Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda amekutana na kuzungumza na Wakuu wa Mikoa ya Mwanza Mhe. Said Mtanda na Mhe. Nurdin Babu na kujadiliana nao mambo Mbalimbali kuhusu Maendeleo ya Mikoa yao.

Viongozi hao waliofika mkoani Arusha kwa shughuli mbalimbali, wamesifu Maandalizi makubwa yaliyofanyika kuelekea maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani yanayotarajiwa kufanyika Jumatano hii kwenye Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Mjini Arusha.

Viongozi hao walioambatana na baadhi ya wasaidizi wao walipata fursa pia ya kujionea shughuli mbalimbali za sanaa zinazoendelea Mjini Arusha kama sehemu ya Shamra shamra za kuelekea kwenye Sherehe za Wafanyakazi.

Wakizungumza na Wananchi waliojitokeza kushuhudia maonesho mbalimbali ya sanaa kuelekea Mei Mosi, Mhe Mtanda amemtaja Mhe. Makonda kama Kiongozi wa Kupigiwa Mfano kutokana na Umahiri na Ubunifu wake katika Uongozi na namna anavyojitoa kushughulikia masuala ya wananchi.

Wakuu hao pia wamesifu namna ambavyo Arusha Imebadilika katika muda mfupi tangu kuteuliwa kwa Mhe. Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mwishoni mwa Mwezi Machi.

Shamrashamra Mbalimbali zinaendelea Mjini Arusha kuelekea sherehe za Mei Mosi suala ambalo limeamsha hisia za watu wengi wanaojitokeza kwenye Viunga vya Jiji la Arusha ili kujionea shughuli mbalimbali za sanaa kutoka kwa vikundi vya Ngoma, dansi na Kikundi cha vijana wa kucheza na Pikipiki Maarufu kama dede.















  


Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Komredi Jokate Urban Mwegelo (MNEC) amesema Viongozi Wakuu wa Chama Cha Mapinduzi Wana Imani kubwa na Vijana hivyo Vijana wana Kila  Sababu ya Kufanya kazi kwa bidii kulilinda Imani hiyo.

"Sisi wote ni Mashahidi wa mambo makubwa yanayofanywa na Viongozi wetu na kama mtakumbuka Juzi tarehe 26 Aprili tumetoka kusherekea Sherehe za Miaka Sitini (60) ya Muungano wetu kwa namna ya kipekee sana na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika hotuba yake aliyoitoa kwa Wananchi alionyesha ni kwa kiasi gani Vijana ndio nguvu kazi ya Taifa kutokana na Wingi wetu"

"Serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Serikali yetu ya Mapinduzi ya Zanzibar zimewekeza kubwa kwa Vijana wote wa Kitanzania na Viongozi wetu Wakuu wana Imani kubwa na sisi Vijana katika ujenzi wa Taifa letu, Hivyo tuna wajibu wa Kuilinda Imani hii Kubwa lakini pia kuulinda Muungano wetu kwa wivu mkubwa sana". Alisema Komredi Jokate.









Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko mewataka waajiri kwa kushirikiana na wadau wanaendelea kuboresha mazingira ya kazi ili kuongeza usalama mahala pa kazi na kuwawezesha watumishi kufanya kazi katika mazingira rafiki na hivyo kukuza uzalishaji na kupunguza gharama za uzalishaji.

Dkt. Biteko amesema hayo (leo Aprili 28, 2024) Jijini Arusha katika maadhimisho ya kilele cha Siku ya Usalama na Afya Mahali Pa kazi Duniani.

 " Niwatake waajiri na waajiriwa kuhakikisha usalama mahali pa kazi, mtu wa kwanza kujali usamala wake ni mwajiriwa, ukiona mtambo hauko salama toa taarifa kwa mwajiri wako; hapa hautaonekana umegoma bali ni kuhakikisha mazingira ya kazi yanakuwa salama ", amesema Dkt. Biteko.

Ameitaka OSHA kwa kushirikiana na wadau katika masuala ya usalama mahali pa kazi kuhakikisha wafanyakazik wanakuwa na mazingira yatakayowawezesha kuwa salama na kupata furaha na matumaiani kisha kupata ari ya kuendelea kufanya kazi na kuongeza ufanisi kazini. 

Amehimiza OSHA kuendelea kutoa elimu kuhusu wa usalama mahali pa kazi badala ya mfumo wa kizamani ambapo mwajiri na mwajiriwa walikuwa wakiogopana na kuhofiana kutokana na kufanya kazi za “KIPOLISI”

Amesema pamoja na hatua zinazochukuliwa kutoa elimu, bado elimu zaidi inahitajika kuhakikisha kwamba pande husika zinaendana na matakwa ya kitaifa na kimataifa.

Aidha, amewataka Watanzania kwa ujumla kuhakikisha wanakuwa mkakati waw a upandaji miti nah atua nyingine za kukabiliana na madhara ya tabia nchi kama vile kuhifadhi vyanzo vya maji.

 Kwa upande wake, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Patrobasi Katambi akimwakilisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu, Mhe. Jenista Mhagama amesema Serikali inashirikiana ILO kuhakikisha Tanzania inazingatia usalama na afya mahala pa kazi.

 " Serikali ina wajibu wa kilinda nguvu kazi ya Taifa kwa kuwa afya njema ni mtaji wa nguvu kazi pia tunasheria ya kuhakikisha afya ya mzalishaji inalindwa", amesema Mhe. Kaatambi. 

 Naye, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda amesema kuwa wafanyakazi ni wadau muhimu katika kufikia malengo ya taifa hivyo tukio hili lina lengo la kuhamasisha kuhusu usalama mahala pa kazi ili kukuza uwekezaji na mafanikio yanayotarajiwa katika nchi.

 "OSHA tutaendelea kusimamia majukumu yetu kwa mustakabali wa Taifa letu na tutaendelea kutoa elimu kuhusu umuhimu wa usalama na afya mahala pa kazi", amesema Bi. 

 Mkurugenzi wa Mkazi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO), Bi. Caroline Mugalla amesema kuwa kauli mbiu ya mwaka huu inaeleza umuhimu wa kuchukua taadhari ili kulinda afya za wafanyakazi. 

 " Naipongeza Serikali kwa kuridhia mikataba miwili ya mchakato huu unaendelea kupitia makubaliano ya pamoja baina ya Wafanyakazi na Serikali ili kuleta ufanisi mahali pa kazi na ILo tunaahidi kutoa ushirikiano kwao.

“Tunashuhudia nchi jirani zinakuja Tanzania kujifunza kuhusu usalama mahala pa kazi ILO tutaendelea kushirikiana nanyi". Amesema Bi. Caroline.

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waajiri (ATE) ametoa wito kwa Serikali na Waajiri kuweka mikakati ya kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa inayozingatia usalama na afya mahala pa kazi.

Aidha, Mwakikishi wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), Bi. Juliana Mpanduji amesema kuwa TUCTA itaendelea kushirikiana na Serikali, OSHA na ATE ili kulinda nguvu kazi kwa ajili ya maendeleo ya Taifa.

Madhimisho hayo ya Siku ya Usalama na Afya Mahala Pa Kazi yenye kauli mbiu "Athari za Mabadiliko ya Nchi katika Usalama na Afya Kazini: Jisajili na OSHA kushiriki Mapambano dhidi ya Athari hizo" yameambatana na shughuli mbalimbali ikiwemo semina kuhusu masuala ya usalama na afya mahala pa kazi.

Awali, Dkt. Biteko alikagua mabanda mbalimbali ya Ofisi, Taasisi, Mashirika na Mamlaka ambapo alipata maelezo kuhusu utendaji wake, ufanisi na changamoto wazokabiliana nazo. Kisha kupokea maandamano ya Madhimisho hayo ya Siku ya Usalama na Afya Mahala Pa Kazi yenye kauli mbiu "Athari za Mabadiliko ya Nchi katika Usalama na Afya Kazini: Jisajili na OSHA kushiriki Mapambano dhidi ya Athari hizo"




Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Komredi Jokate Urban Mwegelo (MNEC) amesema  Mikoa ya Kanda ya Kusisni Mtwara, Lindi na Ruvuma ni wanufaika wakubwa wa Miradi Mbalimbali ya Maendeleo ndani ya kipindi cha Miaka 3 ya Uongozi wa Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

 "Ndugu Vijana wenzangu; ninyi wote ni mashahidi ndani ya kipindi cha Miaka 3 Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan mmenugaifaika kwa ming ya Maendeleo"

"Pamoja na mambo mengi mazuri yaliyofanywa na Serikal yetu ndani ya Mikoa yetu hii katika sekta ya afya, miundombinu, Utalii, Elimu Lakini jambo kubwa na la kipekee sana ni Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini iliyopo Mikindani Mkoa wa Mtwara. Hospitali ambayo  inahudumia Wananchi wa mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma ambayo ujenzi wake umegharimu shilingi bilioni 15.8 haya yote ni Mapinduzi Makubwa katika Sekta ya Afya ndani ya Serikali ya Awamu ya Sita".




Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda ameagiza kupandishwa Mahakamani kwa watendaji wa Mkoa wa Arusha waliohusika na upotevu na wizi wa Milioni 428 zilizokuwa zimetengwa kwaajili ya mpango wa kunusuru kaya maskini TASAF.

Mbele ya wanahabari mjini Arusha, Mkuu wa mkoa Mhe. Paul Christian Makonda ametoa kauli hiyo mara baada ya kukamilika kwa uchunguzi uliokuwa ukifanywa na Taasisi ya kupambana na kuzuia Rushwa TAKUKURU mkoa wa Arusha.

Mhe. Mkuu wa mkoa ameiagiza TAKUKURU kufanya uchunguzi kwenye miradi yote saba ya mfuko wa TASAF mkoa wa Arusha ili kujiridhisha kuhusu thamani ya fedha iliyotumika kwenye miradi inayotekelezwa mkoani Arusha.

Katika hatua nyingine Mkuu wa mkoa Mhe. Paul Makonda ameonya kuhusu watendaji wabadhirifu na wanaoiba fedha za serikali na kusema hatofumbia macho mtu yeyote atakayeenda tofauti na miiko ya Utumishi wa Umma.

Mhe. Makonda ametangaza kuanza kwa uchunguzi maalum kuhusu matumizi ya fedha zinazotolewa na serikali kwaajili ya Utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Arusha na kuahidi kuchukuliwa kwa hatua za kisheria kwa wote watakaobainika kujihusisha na wizi na matumizi mabaya ya fedha za maendeleo.



Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Komredi Jokate Urban Mwegelo (MNEC) amewaasa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi kutembelea Vifua mbele katika kumsemea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuleta Maendeleo katika Taifa letu.

 Ndugu Vijana wenzangu tutembeee kifua mbele kumsemea Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwani kazi zake anazozifanya tunaziona"

"Ndugu zangu Cha Mapinduzi hakijawahi kukosea katika kuchagua na kuteua Viongozi hivyo tuna kila sababu ya kuhabarisha Umma juu ya Utekelezaji Kishindo wa Ilani ya CCM ya Mwaka 2020 uliofanywa na Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa upande wa Tanzania Bara lakini pia Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa upande wa Zanzibar". Alisema Komredi Jokate.






Na Imma Msumba : Ngorongoro

Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imezindua zoezi  la upigaji kura kuwania tuzo ya kivutio bora cha utalii barani Afrika kwa mwaka 2024 katika hafla iliyofanyika ukumbi wa Jengo la Ngorongoro Jijini Arusha.

Akizindua kampeni hiyo ya upigaji kura kaimu kamishna wa Uhifadhi NCAA Victoria Shayo amesema zoezi hilo litachukua siku 131 kuanzia mwezi huu wa aprili na linatarajiwa kukamilika mwezi Septemba 2024.

Amesema eneo la hifadhi ya Ngorongoro mwaka jana lilifanikiwa kushinda tuzo hiyo inayoandaliwa na mtandao wa World travel Awards baada ya kushinda katika kinyang’anyiro hicho kilichohusisha vivutio vingine vya Table Mountain, Harbeestpoort aerial cableway, V & A Waterfront, Ruben Island vya Afrika kusini, ziwa Malawi, Okavango Delta ya Botswana, Pyramids of Giza ya Misri pamoja na hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro hali iliyoitangaza nchi yetu na kuongeza idadi ya watalii.

Kamishna Shayo amesema tuzo hizo zina umuhimu mkubwa katika kuendeleza sekta ya utalii nchini na duniani kwa ujumla na kutoa wito kwa watanzania na wageni wote wanaotembelea Tanzania kuipiga kura nyingi Ngorongoro ili kuiwezesha Ngorongoro kutetea taji lake.

Akizungumzia kuhusu ongezeko la watalii nchini Kaimu Kamishna ameeleza kuwa mpaka kufikia nusu mwaka wa fedha wa 2023/24 hifadhi ya Ngorongoro imeshaingiza watalii zaidi ya laki saba ambapo wageni hao wameweza kuiwezesha mamlaka kupata zaidi ya shilingi bilioni 170.

Kwa upande wake Meneja wa Huduma za Utalii NCAA Mariam Kobelo ametoa wito kwa vyombo vya habari kuendelea kuwahamasisha wananchi kuhusiana na umuhimu wa kutembelea vivutio vya utalii na kupata elimu kuhusiana na vivutio hivyo.

Naye Afisa Utalii Mkuu  wa NCAA Bw. Peter Makutian amewapongeza wageni wote waliotembela hifadhi ya Ngorongoro ambao kutokana na hamasa yao ya kupiga kura kwa wingi mwaka 2023 kuliiwezesha hifadhi ya Ngorongoro kuwa kivutio bora cha utalii barani Afrika kwa mwaka 2023.

Katika mwaka huu wa 2024 jumla ya Nchi tano barani Afrika za tuzo hiyo ambazo ni Tanzania, Afrika Kusini, Botswana, Misri na Malawi zinawania tuzo hiyo.










Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Komredi Jokate Urban Mwegelo (MNEC) amemshukuru Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kupendekeza Jina lake mbele ya Halmashauri kuu kuwa Katibu Mkuu UVCCM Taifa. 

"Nitumie fursa hii kumshukuru sana kutoka kwenye sakafu ya Moyo wangu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi ambae pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu; kwa Imani kubwa aliyonayo kwangu na hatimaye leo hii nasimama mbele yenu nikiwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM)".

"Vilevile; nawashukuru sana kwa Mapokezi haya ya Kipekee yamefana sana na yanaendelea kuthibitisha kuwa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM ndio Jumuiya nambari moja tegemezi ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na kwamba Vijana tukipewa majukumu tunauwezo wa kuyasimamia kwa weledi mkubwa sana, nawashukuru sana".