Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Kenan Laban Kihongosi kenani kihongosi amekutana na viongozi wa Dini na viongozi wa mila wa mkoa huo kwa lengo kufahamiana na kupata baraka, dua na maombi kutoka kwa viongozi hao,  ili anapoianza kazi yake iwe na ulinzi wa Mungu, kikao kilichofanyika  kwenye ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa mkoa,  mapema leo Julai 01, 2025.

Amebainisha kuwa, anaamini Mhe.Rais kumleta Arusha si kwa uwezo wake bali ni mpango wa Mungu, na kuwaomba viongozi hao, licha ya kumpa ushirikiano katika utendaji wake kazi, amewasisitiza kuombea amani ya nchi, kumuombea, kumlea, kumfundisha, kumshauri na kumuelekeza pale atakapopotoka ili aweze kuitenda kazi vizuri na kuendeleza mkoa wao wa Arusha.

"Binafsi ninamshukuru Mungu kwa kunipa kibali cha kuja kuwatumikia tena, lakini  katika utumishi wa Umma kuna mambo ambayo yanahitaji msaada wa Mungu, hivyo ninaamini ushauri kutoka kwenu kutokana na umri wangu mdogo, niwaombe viongozi wangu  msiache kuniombea, ninaombe mnilee mimi ni kajana wenu". Ameweka wazi Mhe. Kihongosi.

Aidha, amewaomba kuuombea amani ya mkoa na Taifa kwa ujumla na kuongeza kuwa, waendeleze ushirikiano wao kama walivyoshirikiana na viongozi waliotangulia kwa kuwa mkoa ni ule ule,  kilichobadilika ni uongozi tu lakini malengo ya kuujenga mkoa wetu yako pale pale.

Hata hivyo amewasisitiza kendelea  kuhubiri amani ya nchi yao, kwa kuangalia manufaa ya amani na utulivu, na kuepuka  kujenga chuki na uadui kwa misingi ya dini na vyama vyetu kwa kuweke mbele utaifa hususani katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 

"Viongozi wa dini mnalojukumu la kuiombea Tanzania na viongozi wa mila wanayo kazi ya kuhubiri maadili na amani ya nchi yetu hivyo viongozi wangu ninaomba tushirikiane kuilinda amani, sisi ni watumishi wa Umma, tumekuja kufanya kazi tu, lakini iko siku tutaondoka, hivyo tusikubali kuharibu nyumbani zaidi tuilinde ardhi yetu" Amesema

Tutambue kuwa, Mheshimiwa Rais anayo nia njema kwa nchi yake kwa kuangali mifano ya miradi mikubwa inayotekelezwa nchini katika seka zote hivyo saidieni kuilinda nchi yetu na kumsaidie Mhe Rais.












Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Gas kwa kushirikiana na Wakala wa Nishati Safi Tanzania (REA) wamezindua rasmi mradi mkubwa ambao utawafikia na kuwawezesha wafanyakazi wote wa Magereza kuacha matumizi ya mkaa na kuni na kuhamia matumizi ya gesi.


Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kuonesha uwezo wake wa kiteknolojia na uaminifu wa huduma zake katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam.

Kupitia kaulimbiu yao ya "TEHAMA SALAMA, TAIFA SALAMA", TTCL linajitambulisha kama mhimili wa maendeleo ya kidijitali nchini, likiwa na huduma mbalimbali bunifu zinazowawezesha wateja wa sekta zote kupata mawasiliano ya uhakika, salama na ya gharama nafuu.

Meneja wa Banda la TTCL, Bi. Janeth Maeda, amesema TTCL linashiriki maonesho hayo si kwa lengo la kibiashara pekee, bali pia kuelimisha jamii kuhusu nafasi muhimu ya Shirika hilo katika kusimamia miundombinu ya mawasiliano ya Taifa.



“Tuna dhamana ya kitaifa ya kusimamia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB) na Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi Data Kimtandao (NIDC). Huduma hizi ni msingi wa usalama wa taarifa na miundombinu ya TEHAMA nchini,” alisema Maeda.




Bi. Maeda alifafanua kuwa shirika hilo linatoa huduma kwa taasisi nyeti kama wizara, hospitali, mashule, taasisi za fedha, mashirika ya umma na sekta binafsi, kwa kutumia teknolojia ya fiber optic yenye kasi, uthabiti na usalama wa hali ya juu.

“Mashirika yanayotumia huduma za TTCL yameshuhudia kupungua kwa gharama za uendeshaji, ufanisi mkubwa katika utoaji wa huduma, na uimarishaji wa usalama wa taarifa,” aliongeza.

Katika msimu huu wa Sabasaba, TTCL linatoa ofasikabambe kwa wateja wake, ikiwa ni pamoja na punguzo maalum kwa vifaa vya mawasiliano kama vile routers, USB modems, na MiFi devices—ikiwa ni mkakati wa kusaidia wananchi kumiliki vifaa bora kwa urahisi zaidi.

Aidha, Bi. Maeda ametoa wito kwa washiriki wa maonesho, taasisi za ndani na nje ya nchi pamoja na wananchi kwa ujumla, kutembelea banda la TTCL namba 26 ili kujionea huduma za kisasa, kupata ushauri wa kitaalamu kuhusu TEHAMA, na kujifunza mbinu za kuongeza ufanisi wa kazi kwa njia za kidijitali.

“TTCL ni zaidi ya mtoa huduma; sisi ni sehemu ya maendeleo ya Taifa,” alisisitiza.


Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Arch. Elius Mwakalinga, ameibuka rasmi kwenye kinyang’anyiro cha kuwania ubunge wa Jimbo la Kyela kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), baada ya kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea leo Julai 1, 2025, katika ofisi za chama hicho wilayani humo.







Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) amewavisha cheo manaibu kamishna wawili na kushuhudia uvishwaji vyeo kwa makamishna wasaidizi waandamizi watano waliovishwa vyeo na mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi NCAA Jenerali Venance Mabeyo (Mstaafu)

Waliovishwa Cheo na Mhe. Waziri ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Joas John Makwati aliyepandishwa cheo kuwa Naibu Kamishna wa Uhifadhi anayesimamia Uhifadhi, utalii na Maendeleo ya Jamii na Naibu Kamishna wa Uhifadhi Aidan Paul Makalla anayesimamia Huduma za Shirika NCAA.

Kwa upande wa makamishna waliovishwa vyeo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi NCAA Jenerali Venance Mabeyo (mstaafu) ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia idara ya Mipango na uwekezaji, Gasper Stanley Lyimo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Paul Geofrey Shaidi anayesimamia Kitengo cha huduma za Sheria, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Charles Marwa Wangwe anayesimamia Idara ya Uhasibu na fedha. 

Wengine ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Godwin Felician Kashaga anayesimamia Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, na Afisa Uhifadhi Mkuu Daraja la kwanza Mariam Kobelo anayesimamia idara ya Huduma za Utalii na masoko aliyepandishwa cheo kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi.

Baada ya kuwavishwa vyeo hivyo waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) amewaelekeza maafisa hao kufanya kazi kwa bidiii na weledi mkubwa katika kutekeleza majukumu yao kwa kuwa cheo ni dhamana na kinakuja na majukumu.

“Nimatumaini yangu kuwa viongozi wote mliovaa vyeo leo mtakuwa chachu ya kufanya kazi kwa kujituma na kuonesha mfano wa kuigwa kwa Maafisa na Askari mnaowaongoza, juhudi zenu ndiyo zitakazochangia kulinda na kuhifadhi eneo la Ngorongoro na kuendelea kuwa kivutio kwa wageni wanaotembelea” ameongeza Balozi Chana.

Kamishna wa Uhifadhi NCAA Abdul-Razak Badru ameeleza kuwa kwa sasa watumishi wote wa NCAA wameshapatiwa mafunzo ya kijeshi kutoka mfumo wa awali wa kiraia na kuwa mamlaka hiyo itahakikisha inatumia rasilimali ya watumishi waliopo kuongeza nguvu ya kuhifadhi, kulinda, kuendeleza jamii na kuboresha miundombinu ya utalii.

Mwenyekiti wa bodi ya NCAA Jenerali, Venance Mabeyo (mstaafu) ameeleza kuwa mafanikio ya Ngorongoro yanategemea uadilifu na uwezo wa viongozi wake na kuwaasa viongozi waliovishwa vyeo kubeba matumaini mapya katika utekelezaji wa majukumu ya uhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii.

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia Mkutano wa Nne wa Kimataifa kuhusu Ufadhili wa Maendeleo (FfD4) unaofanyika Jijini Sevilla nchini Hispania tarehe 30 Juni 2025.



MAKAMU Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa wito wa kufanyika maboresho ya mfumo wa fedha na ufadhili wa maendeleo duniani ili kutoa nafuu ya riba, kuwa endelevu, unaotabirika na unaozingatia usawa na vipaumbele vya mataifa yanayoendelea.

Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akihutubia Mkutano wa Nne wa Kimataifa kuhusu Ufadhili wa Maendeleo (FfD4) unaofanyika Jijini Sevilla nchini Hispania. Amesisitiza umuhimu wa mbinu za kibunifu katika ufadhili ikiwemo kubadili madeni ya kifedha kwenda katika utekelezaji wa miradi mbalimbali kama vile uhifadhi wa mazingira.

Vilevile Makamu wa Rais amesema taratibu za upimaji wa uwezo wa serikali kifedha katika ulipaji madeni unapaswa kupitiwa upya ili kuongeza uwazi na kuwa wa haki. Ameongeza kwamba Mkutano huo unapaswa kutoa ufumbuzi wa namna ya kupunguza gharama za ukopaji na kuongeza fursa za mikopo nafuu na ya muda mrefu.

Makamu wa Rais amesema kutokana na biashara kuwa nguzo ya kiuchumi ni vema mataifa kuwezeshwa katika uzalishaji na uongezawaji thamani wa bidhaa ili kufikia viwango vya kimataifa. Amesisitiza uwepo wa usawa na haki katika taratibu na sheria za kibiashara za kimataifa ikiwemo masuala ya ushuru wa forodha na ukomo wa mauzo kwa mataifa yanayoendelea.

Aidha Makamu wa Rais amesema unahitajika ushirikiano baina ya Mataifa yaliyoendelea na yanayoendelea katika kuharakisha maendeleo ya sayansi, teknolojia na takwimu ili kuweza kusaidia katika utungaji sera na utekelezaji kwa kuzingatia tafiti na takwimu sahihi.

Halikadhalika, Makamu wa Rais amesisitiza umuhimu wa Mataifa tajiri kushirikiana na nchi zinazoendelea katika kupunguza viatarishi kwenye uwekezaji na ufadhili wa miradi mikubwa ya kimkakati ya maendeleo.

Kuhusu Mazingira, Makamu wa Rais ametoa wito wa kutoa kipaumbele katika ufadhili wa usimamizi na urejerezaji wa bioanuai pamoja na kuongeza wigo wa ufadhili katika miradi ya kujenga uhimilivu na miradi ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Amesisitiza umuhimu wa kuanza kazi kwa mfuko wa mazingira wa kukabiliana na hasara na uharibifu unaosababishwa na mabadiliko ya tabianchi (Loss and Demage Fund).

Makamu wa Rais amesema kufikia mwaka 2024, Tanzania imefikia asilimia 60 ya utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) kwa kupiga hatua zaidi katika lengo namba 2 hadi namba 7 hususani katika maeneo ya afya, utoshelevu wa chakula, elimu, usawa wa kijinsia, upatikanaji wa maji safi na salama pamoja na upatikanaji wa nishati.

Ameongeza kwamba ili kuendeleza mafanikio hayo unahitajika ushirikiano na ufadhili wa gharama nafuu katika kuongezea mapato ya ndani ya nchi.

Mkutano wa Nne wa Kimataifa wa kuhusu Ufadhili wa Maendeleo unalenga kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazoikabili dunia katika kugharamia utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), kujadili njia za kurekebisha mfumo wa fedha wa kimataifa ili kuwa jumuishi, wenye usawa na unaozingatia mahitaji ya nchi zinazoendelea.

Malengo mengine ya Mkutano huo ni pamoja na kupendekeza mbinu bora za kupunguza na kushughulikia mzigo wa madeni kwa nchi maskini na zenye kipato cha kati pamoja na kujenga mifumo madhubuti ya kifedha inayoweza kukabili athari za majanga ya kiuchumi, kijamii na kimazingira.

Mkutano kuhusu Ufadhili wa Maendeleo ulianzishwa rasmi mwaka 2002 kupitia Mkutano wa kwanza uliofanyika Monterrey, Mexico na kupelekea kuundwa kwa msingi wa ushirikiano wa kimataifa katika kufadhili maendeleo. Mkutano wa Pili ulifanyika mjini Doha, Qatar mwaka 2008 ambao ulianzisha Azimio la Doha kusisitiza haja ya kuimarisha mshikamano wa kimataifa katika kukabiliana na athari za mtikisiko wa kifedha duniani.

Mkutano wa Tatu ulifanyika Addis Ababa, Ethiopia, mwaka 2015, na matokeo yake yalikuwa ni Addis Ababa Action Agenda (AAAA), ambayo ilijikita katika uhamasishaji wa vyanzo vya ndani vya mapato, ushirikiano wa kimataifa, uwekezaji wa sekta binafsi, pamoja na kushughulikia changamoto za madeni na usawa wa kijinsia.

Mkutano huu wa Nne ambao umepitisha Azimio la Sevilla unalenga kuchambua maendeleo yaliyopatikana tangu Addis Ababa na kujadili njia bora za kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu katika muktadha wa changamoto mpya kama vile mabadiliko ya tabianchi, migogoro ya kimataifa na athari za kiuchumi za janga la Uviko -19.

Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
30 Juni 2025
Sevilla - Hispania.

 -REA kuendela kuwajengea uwezo Magereza uendelezaji Miradi ya Nishati Safi


-Mhe. Balozi Radhia Msuya amewahamasisha Maafisa na Watumishi wa Magereza kuwa Mabalozi wa Nishati Safi

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Hafla ya ugawaji wa mitungi na majiko yake iliongozwa na Mhe. Balozi, Radhia Msuya, Mkurugenzi wa Bodi ya Nishati Vjijini (REB) katika gereza la ukonga, Jijini, Dar es Salaam, leo Juni 30, 2025 ambapo kwa upande wa Magereza uliwakilishwa na Msaidizi wa Mkuu wa Gereza hilo, Kamishna Msaidizi, (ACP); Athuman Recha.

Balozi, Radhia amesema kuwa, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA). Watumishi hao watasambaziwa mitungi ya gesi na majiko yapatayo 464 na kuongeza kuwa huo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Awamu ya Sita; Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kama nyenzo ya kulinda afya za Watanzania, kulinda na kutunza mazingira

Amesema kuwa, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeingia makubaliano na Jeshi la Magereza ili kuwawezesha, kuhama kutoka katika matumizi ya nishati isiyo salama kwenda katika matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia katika magereza yote nchini.

“Serikali kupitia REA, ilishaanza uwezeshaji kwa Jeshi la Magereza na wameshaanza kutumia Nishati Safi na kwa msisitizo huo, tuliona ni vyema, kuwawezesha Watumishi na Maafisa ili nao waachane na nishati chafu ili kulinda afya zao pamoja na kulinda mazingira yetu”. Amesema, Mhe. Balozi, Radhia.

Naye, Mkurugenzi wa Fedha na Uwezeshaji, CPA, Daniel Mungure ambaye alimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), amewataka watumishi wa jeshi la magereza kuibeba Ajenda ya Mhe. Rais Samia ya kuwa Mabalozi wa Nishati Safi ya kupikia kwa kuendelea kutumia gesi na siyo kuni na mkaa.

Akishukuru kwa uwezeshaji huo kwa Watumishi na Maafisa wa Jeshi la Magereza, Mrakibu Mwandamizi, (SSP); Moses Mumbi amesema, wanaishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwajali na kuongeza kuwa teknolojia hizo za Nishati Safi ya Kupikia si tu zinalinda afya zao lakini zinaongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao wakati wa kuwahudumia Mahabusu na Wafungwa.




 


Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum Kundi la Wenye Ulemavu  Ummy Nderiananga  Juni 30,2025 amechukua fomu ya kugombea Ubunge Viti Maalum kundi la Wanawake Wenye Ulemavu.


Nderiananga amekabidhiwa fomu hiyo katika Ofisi ya  Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na Katibu UWT  Mkoa wa Kilimanjaro  Ndug. Jane Chatanda.


Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,akikabidhi Cheti Mhitimu wa mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026 yaliyomalizika leo Juni 28,2025 jijini Dodoma.
.......
MWENYEKITI wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,ameagiza mambo manne kwa wahitimu wa mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi ghalani ikiwemo kufanya kazi kwa uwazi,tija na ufanisi ili kuweka imani kwa wakulima.
Maagizo hayo ameyatoa leo Juni 28,2025 Jijini Dodoma wakati akifunga mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026.
Mkanwa amewataka wahitimu hao kuongeza uwazi na ubora katika utendaji kazi wao ambapo amedai mfumo huo ni madhubiti katika kuondoa dhulma na kurasimisha biashara ya wakulima.
Pia amewataka kushughulikia udanganyifu kwa kuhakikisha haukubaliki katika jamii ya wakulima.
Aidha,amesema katika kukabiliana na jambo hilo,wamefunga CCTV Camera katika kila Ghala lengo likiwa ni kuondoa udanganyifu ambapo amedai wale ambao watawabaini watawachukulia hatua kali za kisheria.
Mkanwa amesema mfumo wa Stakabadhi Ghalani umemsaidia mkulima kupata bei nzuri huku akitoa wito kwa wasimamizi hao kuwa walinzi na waadilifu katika kila walichofundishwa.
"Toeni taarifa kwa uwazi jukumu lenu kutunza Imani ya wakulima na wadau,mkitoa taarifa kwa uwazi ili tutunze Imani ya watu wetu,"amesema Bw.Mkanwa
Kwa upande ,Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) Bw. Asangye Bangu,amewapongeza wahitimu hao kwa kumaliza mafunzo hayo huku akiwataka mafunzo waliyoyapata kuyatumia katika utendaji kazi wao.
"Matarajio yetu tumekufundisha umeelewa,fanya kazi ukiona kitu cha kibunifu usiache kuwasiliana na wataalamu,usifanye maamuzi mwenyewe wasiliana na sisi.Tusisababishe matatizo kwa tamaa,"amesema
Pia amesema lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha watendaji katika maghala wanafuata utaratibu kwa maana ya ubora na uzito.
"Timu za wataalamu zinaendelea kuwapatia mafunzo mara kwa mara mafanikio ni makubwa sasa hivi tuna mazao 16 tulianza na Mikoa ya Kusini, leo tupo zaidi ya mikoa 24 huu ndio mfumo mzuri kwani unaweza kumsaidia mkulima kupata bei ya ushindani,"amesema Bw.Bangu
Kuhusu ufungaji wa CCTV kamera katika maghala amesema tayari Serikali
imetoa Sh milioni 126 kwa ajili ya kununua CCTV Camera ambazo zitafungwa katika maghala mbalimbali nchini.
"Tutahakikisha maghala yote yanakuwa na camera kwa ajili ya kutoa taarifa kwani baada ya kufunga wizi umepungua,"amesema
Mhitimu wa mafunzo hayo, Christina Gerald amesema kupitia mafunzo hayo amejifunza vitu vingi ikiwemo kujua mnyororo wa thamani katika mazao.
MWENYEKITI wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,akizungumza leo Juni 28,2025 Jijini Dodoma wakati akifunga mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026.
MWENYEKITI wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,akizungumza leo Juni 28,2025 Jijini Dodoma wakati akifunga mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026.
MWENYEKITI wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,akisisitiza jambo kwa wahitimu wa mafunzo wakati akifunga mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) Bw. Asangye Bangu,akizungumza wakati wa kuhitimishwa mafunzo ya ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026 yaliyomalizika leo Juni 28,2025 jijini Dodoma.
SEHEMU ya wahitimu wa mafunzo wakisikiliza hotuba ya Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,(hayupo pichani) wakati akifunga mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026.
SEHEMU ya wahitimu wa mafunzo wakisikiliza hotuba ya Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,(hayupo pichani) wakati akifunga mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026.
SEHEMU ya wahitimu wa mafunzo wakisikiliza hotuba ya Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,(hayupo pichani) wakati akifunga mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026.
SEHEMU ya wahitimu wa mafunzo wakisikiliza hotuba ya Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,(hayupo pichani) wakati akifunga mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026.
Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,akikabidhi vyeti kwa wahitimu mbalimbali wa mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026 yaliyomalizika leo Juni 28,2025 jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,akikabidhi vyeti kwa wahitimu mbalimbali wa mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026 yaliyomalizika leo Juni 28,2025 jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,akikabidhi vyeti kwa wahitimu mbalimbali wa mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026 yaliyomalizika leo Juni 28,2025 jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,akikabidhi vyeti kwa wahitimu mbalimbali wa mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026 yaliyomalizika leo Juni 28,2025 jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,akikabidhi vyeti kwa wahitimu mbalimbali wa mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026 yaliyomalizika leo Juni 28,2025 jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,akikabidhi vyeti kwa wahitimu mbalimbali wa mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026 yaliyomalizika leo Juni 28,2025 jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala,Godwin Mkanwa,akikabidhi vyeti kwa wahitimu mbalimbali wa mafunzo ya mfumo wa Stakabadhi Ghala kuelekea Msimu wa mazao ya Mbaazi na Dengu 2025-2026 yaliyomalizika leo Juni 28,2025 jijini Dodoma.