuala ya kikodi yanayotokana na huduma zinazodhibitiwa na EWURA.

 

 


Na Ashrack Miraji

Waziri wa Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka, amewataka viongozi wa Mikoa, Wilaya, Halmashauri na Kata kuacha tabia ya kukaa ofisini na badala yake kushuka chini kuwafuata vijana ili kuwaeleza fursa mbalimbali za kimaendeleo zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kuwainua kiuchumi.

Akizungumza na vijana wa Jimbo la Same Mashariki mkoani Kilimanjaro, Waziri Nanauka alisema viongozi hao wana wajibu wa kuwafikia vijana moja kwa moja kwenye maeneo yao na kuwapatia taarifa sahihi kuhusu fursa za mikopo, mafunzo, ajira na miradi mbalimbali ya kiuchumi inayotolewa na Serikali.

Alisema katika ziara zake tangu ateuliwe kuwa Waziri wa wizara hiyo, amebaini kuwa idadi kubwa ya vijana hawana taarifa za fursa za maendeleo zinazotolewa na Serikali, hali inayosababisha fursa hizo kuwafikia vijana wachache huku wengi wakibaki nyuma kwa kukosa taarifa.


“Nimegundua taarifa nyingi za fursa za vijana hubaki kwa makundi machache. Serikali ya Awamu ya Sita inataka kila kijana, bila kujali itikadi au eneo alipo, apate taarifa na kunufaika na fursa hizi,” alisema Waziri Nanauka.

Aliongeza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameagiza fursa zote zinazohusu vijana zitolewe kwa uwazi na usawa, huku viongozi wa ngazi zote wakihamasishwa kuhakikisha vijana wanapata elimu ya namna ya kuzitumia fursa hizo kwa maendeleo yao binafsi na Taifa kwa ujumla.


Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki, Anne Kilango, alisema kundi la vijana ni kubwa kuanzia ngazi ya dunia, Taifa hadi jimbo lake, akieleza kuwa takribani asilimia 64 ya wakazi wa jimbo hilo ni vijana, hivyo linahitaji mikakati madhubuti ya kuwawezesha kiuchumi.

Kilango alisema miradi mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa ndani ya jimbo hilo imeongeza imani ya vijana kwa Serikali, ikiwemo mradi wa ujenzi wa barabara ya Mkomazi–Kisiwani Same yenye urefu wa kilomita 101 inayojengwa kwa kiwango cha lami, ambayo imefungua fursa za kiuchumi na kijamii kwa vijana wa eneo hilo.

Naye Waziri Nanauka aliahidi kushughulikia changamoto zilizowasilishwa na vijana, hususan miundombinu ya umwagiliaji, akisema Serikali inaendelea kutenga rasilimali ili kuboresha kilimo cha umwagiliaji kwa mazao ya kimkakati yanayolimwa na vijana ili kuongeza tija na kipato.

Kwa upande wao, vijana waliohudhuria mkutano huo, wakati wakiwasilisha risala yao kwa Waziri, walisema wanakabiliwa na changamoto ya miundombinu ya umwagiliaji katika kilimo cha tangawizi kwenye kata za milimani pamoja na kilimo cha mpunga katika kata za tambarare, wakiiomba Serikali kuharakisha upatikanaji wa miradi ya maji kwa ajili ya kilimo.






 

 


 

·       Waziri Akwilapo Ataka Kukamilisha malipo ifikapo Desemba 31, 2025

 

·       Aagiza Vituo vya Makusanyo ya Kodi kutoa huduma bora

 

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo ameelekeza wadaiwa wote wa Kodi ya Pango la Ardhi nchini wawe wamekamilisha malipo ya madeni yao kufikia  Desemba 31, 2025.

 

Akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Masasi mkoani Mtwara leo tarehe 23 Desemba 2025 Mhe. Dkt Akwilapo amesema, kuchelewa kulipwa kodi ya pango la ardhi kutasababisha wamiliki wa ardhi kuwa na malimbikizo ya madeni pamoja na riba. 

 

Kwa mujibu wa Waziri huyo wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, madhara mengine yanayoweza kutokea kwa wamiliki ambao hawajalipa kodi ya pango la ardhi kwa wakati ni pamoja na kufikishwa mahakamani na kufutiwa umiliki wa ardhi. Hatua hiyo ni kwa mujibu wa sheria ya ardhi Sura ya 113 Fungu la 48 (1), 50,  51 na 52.

 

Mhe. Dkt Akwilapo ameelekeza vituo vyote vya makusanyo ya kodi ya pango la ardhi katika ofisi za ardhi za mikoa na halmashauri nchini kuhakikisha vinatoa huduma bora za kuwasaidia wananchi wanaopata changamoto za kulipa kodi hiyo kwa kuzingatia utu pale wanapotekeleza majukumu yao

Katibu Mtendaji wa Mpango wa Hiari wa Nchi za Umoja wa Afrika wa Kujitathmini kwa Vigezo vya Utawala Bora (APRM) Tanzania, Bw. Lamau Mpolo, amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa wanafunzi kutoka vyuo vikuu mbalimbali nchini.

Lengo la kikao hicho lilikuwa kujadili nafasi ya vijana katika kukuza dhana ya Utawala Bora kama nguzo muhimu ya kuimarisha amani na usalama nchini Tanzania.

Katika kikao hicho, Bw. Mpolo alisisitiza umuhimu wa ushiriki wa vijana katika masuala ya utawala, akieleza kuwa vijana ni rasilimali muhimu katika kujenga jamii yenye uwajibikaji, uwazi na maamuzi jumuishi.

Kikao hicho cha siku moja kilifanyika Desemba 22, 2025, katika Ofisi za APRM zilizopo katika jengo la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi ,akizungumza wakati wa ziara yake katika Baraza la Ushindani (FCT) Jijini Dar es Salaam.

....

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi (Mb), ameliagiza Baraza la Ushindani (FCT) kuendelea kusimamia na kulinda ushindani wa haki ili kuondoa vitendo vya ukiritimba, hususan katika suala la kupandisha bei za bidhaa na huduma.

Ameyasema hayo wakati wa ziara yake katika Baraza la Ushindani Desemba 22, 2025 Jijini Dar es Salaam akisisitiza kuwa ushindani wa haki ni msingi muhimu wa ukuaji wa biashara, kwani vitendo vya ukiritimba vimekuwa vikiathiri biashara nyingi na walaji.

Ameeleza kuwa biashara zinapaswa kufanyika kwa kuzingatia ulinzi wa walaji, ambapo bei za bidhaa na huduma ziwe za haki, bidhaa ziwe na ubora, na uchunguzi wowote ufanyike kwa haki na kwa kuzingatia misingi ya kisheria.

Mhe. Katambi amebainisha kuwa Serikali inaendelea kuhamasisha uwekezaji kwa kuboresha sera rafiki, kufanya marekebisho ya sheria na kuendelea na maboresho ya mazingira ya biashara ili kuhakikisha Tanzania inakuwa mahali salama na rafiki kwa kufanya biashara bila kuweka vikwazo kwa wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi.

Amesisitiza kuwa haki katika utatuzi wa migogoro ni kipaumbele, kwa kulinda muda, heshima na maslahi ya wawekezaji na kusimamia sheria za ushindani, ndani na nje ya nchi, kwa lengo la kumlinda mlaji ili awe mnufaika mkuu wa shughuli za kibiashara.

Kwa niaba ya Mwenyekiti wa Baraza la Ushindani Jaji Rose Ibrahim, Dkt. Onesmo Kyauke amesema Baraza la Ushindani lina nafasi ya kipekee katika kuhakikisha malengo ya sera ya ushindani nchini yanatekelezwa kwa ufanisi, hususan kupitia usikilizaji wa rufaa na mashauri yanayotokana na maamuzi ya Tume ya Ushindani pamoja na mamlaka za udhibiti wa soko.

Amesema hatua hiyo inasaidia kujenga mazingira bora ya biashara, kuvutia uwekezaji na kulinda maslahi ya walaji na washiriki wote wa soko.

Kwa miaka kadhaa, suala la kushika mimba lilikuwa kivuli kizito katika ndoa yetu. Tulifanya vipimo, tukafuata ratiba, tukabadili mlo, na tukazingatia ushauri wote wa kawaida tuliopata.

Kila mwezi tulikuwa na matumaini mapya, na kila mwezi uliisha na ukimya ule ule. Haikuwa rahisi kuzungumza kuhusu hilo, hata kati yetu wenyewe. Shinikizo la familia na maswali ya watu viliongeza uzito tulioubeba kimya kimya.

Kadri muda ulivyopita, nilianza kuhisi kuchoka kiakili. Sio kwa sababu hatukuwa tunajaribu, bali kwa sababu jitihada zetu zilionekana hazizai matunda.

Tulihitaji mwelekeo tofauti, si kwa kukata tamaa, bali kwa kutafuta ufahamu mpana zaidi kuhusu miili yetu. Ndipo tukaanza kufikiria njia za asili, kwa tahadhari na kwa nia ya kujifunza. Soma Zaidi................
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/maumivu-ya-ghafla-yalinifanya-nidhani-ni-mwisho-baadaye-nikagundua-mawe-ya-figo-yanatibika-kwa-mitishamba/

Kwa miaka kadhaa, suala la kushika mimba lilikuwa kivuli kizito katika ndoa yetu. Tulifanya vipimo, tukafuata ratiba, tukabadili mlo, na tukazingatia ushauri wote wa kawaida tuliopata.

Kila mwezi tulikuwa na matumaini mapya, na kila mwezi uliisha na ukimya ule ule. Haikuwa rahisi kuzungumza kuhusu hilo, hata kati yetu wenyewe. Shinikizo la familia na maswali ya watu viliongeza uzito tulioubeba kimya kimya.

Kadri muda ulivyopita, nilianza kuhisi kuchoka kiakili. Sio kwa sababu hatukuwa tunajaribu, bali kwa sababu jitihada zetu zilionekana hazizai matunda.

Tulihitaji mwelekeo tofauti, si kwa kukata tamaa, bali kwa kutafuta ufahamu mpana zaidi kuhusu miili yetu. Ndipo tukaanza kufikiria njia za asili, kwa tahadhari na kwa nia ya kujifunza. Soma Zaidi................
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/tulijaribu-kila-njia-ya-kawaida-ya-kushika-mimba-kabla-hatujafikiria-njia-ya-asili-iliyofanya-kazi/
Kulikuwa na kipindi ambacho amani ilinipotea ghafla. Hakukuwa na ugomvi mkubwa, ugonjwa uliotambulika, wala msiba uliotokea. Hata hivyo, nilikuwa na hofu isiyoelezeka, usingizi ulikatika, na moyo wangu haukutulia.

Nilifanya kila nilichodhani ni sahihi kupumzika, kujishughulisha, kuzungumza na watu wa karibu ila utulivu haukurudi. Kadri siku zilivyopita, nilianza kujiuliza maswali mengi. Kwa nini hali hii ilinijia bila dalili?
Kwa nini nilihisi kama kuna kitu kinanizuia kuendelea mbele, hata kwenye mambo niliyoyapenda? Nilihitaji ufafanuzi ulioenda zaidi ya nilichokuwa nikiona juu juu. Ndipo nikafikiria kusikiliza hekima ya asili.Soma Zidi...........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilipoteza-amani-bila-sababu-inayoonekana-ufafanuzi-wa-kienyeji-ulinipa-mwanga/
Kwa muda mrefu, nyumba yetu haikuwa na utulivu. Hakukuwa na ugomvi mkubwa unaoonekana, ila kulikuwa na mvutano wa kila siku. 

Watoto walikuwa wakigombana mara kwa mara, mimi na mwenzi wangu tulizungumza kwa sauti nzito, na hata mambo madogo yaligeuka kuwa makubwa.

Nilijiuliza ni wapi tulikosea, maana tulijitahidi kuwa wazazi na wenzi wema. Nilijaribu kubadilisha ratiba, kuanzisha mazungumzo ya familia, na hata kupuuza baadhi ya mambo ili kulinda amani. Haikudumu.

Kila tulipojaribu kusonga mbele, kulikuwa na kitu kilichoturudisha nyuma. Ndani yangu, nilihisi kama kuna mzigo usioonekana uliokuwa umeikalia familia yetu.Soma Zaidi..............
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/familia-yetu-ilikosa-baraka-ya-utulivu-tulipoelewa-chanzo-njia-ikafunguka/

WATOA huduma za mionzi kwenye vituo mbalimbali vya afya nchini wameagizwa kuepuka kiwango kikubwa cha mionzi kwa wagonjwa na kwao ili kisiweze kuleta madhara zaidi

Hayo yalisemwa jana Jijini Arusha na Kaimu Mkuu wa Ofisi ya Kanda ya Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC), Peter Pantaleo wakati wa kufunga mafunzo yaliyoshirikisha wataalam wa Radiolojia zaidi ya 90 yaliyotolewa na tume hiyo

Pantaleo alisema kiwango kikubwa cha mionzi kinamadhara zaidi kuliko kiwango kidogo hivyo wataalam hao wanapaswa kuepuka viwango hivyo vikubwa ili kuzuia madhara

Alisema pia watoa huduma hiyo lazima wajue pia kunawagonjwa wanaohitaji huduma hiyo kwa usalama zaidi ikiwemo kuwakinga wale walioambatana nao 

"Mafunzo haya ni muhimu kwa wataalam wa mionzi ili kuhakikisha usalama wao na kwa wale wanaopata huduma hiyo au kwa wale wanaokwenda hospitali"

Huku mkufunzi wa mafunzo hayo, Mungubariki Nyaki alisisitiza wataalam hao kuhakikisha wanatoa huduma nzuri kwa wagonjwa ikiwemo  kuzingatia matumizi sahihi ya mionzi hiyo

"TAEC itaendelea kutoa mafunzo katika kada mbalimbali katika kuhakikisha watoa huduma na wataalam wa mionzi wanajikinga na mionzi lakini pia huduma za mionzi ni salama hivyo wagonjwa wasiogope kwani mionzi imedhibitiwa"

Wakati huo huo baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo Beatrice Mallya na Hussein Shabani walishukuru TAEC kwa kutoa mafunzo hayo ambayo yanakumbusha kutumia kwa usahihi mionzi hiyo pamoja na kuhakikisha vyumba vinavyotolea huduma hiyo vinakuwa vya kisasa zaidi

Huku  Shabani alisisitiza matumizi sahihi ya mionzi ndio chachu ya huduma bora kwa wagonjwa wanaofika hospalini kupata huduma hizo

Na Munir Shemweta, WANMM MTWARA

 

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo leo tarehe 22 Desemba 2025 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala.

 

Mhe. Dkt Akwilapo ambaye yuko ziarani mkoani Mtwara amemueleza Kanali Sawala juhudi za wizara yake katika kushughulikia changamoto za sekta ya ardhi nchini.

 

"Sisi kama wizara tutazifanyia kazi changamoto zote za sekta ya ardhi na hapa Mtwara tayari tumeshaanza kuzifanyia kazi, lengo ni kutaka kuwaacha wananchi wetu wawe na furaha". Amesema

 

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Sawala amempongeza Mhe. Dkt Akwilapo kwa kuaminiwa na Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kuteuliwa kuwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi wizara aliyoieleza kuwa ni nyeti kutokana na kugusa maisha ya kila mtu.

 

"Nikuahidi Mhe. Waziri sisi kama mkoa tutajitahidi kukusemea kwa yale yote mazuri unayofanya katika mkoa wetu". Amesema Kanali Sawala

 



Na Munir Shemweta, WANMM MASASI

 

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amesema wizara yake haitaki watumishi wa sekta ya ardhi kuwa sehemu ya migogoro ya ardhi nchini.

 

Mhe. Dkt Akwilapo ametoa kauli hiyo leo tarehe 22 Desemba 2025 wilayani Masasi wakati alipowasili wilayani Masasi na kupokelewa kwa mara ya kwanza tangu ateuliwa kuwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

 

"Kuanzia sasa hatutaki mtumishi wetu awe sehemu ya tatizo tukigundua wewe mtumishi wa sekta ya ardhi umekuwa sehemu ya tatizo basi wewe siyo mfanyakazi wetu na hilo tutalisimamia". Amesema

 

Amebainisha kuwa, matatizo ya ardhi yapo na yanatengenezwa na watumishi wa sekta ya ardhi pamoja na wananchi ambapo ameweka wazi kuwa, matatizo yaliyotengenezwa basi wizara yake itayatatua.

 

"Hatupendi kufukuza kazi watumishi maana tunajua kila mfanyakazi anategemewa na kumfukuza itakuwa kitu cha mwisho lakini kuna mahali inabidi sheria ifuate mkondo wake.

 

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo yupo wilayani Masasi mkoa wa Mtwara ambapo pamoja na mambo mengine atakutana na wananchi wa jimbo lake kwa lengo la kusikiliza na kizitafutia ufumbuzi changamoto mablimbali jimboni humo

Baada ya kunicheat, uhusiano wetu ulivunjika vibaya. Aliniambia waziwazi hatarudi tena, hata nikijaribu kiasi gani. Maneno yake yaliniumiza, sio tu kwa sababu ya kuachwa, bali kwa sababu nilijua nilikuwa nimekosea.

Nilijilaumu, nikajuta, na nikaanza safari ngumu ya kujijenga upya nikiwa peke yangu. Sikuanza kwa kumfuata. Nilianza kwa kujitazama. Nilijifunza kukaa kimya, kukubali makosa yangu, na kubadilisha mienendo yangu.

Nilijenga nidhamu, nikabadilisha marafiki, na nikaanza kujiheshimu tena. Mabadiliko hayo hayakuwa ya kuigiza; yalitoka moyoni. Hapo ndipo nilitambua kuwa hata asiporudi, nilihitaji kupona mimi kwanza. Soma Zaidi........
https://kiwangadoctor.com/kiswahili/ex-aliapa-peupe-hatanirudia-baada-ya-kucheati-njia-hii-ya-kipekee-ilimvuta-kurudi/