Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa licha ya mvua zinazoendelea kunyesha nchini, Bwala la Umeme la Julius Nyerere (JNHPP) lipo salama kutokana na kujengwa kisayansi na hivyo kuendelea kuzalisha umeme kupitia mtambo namba tisa huku mitambo mingine miwili ikiwa ukingoni kukamilika.

Dkt. Biteko amesema hayo tarehe 18 Aprili 2024  jijini Dodoma  katika  mahojiano Mbashara kupitia kipindi cha  Jambo Tanzania cha TBC kuhusu  Maonesho ya Wiki ya Nishati 2024 yanayoendelea katika Viwanja vya Bunge.

“ Bwawa letu lipo salama kwani limejengwa kisayansi, ujazo wake wa maji ni mita za ujazo 183 na kwa takwimu za leo  ni mita za ujazo 183.4, huko nyuma maji yalikuwa yakiingia mengi sana kwa kiasi cha mita za ujazo 8400 kwa sekunde hivyo yalipaswa kupunguzwa ili kuendana na ujazo wa bwawa.” Amesema Dkt. Biteko

Amesema  kuwa,  bila ya  kuwepo kwa Bwawa hilo athari za mvua zingeanza kuonekana tangu mwezi Oktoba mwaka jana lakini hali hiyo haikutokea mapema kwa sababu maji yalikuwa yakiijazwa katika bwawa kwa ajili ya kuzalisha umeme.

Ameongeza kuwa, Wizara ya Nishati na TANESCO ilishabaini uongezekaji wa maji katika mto Rufiji kuanzia mwezi Februari, mwaka huu na tahadhari ilianza kutolewa kuhusu  kasi hiyo ya maji ili kuanza kuchukua hatua  stahiki.

Dkt. Biteko ameeleza kusikitishwa kwake na athari zilizotokea  kutokana na mafuriko ambayo yamesababisha athari katika maisha ya watu na mali zao na kueleza kuwa  Serikali inafanya kila jitihada kurejesha hali ya kawaida  kwa wananchi waliokumbwa na maafa hayo.

Kuhusu utekelezaji wa ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia nchini, Dkt. Biteko amesema kuwa, watu wengi bado wanatumia nishati isiyo safi ya kupikia kama vile mkaa na kuni na wananchi wachache wanatumia gesi na nishati nyingine kama vile umeme.

Ameeleza kuwa, lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa ndani ya miaka 10 asilimia  80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia na kwamba Serikali imepitisha Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia ikiwa ni moja ya njia za utekelezaji wa ajenda hiyo ambayo inanadiwa na Kinara wake, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ameongeza kuwa, katika kutekeleza mpango huo wa Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais, imeshatoa waraka wa kutotumia kuni na mkaa kwa taasisi  zinazolisha watu kuanzia 100 na zaidi kama vile Shule na Magereza.

Kuhusu upatikanaji wa umeme wa uhakika Dkt. Biteko amesema kuwa kwa sasa uzalishaji umezidi mahitaji hivyo kinachofanyika sasa ni kuboresha miundombinu ya umeme ikiwemo ya kusafirisha umeme kwani baadhi ya sehemu laini za umeme ni ndefu sana hivyo vitajengwa vituo vya kupoza umeme takriban 83 nchini ili kuondoa athari za watu wengi kutopata umeme pale laini inapopata hitilafu.

Kuhusu Bei ya Gesi amekiri kuwa  bei ni kubwa  na kueleza kuwa, Serikali inaangalia kwa karibu sana suala hilo ili kuweza kupunguza gharama na hii haiishii kwenye gesi pekee bali kwenye majiko banifu na katika mwaka huu wa fedha Serikali itaanza kutengeneza majiko ya bayogesi kwenye nyumba za wananchi wanaofuga mifugo ili watumie  nishati hiyo kwa ajili ya kupikia.

Na John I. Bera - Arusha


Timu ya Wizara ya Maliasili na Utalii ya Mpira wa Miguu, leo  Aprili 18, 2024 imefuzu hatua ya makundi kwenye Mashindano ya Mei Mosi yanayofanyika Jijini Arusha.


Akizungumza mara baada ya kufuzu kwa kuifunga Timu ya Chuo cha Ufundi cha Arusha  (ATC) kwa goli mbili kwa nunge, Kapteni wa Timu hiyo, Bw. Arnold Elias amesema ushindi huo umetokana na juhudi mbalimbali za Wachezaji, Viongozi pamoja na Waalimu ambao wamekuwa wakipambana kuhakikisha kuwa Wizara inapata ushindi


Ameongeza kuwa, ushindi huo utaleta chachu na ari zaidi kwani kwa kufanya hivyo, kuitangaza Wizara pamoja na majukumu yake ikiwemo kuutangaza utalii wa ndani.

"Tunaushukuru Uongozi wa Wizara ya Maliasili kwa ujumla, umetupa hamasa kubwa tunawahakikishia viongozi kuwa tutapambana ili kufikia malengo na kufika fainali kwani tunaposhinda tunatangaza utalii" Amesema Elias


Kwa upande wa Kocha wa Timu hiyo, Bw. Abdallah Juma amewapongeza wachezaji kwa jitihada zao za kuhakikisha wanaipambania Wizara huku akisisitiza ya kuwa wao kama Timu watahakikisha wanailetea Wizara Ushindi


" Nawapongeza Wachezaji kwa ujumla, wamepambana sana kuhakikisha wanailetea Wizara ushindi na tumeweza kufuzu hatua inayofuata" Amesema Juma


Naye mfungaji bora kwa upande wa Wizara, Bw. Newton Mlai amesema ataendelea kujituma kwa ari kubwa ili kuhakikisha wanafuzu kwenye hatua inayofuata ili kutwaa ushindi.



 Aidha, Bw. Mlai ameshukuru wachezaji wenzake wote kwa kujituma na kupambana pia ameupongeza uongozi Mzima wa Wizara kwa uongozi mahiri unaosababisha matokeo ya ushindi.


Katika Kundi Wizara ya Maliasili imefuzu pamoja na Timu kutoka Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) huku Timu zingine za TPDC pamoja na Chuo cha Ufundi cha Arusha (ATC) zikishindwa Kufuzu kwa hatua inayofuata.


Sanjari na Kufuzu huko, Michezo mbalimbali imechezwa leo ikiwemo Mchezo wa Kamba kwa upande wa Wanaume na Wanawake ambapo Wizara imeibuka Mshindi kwa point 2 kwa sifuri dhidi ya RUWASA kwa upande wa Wanaume na Point 2 kwa Sifuri dhidi ya Taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO)




Na Mapuli Kitina Misalaba
Wakala wa Barabara Tanzania TANROADS Mkoa wa Shinyanga  umewakutanisha wadau mbalimbali wa usafiri wa anga kutoka taasisi za serikali na binafsi kwa lengo la kujadili maendeleo na fursa kwa wananchi katika uwanja wa ndege uliopo Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga.

Akitoa  taarifa leo Jumatano Aprili 17,2024 Mhandisi wa Mradi wa uwanja wa Ndege Shinyanga kutoka TANROADS, Binemungu Donatus amesema kwa kuzingatia shughuli zote ambazo zimefanyika katika ujenzi, mpaka sasa mradi huo umefikia asilimia 12.07.

Amesema ujenzi wa njia ya kuruka na kutua ndege imefikia asilimia 40.3, barabara ya kiungo imefikia asilimia 40, eneo la maegesho limekamilika kwa asilimia 40 huku ofisi ya mhandisi imekamilika kwa asilimia 100.

Amesema zaidi ya watanzania 100 wakiwemo wakazi wa Mkoa wa Shinyanga wameajiriwa katika mradi huo.

“Mradi huu umetoa jumla ya ajira 112 ambapo ajira 96 sawa na asilimia 86 zimetolewa kwa watanzania, changamoto kubwa inayokwamisha utekelezaji wa mradi huu ni mvua nyingi zinazoendelea kunyesha kwa sababu Mvua ikinyesha tunasubiria kuanzia siku tatu ardhi ikauke kwanza ndiyo tunaendelea ikiwa inashenye kila siku inakwamisha sana lakini pia tulipata changamoto ya ucheleweshwaji wa uhamishaji huduma za maji pamoja na miundombinu ya umeme kutoka eneo la mradi”, amesema Mhandisi Donatus.

“Mradi huu ukikamilika utarahisisha usafiri kwa wakazi wa Mkoa wa Shinyanga, Simiyu na Mikoa ya jirani lakini pia utarahishaji shughuli za kibiashara hasa uchimbaji madini, ufugaji na kilimo pia utawezesha shughuli mbalimbali za kijamii lakini pia mradi huu utasaidia sana kukuza uchumi wa Mkoa wa Shinyanga na Simiyu, utasaidia shughuli za utafiti wa kilimo pamoja na kukuza utalii katika Mkoa wa Shinyanga, Mikoa jira na Taifa”,amesema Mhandisi Donatus

Kaimu Meneja TANROADS Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Samwel Joel amesema uwanja wa ndege Shinyanga kwa hatua za awali utaanza kutumika kuanzia Mwezi Agosti,2024 na kwamba mkandarasi anaratajiwa kukamilisha Mwezi Oktoba Mwaka huu 2024 ambapo gharama ya mradi ni Bilioni 44.8.

Mhandisi Joel ameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha katika mradi huo ambapo ametumia nafasi hiyo kuwaomba wananchi kuchangamkia fursa zilizopo.

“Ujenzi unaenda vizuri sana kwa kasi jengo letu linaendelea vizuri na tunatarajia uwanja wetu wa Ndege utaanza kutumika kwa hatua za awali kuanzia Mwezi wa nane mwanzoni lakini ujenzi utakuwa unaendelea kufikia Mwezi wa kumi tunatarajia mkandarasi awe ameshakamilisha shughuli zote za uwanja wa Ndege Shinyanga”,amesema.

“Niendelee kuishukuru serikali inayoongozwa na Mama yetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jinsi anavyoendelea kuleta fedha na kufungua fursa katika Mkoa wa Shinyanga na sisi tutahakikisha hii miundombinu inajengwa kama inavyokusudiwa na ile thamani ya fedha inaonekane ili uchumi wa Shinyanga na taifa kwa ujumla uendelee kuimarika, niendelea kutoa rai kwa wananchi kwamba huu mradi una fursa nyingi sana ambazo zipo kipindi cha ujenzi lakini pia hata baada ya kukamilika kwa ujenzi niwaomba hasa wakazi wa Shinyanga wajitokeze kupokea hizo fursa”,amesema Mhandisi Joel.

Wadau mbalimbali kutoka kwenye taasisi za serikali na taasisi binafsi wamepongeza kwa hatua iliyofikiwa katika ukarabati na uboreshaji wa uwanja wa Ndege wa Shinyanga ambapo wameahidi kuendelea kuunga mkono juhudi hilo kwa la kutoa fursa kwa wananchi.

Mradi wa Ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Shinyanga unaojengwa na Mkandarasi China Hennan International Corperation Group Co. Ltd (CHICO) na unaosimamiwa na Wakandarasi kutoka Kampuni ya SMEC International ya nchini Australia umeanza Aprili 4,2023 na unatarajia kukamilika ifikapo Oktoba 3,2024 (ndani miezi 18) ukijengwa kwa fedha za serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mkopo kutoka Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (EIB).
Viongozi na wadau mbalimbali kutoka kwenye taasisi za serikali na binafsi wakisikiliza maelezo ya hatua za mradi wa ukarabati na uboreshaji wa uwanja wa Ndege wa Shinyanga, leo Aprili 17,2024.
Viongozi na wadau mbalimbali kutoka kwenye taasisi za serikali na binafsi wakisikiliza maelezo ya hatua za mradi wa ukarabati na uboreshaji wa uwanja wa Ndege wa Shinyanga, leo Aprili 17,2024.
Viongozi na wadau mbalimbali wakitembelea Mradi wa Ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Shinyanga
Viongozi na wadau mbalimbali kutoka taasisi za serikali na taasisi binafsi wakiendelea kutembelea mradi Mradi wa Ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Shinyanga
Viongozi na wadau mbalimbali kutoka taasisi za serikali na taasisi binafsi wakiendelea kutembelea mradi Mradi wa Ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Shinyanga

Viongozi na wadau mbalimbali kutoka taasisi za serikali na taasisi binafsi wakiendelea kutembelea mradi Mradi wa Ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Shinyanga
Viongozi na wadau mbalimbali kutoka taasisi za serikali na taasisi binafsi wakiendelea kutembelea mradi Mradi wa Ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Shinyanga

Mhandisi wa mradi wa uwanja wa Ndenge Shinyanga, kutoka TANROADS , Binemungu Donatus akieleza hatua mbalimbali za mradi wa ukarabati na uboreshaji wa uwanja wa Ndege wa Shinyanga.
Mhandisi wa mradi wa uwanja wa Ndenge Shinyanga, kutoka TANROADS , Binemungu Donatus akieleza hatua mbalimbali za mradi wa ukarabati na uboreshaji wa uwanja wa Ndege wa Shinyanga.
Kaimu meneja TANROADS Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Samwel Joel Mwambugu akizungumza kwenye kikao cha pamoja na wadau mbalimbali wa usafiri wa anga
Viongozi na wadau mbalimbali wa uwanja wa Ndege wa Shinyanga, kutoka kwenye taasisi za serikali na binafsi wakiwa katika kikao cha pamoja na TANROADS Mkoa wa Shinyanga 
Viongozi na wadau mbalimbali wa uwanja wa Ndege wa Shinyanga, kutoka kwenye taasisi za serikali na binafsi wakiwa katika kikao cha pamoja na TANROADS Mkoa wa Shinyanga 
Viongozi na wadau mbalimbali wa uwanja wa Ndege wa Shinyanga, kutoka kwenye taasisi za serikali na binafsi wakiwa katika kikao cha pamoja na TANROADS Mkoa wa Shinyanga 
Viongozi na wadau mbalimbali wa uwanja wa Ndege wa Shinyanga, kutoka kwenye taasisi za serikali na binafsi wakiwa katika kikao cha pamoja na TANROADS Mkoa wa Shinyanga 
Viongozi na wadau mbalimbali wa uwanja wa Ndege wa Shinyanga, kutoka kwenye taasisi za serikali na binafsi wakiwa katika kikao cha pamoja na TANROADS Mkoa wa Shinyanga 
Meneja wa Benki ya NBC tawi la Shinyanga Bi. Joyce Chagonja akitoa maoni yake kuhusu maboresho na fursa mbalimbali katika uwanja wa Ndege wa Shinyanga kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga
Afisa mahusiano kutoka NMB Benki tawi la Shinyanga Firbert Uyalo akitoa maoni  kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga mkoa wa Shinyanga
Afisa matekelezo mkuu kutoka NSSF Mkoa wa Shinyanga Bi. Hawa Godigodi akitoa maoni yake kuhusu maboresho na fursa katika uwanja wa Ndege wa Shinyanga akizungumza kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga mkoa wa Shinyanga
Meneja TRA Mkoa wa Shinyanga Bwana Faustine Mdessa akitoa maoni yake kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga mkoa wa Shinyanga

Beni Lucas Lihawa kutoka Karena Hotel akitoa maoni yake kuhusu maboresho na fursa katika uwanja wa Ndege wa Shinyanga kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga mkoa wa Shinyanga
Meneja mahusiano na biashara wateja wakati na wakubwa NBC Benki tawi la Shinyanga Carcos Kapinga akitoa maoni yake kuhusu maboresho na fursa kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga mkoa wa Shinyanga
Mhandisi Sai Kapera kutoka KASHWASA akitoa maoni yake kuhusu maboresho na fursa katika uwanja wa Ndege wa Shinyanga, kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga mkoa wa Shinyanga
Afisa mkuu uendeshaji NSSF Mkoa wa Shinyanga Ahmed Ally Salum akitoa maoni yake kuhusu maboresho na fursa katika uwanja wa Ndege wa Shinyanga kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga mkoa wa Shinyanga
Meneja wa uwanja wa Ndege wa Shinyanga Mhandisi Lugano Mwinuka akitolea ufafanuzi maoni na maswali mbalimbali yaliyoulizwa na wadau kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga mkoa wa Shinyanga
Kikao kikiendelea.
Mhandisi mkuu huduma za usafiri wa Anga Tanzania, Mpeli Ngonywike akizungumza kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga mkoa wa Shinyanga
Meneja mamlaka ya hali ya hewa kanda ya ziwa, Augustino Nduganda akizungumza kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga mkoa wa Shinyanga
Mhandisi mradi kutoka mamlaka ya viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) mhandisi Simon Mathias akizungumza kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga mkoa wa Shinyanga
Nasser Elgohary kutoka kampuni ya SMEC International Ltd akizungumza kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga mkoa wa Shinyanga
Nasser Elgohary kutoka kampuni ya SMEC International Ltd akizungumza kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga mkoa wa Shinyanga
Meneja mradi kutoka kampuni ya China Henan International Cooperation Group Ltd (CHICO), Shi Yinlei akizungumza kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga mkoa wa Shinyanga
Meneja mradi kutoka kampuni ya China Henan International Cooperation Group Ltd (CHICO), Shi Yinlei akizungumza kwenye kikao cha wadau wa usafiri wa anga mkoa wa Shinyanga
Shughuli mbalimbali zikiendelea katika ukabarati na uboreshaji uwanja wa Ndege wa Shinyanga.
Shughuli mbalimbali zikiendelea katika ukabarati na uboreshaji uwanja wa Ndege wa Shinyanga.
Shughuli mbalimbali zikiendelea katika ukabarati na uboreshaji uwanja wa Ndege wa Shinyanga.