Na Oscar Assenga, TANGA



SERIKALI imesema kwamba ina mpango wa kuendelea kufanya uwekezaji katika Bandari ya Tanga kwa kuongeza sehemu ya kutoa huduma mara mbili kutoka mita 450 hadi kufikia mita 900 ili kuendelea kuongeza ufanisi wa kuhudumia shehena



Hayo yalibainishwa Septemba 1,2025 na Msajili wa Hazina Nehemiah Mchechu wakati alipofanya ziara katika Bandari ya Tanga kuona uwekezaji uliofanywa na Serikali wa Sh.Bilioni 429.1, huku akiridhishwa na maboresho yaliyofanyika ambayo yameiwezesha kufanya shughuli zao kwa ufanisi.

Alisema kwamba uwekezaji katika Bandari hiyo utaendelea kuwa chachu ya kuongeza matokeo ya wazi ya kiuchumi kutokana na kuchangia uwepo wa shughuli mbalimbali za kiuchumi na hivyo kuchangia maendeleo ya mkoa na Taifa kwa ujumla.

Aidha alisema kwamba katika sehemu ya kutolea huduma kuna mita 450 na kina mita 3 na kinaenda kuwa mita 13 ikiwemo lango la kuingilia limepanuliwa na kufikia upana mita 135 kwa kina cha mita 13 lakini bado kuna mipango inafanyika kuongeza ifike mita 900.

“Tunaiona Bandari hii ikichangamka tayari Serikali inakwenda kufanya uwekezaji mara mbili kutoka mita 450 mpaka mita 900 maana yake ni mita ni 1800 sasa unapokuwa unaangalia maeneo ya Bandari uwekezaji huo na ule uwekezaji wa Chongoleni kwa ajili ya mafuta ukiangalia gati inayotengenezwa kwa ajili ya Meli kubwa zinazokuja kusafirisha mafuta ghafi yanayotoka nchini Uganda huu ni uwekezaji mkubwa ”Alisema



Aliongeza kwamba maana tayari eneo la Tanga litakuwa ni kitovu cha biashara pamoja na eneo ambalo kila mtu kutoka mataifa mbalimbali atakuwa anaifahamu na kuwa na uwekezaji mkubwa na kuleta nafasi kubwa za kiuchumi sio kwa mkoa bali nchi nzima.

“Kimsingi mimi kama Msimamizi wa Mashirika na Mmiliki kwa niaba ya Serikali ninafarijika na huduma zinazotolewa na TPA na utulivu tunauona uimara wa huduma maana yake ni muunganiko wa vitu viwili uongozi inayofahamu kazi yake na watumishi wanaofanya kazi yao kwa ustawi wa juu”Alisema



Alisema kwamba wanazidi kuwa na matumaini makubwa sana kwa sababu Bandari asilimia kubwa ya mapato yake yanayokusanywa na TRA wanatoka Bandari na wanafikiria ni muhimu kuendelea kuitazama Bandari kwa jicho la Pekee.

“Lakini niwasihi wafanyakazi wa Bandari tuone ufahari tupo sehemu ambayo ni jicho na mboni ya Serikali katika uchumi wa nchi kwa hivyo lazima tuichukulie kama sehemu muhimu inayohitaji huduma zilizobora na tija kwa ajili ya maendeleo”Alisema



Hata hivyo alisema kwamba jambo jingine ni kuendelea kuhakikisha sekta binafsi na umma zinaungana lakini mali inabaki kuwa ni ya Bandari na zitabali kuwa mali ya nchi na wananchi kwa ujumla.

“Tunachokizungumza hapo ni na wanachokizungumza ni wawekezaji ambao watakuja kuziendesha na watapata mapato lakini baada ya muda kile kitu ni mali yetu na hakiondoki na maana yake tunakuwa na ushindani na ufanisi na huduma zitaendelea kuwa bora hivyo ni jambo la msingi na watanzania waendelea kujiunga na kujifunza kwa waliokuja kuwekeza”Alisema



Awali akizungumza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Plasduce Mbossa alisema uwekezaji wa viwanda huo umesaidia kuhudumia meli kwa urahisi na gharama nafuu kutokana na kuimarika miundombinu ya Bandari ya Tanga



“Sisi tumekusanya Bilioni 75 ambazo tunatumia kulipa wafanyakazi,vifaa na kufanya ukarabati tunatumia fedha hizo Tanga kuna ukuaji mkubwa wa viwanda na kichosabababisha ni Bandari sasa tunaweza kuhudumia meli kwa urahisi na bei nafuu ndio inapeleka uwekezaji wa viwanda”Alisema

Hata hivyo alisema ujenzi viwanda vilivyo vinasababisha ukuaji wake kuimarika kwa Bandari ikiwemo maboresho walioyafanya na ukuaji wa uchumi na mahitaji na maendeleo yanazidi kufanywa ikiwemo upanuzi zaidi na watajenga mita 900 zaidi.

“ Leo utaona kuna meli mbili zinahudumiwa na meli tatu nje zinasubiri hivyo tunahitaji kupanua miundombinu ili kuweza kuzihudumia meli zote kwa wakati na kuwasaidia wafanyabiashara na wakulima kulifikia soko kupitia Bandari ya Tanga”Alisema

Kwa upande wake Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha alimhakikishia Msajili huyo kuwa huduma katika Bandari ya tanga itazidi kuimarika kwa maana ya kwamba meli zitakapokuwa zinakuja watazihudumia sio kwa zaidi ya siku tatu meli inaondoka huku akitoa wito kwa watumiaji wa Bandari hiyo waendelee kuitumia

  


Kila usiku nilipozima taa na kujaribu kulala, nilihisi kama macho fulani yananitazama gizani. Mara nyingi ningejigeuza kitandani, nikafunika kichwa kwa shuka, lakini hisia ile haikuondoka. Nilihisi sauti za minong’ono zikiniita majina yangu, wakati mwingine miguu ikitembea sebuleni ilhali nilikuwa peke yangu nyumbani. Mwanzoni nilidhani ni mawazo yangu tu, lakini mambo yalizidi kuwa mabaya.

Kila saa sita usiku, nilihisi kivuli kizito kikisimama pembeni ya kitanda changu. Mara nyingine niliona kama ni mtu mrefu amevaa mavazi meusi, uso wake haukuwa na maumbile. Ningejaribu kupiga kelele, lakini sauti yangu haikutoka.

Nilijikuta nikipumua kwa shida, nikihisi kama kuna kitu kimenikalia kifuani. Asubuhi, nilipoamka, nilikuwa nimechoka mno kana kwamba sikulala kabisa.

Familia yangu haikunielewa. Wengine walidhani labda ninasumbuliwa na msongo wa mawazo au labda nimezidi kuamini hadithi za usiku. Lakini mimi nilijua hii haikuwa ndoto wala mawazo. Nyumbani nilianza kuhisi baridi kali isiyo ya kawaida, hata wakati wa mchana. Vitu vilianguka bila mtu kugusa, na mara nyingine taa ziliwaka na kuzimika zenyewe. Soma zaidi hapa 

 


Na Elizabeth Joseph, Monduli.

Wakristo wilayani Monduli wametakiwa kuishi kwa Upendo kama mafundisho ya Dini yanavyowataka ili kuepusha vitendo vya Ukatili hasa kwa watoto.

Kauli hiyo imetolewa Agosti 31 2025 na Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mh,Gloriana Kimath wakati akisalimia waumini waumimi katika Ibada ya Uwekaji Jiwe la Msingi la Jengo la Kanisa Anglikana (St.Peter's) Dayosisi ya Mount Kilimanjaro ambapo Ibada hiyo iliongozwa na Askofu wa Dayosisi ya Mount Kilimanjaro Dkt Stanley Hotay.

Alisema kuwa kumekuwa na ongezeko la vitendo mbalimbali vya Ukatili hasa kwa watoto jambo alisema kwa kiasi kikubwa linachangiwa na kukosekana kwa upendo katika jamii zinazowazunguka.

"Mafundisho ya Dini yanatufundisha juu ya upendo lakini kwasasa wengi wetu hatuuishi huo upendo tunaoelekezwa kwenye vitabu vya Dini,Mfano Wakina Mama tunaishi kwa kuwanyanyasa hawa Wasaidizi wetu wa kazi majumbani yaani hatuwaoneshi upendo wakati wao ndio wanatupikia,wanalea watoto wetu tukiwa na bize na kazi zetu na kufanya shughuli nyingine majumbani mwetu lakini tunawalipa mabaya badala ya kuwapenda.

"Jambo hili linawafanya na wao kuhamisha hasira  na chuki zao kwa watoto wetu kwa kuwafanyia vitendo vya kikatili,niwaombe sote tubadilike, tupendane ili tuweze kutokomeza vitendo hivi kwenye jamii zetu maana palipo na upendo hakutakuwa na chuki. "alifafanua Mh,Kimath.

Kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Rais na Viongozi wengine Mh,Kimathi aliwaomba waumini hao kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh,Samia Suluhu Hassan na Viongozi wengine ikiwa ni pamoja na kuliombea Taifa la Tanzania katika mchakato huo ili amani iendelee kutawala nchini.

Naye Askofu wa Dayosisi ya Mount Kilimanjaro Dkt Stanley Hotay katika mahubiri yake aliwaomba waumini hao kuhakikisha wanadumisha Amani ya Nchi na kwakuwa ndio kipaumbele kikubwa katika maisha ya kila mmoja.

"Usiombe kukosa Amani maana hata uwe na mali kiasi gani hilo Gari,Nyumba na pesa ulizonazo hazitakuwa na faida kwenye maisha yako kwakuwa utaishi maisha ambayo hutajua usalama wa maisha yako kwa saa zijazo utakuwa wapi,utatamani kwenda mjini ama mahali pengine lakini hutakuwa na uhakika wa kurudi salama hivyo ni muhimu kulinda  na kuombea sana Amani yetu "Alisisitiza Dkt Hotay.

Mgombea ubunge wa Jimbo la Same Magharibi kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Mathayo David maarufu kama Mwana wa Kaya, ameweka wazi kuwa uchaguzi wa Oktoba si wa majaribio, bali ni wa kuchagua kasi, utekelezaji na maendeleo.

Akizungumza katika uzinduzi wa kampeni uliojaa shamrashamra, zilizofanyika katika katika kata ya Hedaru,Dkt. Mathayo alitoa wito mzito kwa wananchi wa Same Magharibi kuhakikisha wanawachagua viongozi wa CCM – kuanzia kwa Rais Samia Suluhu Hassan, yeye mwenyewe kama mbunge, hadi kwa madiwani – akisema viongozi hao “wanatekeleza wanachoahidi.”

“Miaka mitano iliyopita tumefanya kazi. Sasa tunakuja kuhitaji nafasi ya kuendelea – kazi ya maendeleo ya kweli,” alisema kwa msisitizo.

Wananchi Wapaza Sauti: “Tunaiona kazi ya Mama Samia!”

Katika hali iliyojaza hamasa, wananchi wa Same Magharibi walitumia jukwaa hilo kuipongeza serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutekeleza Ilani ya CCM kwa kiwango cha juu asilimia 100, wakisema kazi imeonekana katika kila kijiji, kata na kata ndogo.

“Mama Samia ametupa maji, afya, shule, barabara, umeme… hatuna cha kulalamika. Sasa tunaomba aendelee pamoja na Dkt. Mathayo ambaye kazi yake tunaijua,” alisema mama mmoja kutoka Kata ya Bwambo huku akishangiliwa na umati.

Aidha, wananchi walishukuru Kamati Kuu ya CCM kwa uamuzi wake wa kurejesha jina la Dkt. Mathayo David kuwa mgombea wa CCM katika jimbo hilo, wakieleza kuwa ni kiongozi mchapakazi, mnyenyekevu na mwenye kuelewa vipaumbele vya wananchi wake.

“Tunawashukuru sana Kamati Kuu. Mmetusikiliza. Tumempata mtu wetu – Mwana wa Kaya. Tunaamini atatufikisha mbali zaidi,” alisema kijana mmoja aliyeshiriki mkutano huo kwa hisia kali.

Ahadi Kubwa: Afya Bila Malipo, Mochwari Bila Deni

Katika kile kinachoonekana kama ahadi yenye uzito wa kihistoria, Dkt. Mathayo alitangaza mpango wa huduma za afya kwa wote, akisema:

“Tunaposema afya bora kwa wote, tunamaanisha kweli. Hata motuary itakuwa bure – hakuna mzazi atakayeambiwa hawezi kumzika mpendwa wake kwa sababu ya deni.”

Kupitia mpango huu mpya, unaotarajiwa kuzinduliwa ndani ya siku 100 za kwanza za uongozi wa Rais Samia iwapo atachaguliwa tena, serikali inalenga:

Huduma za bima ya afya kwa wote

Matibabu bure kwa wazee, wajawazito, watoto na watu wenye ulemavu

Mochwari bure, kwa heshima ya wafu na familia zao

Kazi Iliyoonekana: Maji, Miundombinu, Elimu na Umeme

Katika tathmini ya mafanikio ya miaka mitano, Dkt. Mathayo alieleza hatua zilizopigwa:

✅ Zahanati na vituo vya afya vyenye vifaa na watumishi

✅ Visima na mtandao wa maji vijijini

✅ Madarasa, mabweni na nyumba za walimu

✅ Barabara na miundombinu bora ya kijamii

✅ Usambazaji wa umeme vijijini unaoendelea

Mpango wa awamu ijayo unalenga kukamilisha kilichobaki – kuhakikisha kila kijiji kinapata huduma zote za msingi.

“Kila kijiji, kila kata – tunaleta maendeleo,” alisema Dkt. Mathayo, huku akipigiwa makofi na umati wa wananchi waliokuwa wakiimba: “Kazi iendelee!”

Ilani 2020 Yatekelezwa – Sasa Ni Wakati wa Hatua Zaidi

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Same Abdilah Suleiman alieleza kuwa Ilani ya Uchaguzi ya 2020-2025 imetekelezwa kwa mafanikio, na sasa chama kiko tayari kusukuma mbele ajenda ya maendeleo.

“Leo tunamkabidhi Dkt. Mathayo zana za utekelezaji – kwa sababu kazi imeonekana,” alisisitiza.

Wito wa Mwisho: “Samia, Mathayo, Madiwani – CCM Tena!”

Akihitimisha mkutano huo, Dkt. Mathayo aliwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi Oktoba 29 mwaka huu na kufanya uamuzi wa maendeleo:

“Tunaomba tena mtuchague – Mama Samia, Mathayo na madiwani wa CCM – kwa sababu mnatujua. Tukiahidi, tunatekeleza.





  


Nakumbuka siku ambayo maisha yangu yalibadilika ghafla, na hadi leo majirani wangu bado wananiangalia kwa macho ya mshangao na hofu. Ilikuwa usiku wa manane, na mimi nikiwa nimevaa kanga ya kulalia, nilikuwa jikoni nikichemsha wali na supu ya kuku. Nilihisi kama mtu yuko pale nami lakini hakuna kiti kilichosogea, wala mlango haukufunguka.

Sauti ya kiume, tulivu lakini yenye mamlaka, ilinong’ona masikioni mwangu, “Hakikisha unaweka pilipili, kama nilivyopenda zamani.” Nilishikwa na bumbuwazi. Sikuwahi kuishi na mwanaume ambaye anapenda pilipili namna hiyo, lakini sauti hiyo ilihisi kama ya mtu niliyemfahamu. Niliendelea kupika, nikihisi joto la uwepo wa mtu nyuma yangu, ingawa nilipogeuka, hewa tu ndiyo iliyoigusa shingo yangu. Soma zaidi hapa 


*📌Vijiji vyote 763 sawa na asilimia 100 vimeshapata huduma ya umeme Tanga*


*📌Vitongoji 2,382 sawa na asilimia 52.6 vimeshapata huduma ya umeme*


*📌Shilingi bilioni 68.5 yawezesha utekelezaji miradi ya REA Tanga*


📍Korogwe - Tanga


Wakandarasi wote waliopewa zabuni ya kutekeleza miradi mbalimbali ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA, wametakiwa kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa ubora uliopangwa ili iweze kuwanufaisha wananchi. 


Rai hiyo imetolewa leo Agosti 31, 2025 wilayani Korogwe na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu,  wakati akizungumza na Wakandarasi wa miradi ya umeme wanaotekeleza miradi hiyo mkoani Tanga. 

"Katika utekelezaji wa miradi hii bado kuna changamoto ya uunganishaji mdogo wa wateja kwa sababu mbalimbali na kufanya miradi hii kutokumalizika kwa wakati, hakikisheni mnaongeza kasi, maarifa ya kuwahudumia wateja na ubunifu ili uunganishaji uweze kuleta tija," Amesisitiza Mhe. Balozi Kingu. 


Katika hatua nyingine, Balozi Kingu amesema mkoa wa Tanga vijiji vyote 763 vimeshapata huduma ya umeme kupitia miradi ya REA na vitongoji 2,382 kati ya vitongoji 4,531 navyo vimepata huduma ya umeme na kasi kubwa inaendelea ya kuwaungashia wateja katika maeneo yao. 

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amemtaka mkandarasi Ok electrical and Electronics Services Ltd  na Wakandarasi wengine kuhakikisha wanaongeza kasi ya kupeleka umeme kwa wateja ili wateja wengi wapate huduma hiyo.


"Sisi REA tutaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya umeme pamoja na kuwasimamia kwa karibu wakandarasi wote waliopewa zabuni ya kutekeleza miradi hii ili iweze kuwa na mchango mkubwa kwa jamii, " Amesema Mha. Saidy. 

Naye, Kaimu Mhandisi Miradi ya REA Mkoa wa Tanga, Mha. Kelvin Melchiad amesema, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetoa jumla ya kiasi cha shilingi bilioni 68.5 ili kuhakikisha miradi yote inatekelezwa na wananchi wanapatiwa huduma ya umeme ili kuwapatia maendeleo ya kiuchumi na kijamii. 

Wakandarasi waliohudhuria kikao hicho ni mkandarasi Ok electrical and Electronics Services Ltd, Tontan Project Technology Co. Ltd na Transpower Ltd and Whitecity International Contractor Ltd.

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza na waandishi wa habari kuhusu wahitimu 50  waliofanya vizuri katika masomo ya Sayansi kwenye matokeo ya Kidato cha Sita mwaka 2025 na kuchaguliwa kupata ufadhili wa Samia Scholarship Extended, kusomea programu za Akili Unde, Sayansi ya Data na Sayansi zingine Shirikishi katika vyuo vikuu mahiri duniani.

Na.Mwandishi Wetu.

WAHITIMU  50 waliofanya vizuri katika masomo ya Sayansi kwenye matokeo ya Kidato cha Sita mwaka 2025 wamechaguliwa kupata ufadhili wa Samia Scholarship Extended, kusomea programu za Akili Unde, Sayansi ya Data na Sayansi zingine Shirikishi katika vyuo vikuu mahiri duniani.

Taarifa hiyo imetolewa Agosti 31, 2025 jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, ambaye amesema kuwa wahitimu waliochaguliwa walitokana na ufaulu wao bora katika masomo ya PCM, PMC na PGM.

Prof. Nombo amesema kuwa wanafunzi hao watawekwa katika Kambi Maalumu ya Maarifa (Boot camp), ambako watapatiwa mafunzo ya kujenga misingi katika matumizi ya kompyuta, programu na uchambuzi wa mifumo, pamoja na kusaidiwa kufanya maombi ya udahili katika vyuo vya nje kwa kushirikiana.

Ameeleza kuwa mafunzo hayo yatatolewa na wataalamu wabobezi kutoka ndani na nje ya nchi, wakiwemo kutoka sekta binafsi na diaspora, kwa kipindi cha miezi 10.

Aidha watapata fursa ya kufanya mitihani itakayowawezesha kupata vyeti vya kitaaluma mfano IBM, Certificate- Machine Lerning for for Data Science Projects, Certified Certificate in Cyber Security Standards na AWS Certified Cloud Practitioner vinavyotambulika kimataifa.

Ufadhili huu ni utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014, toleo la 2023, inayolenga kutoa elimu inayozingatia ujuzi kulingana na soko la ajira na stadi za karne ya 21 ili kuchangia katika maendeleo ya Taifa na kimataifa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza na waandishi wa habari kuhusu wahitimu 50  waliofanya vizuri katika masomo ya Sayansi kwenye matokeo ya Kidato cha Sita mwaka 2025 na kuchaguliwa kupata ufadhili wa Samia Scholarship Extended, kusomea programu za Akili Unde, Sayansi ya Data na Sayansi zingine Shirikishi katika vyuo vikuu mahiri duniani.

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo,akizungumza na waandishi wa habari kuhusu wahitimu 50  waliofanya vizuri katika masomo ya Sayansi kwenye matokeo ya Kidato cha Sita mwaka 2025 na kuchaguliwa kupata ufadhili wa Samia Scholarship Extended, kusomea programu za Akili Unde, Sayansi ya Data na Sayansi zingine Shirikishi katika vyuo vikuu mahiri duniani.

Wakisikiliza hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo (hayupo pichani) wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu wahitimu 50  waliofanya vizuri katika masomo ya Sayansi kwenye matokeo ya Kidato cha Sita mwaka 2025 na kuchaguliwa kupata ufadhili wa Samia Scholarship Extended, kusomea programu za Akili Unde, Sayansi ya Data na Sayansi zingine Shirikishi katika vyuo vikuu mahiri duniani.

 


Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuimarisha miundombinu ya barabara na kujenga soko pamoja na stendi mpya katika Wilaya ya Chemba, mkoa wa Dodoma, ili kuchochea shughuli za kiuchumi na kurahisisha maisha ya wananchi.

Akihutubia, Agosti 31, 2025, kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika jimboni Chemba, Dkt. Samia amesema changamoto kubwa iliyojitokeza kwa wananchi wa eneo hilo ni ubovu wa miundombinu ya barabara, hasa barabara ya Chemba–Soya yenye urefu wa kilomita 32.

“Barabara hii ni ya uchumi, ndiyo barabara ambayo kuna minada hufanyika kila Jumapili. Minada hii inaingiza kiasi kikubwa cha fedha ndani ya Halmashauri, lakini pia mifukoni mwa wafugaji na wafanyabiashara wadogo. Ni barabara muhimu na tunawaahidi kwamba tutaichukua na kuifanyia kazi. Inaweza isiishe mwaka huu wa fedha, lakini katika miaka ijayo tutaiweka kwa kiwango cha lami,” amesema Dkt. Samia.

Ameongeza kuwa mbali na Chemba–Soya, barabara nyingine tatu za ndani ya Wilaya ya Chemba zitaangaliwa uwezekano wa kukarabatiwa kupitia TARURA ili ziweze kupitika mwaka mzima, iwe ni kipindi cha mvua au kiangazi.

 


Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuanzisha mashamba makubwa ya kilimo kwa ajili ya vijana wa Chamwino, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa serikali wa kuwawezesha vijana kujitegemea kiuchumi.

Akizungumza Agosti 31, 2025, kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Chamwino, mkoani Dodoma, Dkt. Samia amesema mashamba hayo yataletwa kwa mfano wa yale yaliyopo eneo la Chinangali ambayo yamekuwa chachu ya maendeleo kwa vijana.

“Kwa upande wa kilimo ndugu zangu wa Chamwino tunakwenda kuanzisha mashamba makubwa hasa yale ya vijana, kama yale ambayo tumefanya pale Chinangali. Tutaanzisha mashamba hayo kwenye maeneo kadhaa ndani ya Jimbo letu la Chamwino ili vijana wetu wapate pahali pazuri pa kueleweka, waweze kufanya kazi zao na waweze kujitegemea,” amesema Dkt. Samia.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi wa Chamwino kuendeleza mshikamano na kufanya kampeni za nyumba kwa nyumba ili kuhakikisha CCM inapata ushindi katika uchaguzi ujao.




SAMIA AAHIDI VITUO VYA AFYA NA ZAHANATI MPYA CHAMWINO

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuimarisha zaidi huduma za kijamii katika Jimbo la Chamwino ikiwa ni pamoja na afya, maji na barabara.

Akizungumza leo, Agosti 31, 2025, katika mkutano wa kampeni uliofanyika Chamwino, mkoani Dodoma, Dkt. Samia amesema serikali ya CCM ina dhamira ya kuhakikisha wananchi wa jimbo hilo, ambalo pia ndilo lina Ikulu ya Rais, hawakabiliwi na changamoto za huduma za msingi.

Kuhusu upatikanaji wa maji, Dkt. Samia amesema: “Ninajua tuna shida ya maji, mgombea ubunge hapa amesema mradi mkubwa upo, ninataka niwahakikishie tutahakikisha Chamwino yote inapata maji kwa karibu zaidi.”

Aidha, ameahidi kuendeleza ujenzi wa miundombinu ya barabara, akisema serikali itajenga kilomita 10 za barabara za kiwango cha lami na kuimarisha barabara za changarawe katika maeneo mbalimbali ya jimbo hilo.