Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imeshiriki mkutano mkuu wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania kwa lengo la kunadi vivutio vya utalii na kuimarisha ushirikiano kati ya Ngorongoro na Mahakama.
Mkutano huo uliofunguliwa tarehe 13 januari, 2026 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan unaendelea hadi tarehe 16 Januari, 2026 ambapo wadau mbalimbali wa sekta ya sheria kutoka maeneo tofauti ya nchi wanashiriki kujadili masuala mbalimbali yanayohusu haki, utawala wa sheria na maendeleo ya mfumo wa utoaji haki nchini.
Ujumbe wa Ngorongoro uliongozwa na Kamishna msaidizi mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia idara ya utalii na Masoko Mariam Kobelo pamoja na Afisa Uhifadhi mwandamizi-Sheria Usaje Mwambene ambapo mada mbalimbali kuhusu vivutio vya utalii, fursa za uwekezaji, huduma zinazotolewa na upekee wa Ngorongoro kama kivutio bora cha utalii barani afrika kwa mwaka 2023 na 2025.
Aidha, NCAA imetumia mkutano huo kujenga uelewa kwa wadau wa sheria kuhusu misingi ya kisheria inayosimamia uhifadhi wa rasilimali za asili ili kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii vinavyopatikana katika hifadhi hiyo ikiwemo Kreta za Ngorongoro, Empakai, Olmoti, maporomoko yaa maji endoro, Ndutu ambalo ni maarufu kwa mazalia ya nyumbu wanaaohama, mchanga unaohama, makumbusho ya olduvai, makumbusho na jiopaki na vingine vingi.
Na Mwandishi Wetu, WMTH – Dodoma
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Mb), amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ili kuwawezesha wadau wa sekta ya sanaa kufanya kazi zao kwa ubora na tija.
Waziri Kairuki ameyasema hayo tarehe 14 Januari 2026, alipofanya mazungumzo na mtengeneza maudhui ya mtandaoni, Bw. Vicent Pendael Njau maarufu kama KIREDIO, aliyefika katika ofisi za Wizara hiyo zilizopo Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma.
Katika mazungumzo hayo, masuala yaliyojadiliwa ni pamoja upatikanaji wa huduma ya intaneti ya uhakika, fursa za kujipatia kipato kupitia mitandao ya kijamii, pamoja na uwepo wa sera na mifumo ya kiserikali ikiwemo ya kikodi inayogusa sekta ya ubunifu na maudhui ya mtandaoni.
Waziri Kairuki alimpongeza Bw. Njau (Kiredio) kwa kazi nzuri anayofanya na kutoa wito kwa watengeneza maudhui pamoja na wasanii kwa ujumla kuzingatia maadili, mila na desturi za Kitanzania pindi wanapotengeneza maudhui yao na kabla ya kuyaweka mtandaoni.
Kwa upande wake, Kiredio ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwasikiliza vijana na kutambua mchango wao katika uchumi wa kidijitali, huku akiwasilisha changamoto mbalimbali zinazokabili sekta ya utengenezaji wa maudhui ili zifanyiwe kazi kwa wakati na kuiwezesha sekta hiyo kuendelea kukua.
Mazungumzo hayo yalihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Mohammed Abdulla pamoja na baadhi ya Viongozi wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, amekagua ujenzi wa bweni la wanafunzi wenye mahitaji maalum pamoja na kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa nyumba ya mlezi (matroni) katika Shule ya Msingi Segese, Halmashauri ya Wilaya ya Msalala. Miradi hiyo ina thamani ya zaidi ya shilingi milioni 490 na inalenga kuboresha mazingira ya upatikanaji wa elimu kwa kundi hilo muhimu katika jamii.
Mhe. Mhita alifanya ukaguzi huo Januari 14, 2025, alipokuwa kwenye ziara ya kukagua miradi ya maendeleo na kusikiliza kero za wananchi katika Kijiji cha Segese, Kata ya Segese.
Akizungumza baada ya kukagua miradi hiyo, Mkuu wa Mkoa aliipongeza Serikali kwa kuendelea kuwekeza katika sekta ya elimu, hususan kwa watoto wenye mahitaji maalum, akisema miradi hiyo itasaidia kuongeza usalama, malezi bora na mazingira rafiki ya kujifunzia kwa wanafunzi hao.
Ujenzi wa bweni la wanafunzi umegharamiwa kupitia fedha kutoka Serikali Kuu pamoja na mapato ya ndani ya Halmashauri ya Msalala. Aidha, ujenzi wa uzio wa bweni hilo umefadhiliwa na Kampuni ya Bulyanhulu Gold Mine (BARRICK) kupitia mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) kwa gharama ya shilingi milioni 238, huku ujenzi wa nyumba ya mlezi ukigharimu shilingi milioni 79.2.
Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Frank Nkinda ameshukuru Serikali kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya Elimu na kuwataka kuitunza na kuitumia vyema ili iweze kuwasaidia watoto hao wenye mahitaji maalum.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala Bi. Rose Manumba amesema ataendelea kuhakikisha miradi inasimamiwa vyema na kukamilika kwa wakati katika Halmashauri hiyo kusudi wananchi waweze kupata huduma bora na nzuri.
Akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo, Mkuu wa Shule ya Msingi Segese, Ndg. Alpha Matambo, amesema ujenzi wa majengo hayo utachangia kwa kiasi kikubwa kuongeza usalama, uangalizi na malezi bora kwa watoto wenye mahitaji maalum, tofauti na ilivyokuwa awali kabla ya utekelezaji wa miradi hiyo.
Amesema kukamilika kwa miradi hiyo kutaongeza ari ya wanafunzi kuhudhuria masomo na kuwapa wazazi na walezi imani ya kuwapeleka watoto wao shule katika mazingira salama na rafiki.
Nilihisi kukosa udhibiti wa biashara yangu, na hofu ilianza kunishika. Nilijua kwamba ikiwa sitafanya kitu haraka, kila kitu nilichojenga kitakuwa kimeharibika. Nilijaribu njia mbalimbali kupiga matangazo.
Kutoa punguzo, hata kuwasiliana moja kwa moja na wateja waliokuwa wanarudi mara kwa mara lakini matokeo yalikuwa hafifu. Hali ilikuwa mbaya kiasi kwamba siku moja nikakaa tu nikijaribu kuelewa ni wapi nilikosea.Soma Zaidi..https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilipoteza-wateja-wangu-wote-ghafula-lakini-njia-moja-niliyojaribu-iliwarudisha-kwa-kasi-isiyotarajiwa/
Nilikuwa nikiwa na ndoa ya miaka minne, lakini kila siku ilikuwa ni changamoto. Tulikuwa tukigombana mara kwa mara, hisia za hasira na huzuni zilijaza nyumba yetu. Kila jaribio la kuzungumza au kutafuta suluhisho lilimalizika kwa chuki na kuchukiana.
Nilihisi kwamba maisha yangu ya ndoa yalikosa maana na kila kitu kilikuwa kikienda mrama.
Hali ilikuwa mbaya kiasi kwamba nilianza kujiuliza kama nilikuwa nimechagua mke sahihi.
Nilijaribu kila kitu; kuzungumza, kujaribu upendo, hata kutafuta ushauri wa rafiki, lakini hakuna kilichofanya tofauti. Hisia za upweke na huzuni zilikuwa sehemu ya maisha yangu ya kila siku. Soma Zaidi.....https://kiwangadoctor.com/kiswahili/miaka-nne-ndoani-bila-amani-kilichobadilika-baada-ya-kuchukua-uamuzi-mmoja-kilinishangaza-mwenyewe/
Lakini ghafla alibadilika. Alinitupa bila sababu ya wazi. Aliniacha nikihisi kuchukuliwa na kutupwa bila huruma. Siku za mwanzo nilijaribu kukabiliana na maumivu haya peke yangu, lakini kila jaribio liliishia kwa huzuni na hisia za upweke.
Nilihisi kuwa maisha yangu yalikuwa yamevunjika. Hata hivyo, mambo yalibadilika baada ya muda mfupi. Bila mimi kujitahidi, alianza kunisumbua kila siku.
Nilihisi kuharibika kihisia. Kila kitu kilionekana kuwa nje ya udhibiti wangu. Nilihisi hisia za hasira, kuchoshwa, na hofu kwa kila hatua yake. Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/alinitupa-bila-majuto-lakini-muda-mfupi-baadaye-alianza-kunisumbua-kila-siku-bila-mimi-kujitahidi/
Hali yangu ya hofu ilinifanya nishindwe hata kufanya kazi za kawaida nyumbani. Nilijaribu njia nyingi za kujilinda. Nilipata kila aina ya vidokezo kutoka kwa majirani na marafiki. Lakini hakuna kilichonisa matokeo.
Kila mara nilihisi hatari iko karibu. Nilihisi kama kila kitu kilikuwa kikinikabili, na siku nzima ilinifanyia shaka. Soma Zaidi........https://kiwangadoctor.com/kiswahili/nilihofia-usalama-wangu-mwaka-huu-hatua-nilizochukua-kuweka-kinga-yangu-iliyobadilisha-kila-kitu/
Nilijaribu dawa za kawaida, lakini mara nyingi zilikuwa kali sana au hazikutoa nafuu.
Nilijaribu njia mbalimbali za asili na mbinu za kitamaduni. Baadhi zilikua huru kwa muda mfupi, lakini maumivu yalirudi mara nyingi zaidi.
Nilihisi kuchanganyikiwa na kuchoka. Mara nyingine nilikuwa naogopa kuwa hali yangu ingeendelea kuwa mbaya zaidi, na maisha yangu ya kila siku yalikuwa kwenye hatari. Soma Zaidi...https://kiwangadoctor.com/kiswahili/kila-siku-nilikuwa-nikipata-maumivu-makali-ya-tumbo-hatua-moja-ilinisaidia-kupona-bila-dawa-kali/
Na. Joseph Mahumi na Saidina Msangi, WF, Dodoma.
Tanzania na Indonesia zimekubaliana kuendeleza zaidi ushirikiano wa kimaendeleo katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii ikiwemo kilimo na nishati kwa faida ya nchi hizo mbili.
Hayo yamebainishwa jijini Dodoma, baada ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omary (Mb), kukutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Tri Yogo Jatmiko Avetisyan.
Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Balozi Omar, ameishukuru Serikali ya Indonesia kwa mchango wake mkubwa katika kusaidia sekta mbalimbali za uchumi wa Tanzania ikiwemo sekta za madini, kilimo na mifugo tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia mwaka 1964.
“Mwaka huu ni maadhimisho ya miaka 62 tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Indonesia, na uhusiano wetu umeendelea kuimarika zaidi kadiri miaka inavyosonga mbele, na pia tumeona ziara kati ya viongozi wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipotembelea Indonesia, na Mhe. Prabowo Subianto Rais wa Indonesia alipokuja Tanzania, hii ni ishara ya uhusiano thabiti unaojengwa juu ya heshima na ushirikiano wa kweli,” alisema Mhe. Balozi Omar.
Aidha, Mhe. Balozi Omar alisema kuwa, dhamira ya Indonesia katika kukuza maendeleo endelevu na kupunguza umasikini imechangia kubadilisha kwa kiasi kikubwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini Tanzania kupitia misaada ya kifedha, ushauri wa kitaalamu, na programu za kujenga uwezo.
Aidha Mhe. Balozi Omary aliwaalika wawekezaji kutoka Indonesia kuja kuwekeza nchini katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii ikiwemo kilimo, uongezaji thamani wa mazao, madini, viwanda, nishati, miundombinu, afya, elimu na utalii.
Kwa upande wake, Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Mhe. Tri Yogo Jatmiko Avetisyan, alisema kuwa katika kuhakikisha kuwa nchi hizo zinadumisha ushirikiano zaidi ya Watanzania 170 wamepata manufaa kupitia programu hizo za kujenga uwezo katika sekta mbalimbali ikiwemo kilimo, mifugo, nishati, madini, uvuvi na fedha.
“Tutahakikisha tunaimarisha zaidi uhusiano huu kwa kuongeza kuwajengea uwezo wataalmu wa Tanzania ili maeneo yote tuliyokubaliana kushirikiana yanaleta tija na ustawi mpana wa uhusiano wa nchi hizi mbili,” alisema Mhe. Balozi Avetisyan.
Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban, Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Dkt. Blandina Kilama, Kamishna wa Idara ya Fedha za Nje Wizara ya Fedha, Bw. Rished Bade, Kamishna Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Bi. Tiba Kisonga na maafisa wengine waandamizi kutoka Wizara ya Fedha na ubalozi wa Indonesia nchini
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla ameiagiza Wakala wa barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Mkoa wa Arusha, Jeshi la Polisi pamoja na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kushughulikia kadhia ya foleni kwenye Jiji la Arusha kwa wakati ili kuondoa vikwazo katika shughuli za kila siku za kiuchumi na Kijamii ndani ya Jiji la Arusha.
Katika kutekeleza agizo hilo, leo Jumatano Januari 14, 2026, kimefanyika kikao kilichowahusisha Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa, TARURA, LATRA, TANROAD, Polisi na Idara ya Mipango Miji Jiji la Arusha, ambapo pamoja na mambo mengine wametangaza kufutwa kwa Vituo vya Mabasi katikati ya Jiji ambavyo vimekuwa vikitumika kushusha na kupakia abiria, wamiliki wa mabasi wakiagizwa kutumia Kituo Kikuu cha mabasi Arusha kwaajili ya abiria wao.
Kulingana na Mhandisi Julius Kaaya, Kaimu Meneja wa TARURA Mkoa wa Arusha akizungumza kwaniaba ya washiriki wa Kikao hicho, agizo hilo linaanza utekelezaji wake mara moja, wakitangaza kuchukua hatua kali za kisheria kwa kampuni ya mabasi itakayokaidi kutekeleza agizo hilo.
Kwa upande wake Afisa Mipango Miji Jiji la Arusha Bi. Doroth Absalom ameeleza kuwa kulingana na sheria, Kampuni za mabasi haziruhusiwi kutumia majengo ya makazi na biashara kama Vituo vyao vya mabasi, akisema ni sheria kwamba kila Basi kuanzia safari zake kwenye Kituo Kikuu cha mabasi Arusha, akionya pia kuhusu uoshaji holela wa mabasi pembezoni mwa barabara.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, akizungumza wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau Juu ya Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, akizungumza wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau Juu ya Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (Sekta ya Sayansi), Prof Daniel Mushi, akizungumza wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau Juu ya Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo (hayupo pichani),wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau Juu ya Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.


Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo (hayupo pichani),wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau Juu ya Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Wadau wakichangia mada mbalimbali wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau Juu ya Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau Juu ya Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau Juu ya Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau Juu ya Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau Juu ya Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau Juu ya Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau Juu ya Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau Juu ya Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau Juu ya Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.
Na.Alex Sonna-DODOMA
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imezitaka taasisi zote za elimu nchini kuongeza ubunifu na ufanisi katika ufundishaji na ujifunzaji kupitia matumizi bora, salama, na yenye uwajibikaji wa teknolojia za kidijitali.
Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Carolyne Nombo,wakati wa Warsha ya Kujenga Uelewa kwa Wadau Juu ya Mkakati na Miongozo ya Kitaifa kuhusu Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali kwenye Sekta ya Elimu iliyofanyika leo Januari 14,2026 jijini Dodoma.
Prof. Nombo amewataka wadau wa elimu kuzingatia mabadiliko ya kidijitali kama hitaji la lazima, huku akisisitiza kwamba ustawi wa baadaye wa Tanzania unategemea nguvu kazi yenye ujuzi wa kidijitali na ubunifu, kama inavyobainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
“Mkakati huu unalenga kuweka mfumo wa kitaifa wa kuratibu na kuongoza mageuzi ya kidijitali katika ngazi zote za elimu kuanzia shule, vyuo vya ualimu, taasisi za TVET, vyuo vikuu, hadi ujifunzaji wa mtandaoni,” amesema Prof. Nombo.
Aidha, Prof. Nombo amesisitiza umuhimu wa ufundishaji wa kidijitali na ujumuishaji wa TEHAMA, pamoja na uelewa wa Akili Unde (AI) na stadi za data katika mafunzo ya walimu. Ameeleza kuwa maendeleo endelevu ya kitaaluma kupitia majukwaa ya kidijitali ni muhimu ili kuwawezesha walimu kutumia teknolojia kwa ubunifu na uwajibikaji.
“Nafasi ya walimu ni nguzo kuu ya mageuzi kidijitali. Teknolojia peke yake haiwezi kuleta mabadiliko bila walimu wenye ujuzi na utayari wa kutumia teknolojia za kufundishia na kujifunzia,” amefafanua.
Prof. Nombo pia amesisitiza umuhimu wa Miongozo ya Kitaifa ya Elimu ya Kidijitali na Mwongozo wa Matumizi ya Akili Unde katika Elimu, ambayo inalenga kuhakikisha matumizi ya teknolojia hayaingilii maadili, ulinzi wa data, ujumuishi, na ubora wa kitaaluma. Vyuo vikuu na taasisi za utafiti wanahimizwa kuongeza ubunifu na utafiti unaozingatia AI na teknolojia nyingine zinazochipuka.
Aidha,ametoa wito kwa taasisi za udhibiti na uthibitishaji ubora kama TCU, NACTVET, COSTECH, TCRA na ICTC kushirikiana na wizara na kutoa elimu ili kuhakikisha mshikamano wa kisera, ulinganifu, na muingiliano wa mifumo sambamba na sera na miongozo ya kitaifa.
Prof. Nombo amewahimiza kutoa ushirikiano na washirika wa maendeleo na sekta binafsi, wakihimizwa kuunda suluhisho zinazolingana na muktadha wa Tanzania na kuunga mkono ukuaji wa stadi, ubunifu, na uendelevu wa elimu ya kidijitali.
“Usambazaji ni hatua ya kwanza tu. Utekelezaji unahitaji uongozi, uratibu, rasilimali na uwajibikaji. Naomba taasisi zote kuingiza Mkakati wa Kitaifa wa Elimu ya Kidijitali na Miongozo yake katika mipango yao, kuteua waratibu, kutenga rasilimali, na kushiriki kikamilifu katika ufuatiliaji, tathmini na kujifunza kwa pamoja.”amesema Prof. Nombo
Kwa upande wake,Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (Sekta ya Sayansi), Prof Daniel Mushi, amepongeza hatua ya Serikali kuandaa Mkakati na Miongozo ya Kitaifa ya Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali katika Elimu, akisema juhudi hizo zinaweka msingi madhubuti wa mageuzi ya elimu yanayoendana na kasi ya dunia ya sasa.
Prof Mushi amesema hatua hiyo inalenga kuboresha ubora wa ufundishaji na ujifunzaji, kukuza ubunifu, na kuwaandaa walimu na wanafunzi kukidhi mahitaji ya zama za kidijitali.
Warsha hiyo ya siku mbili, inayofanyika Januari 14–15, 2026, inawakutanisha wataalam na viongozi mbalimbali wakiwemo makatibu wakuu, wakuu wa vyuo vikuu, viongozi wa VETA, wakuu wa vyuo vya ualimu, taasisi za maendeleo pamoja na wadau wengine wa elimu kutoka sekta za umma na binafsi.
“Huu ni mwendelezo wa jitihada za Serikali kujenga mfumo mmoja na shirikishi wa matumizi ya teknolojia za kidijitali kwenye elimu. Ushiriki wenu unaonesha dhamira ya dhati ya kuijenga Tanzania yenye elimu bora, jumuishi na inayoshindana kikanda na kimataifa,” amesema Prof Mushi.


.jpeg)

.jpeg)


.jpeg)


.jpeg)

















