MBUNGE wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi kulia akimkabidhi Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhamani Shiloo kushoto gari la kubebea Wagonjwa (Ambulace) kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Mikanjuni ambalo limetolewa na Mbunge huyo mapema leo kulia anayeshuhudia ni Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mikanjuni Mwajame Bausy wa pili kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Spora Liana 

Gari la Kubeba wagonjwa Ambulance ambalo limetolewa na Mbunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu kama linanyoonekana 

Mbunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi akiwa kwenye picha ya pamoja mara baada yua makabdhiano hayo leo

Mbunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi akizungumza na wananachi waliofika kwenye kituo cha Afya Mikanjuni Jijini Tanga mara baada ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa ambalo amelitoa kulia ni Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhamani Shiloo  wa wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Spora Liana
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abduraham Shiloo akizungumza wakati wa halfa hiyo kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Tanga(CCM) Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi na kulia ni Diwani wa Kata ya Mabawa
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mikanjuni Mwajame Bausy akitoa taarifa ya kituo hicho kwa Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi
Diwani wa Kata ya Mabawa akizungumza

 

 
NA OSCAR ASSENGA, TANGA

 

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi Ummy Mwalimu amemtaka Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Spora Liana kutokumuonea aibu Afisa wa Afya yoyote ambaye atakwenda kunyume na miongozo na taratibu za utoaji huduma kwenye vituo vya afya Tanga Jijini humo.

Aliyasema hayo leo wakati akikabidhi gari maalumu ya kubebea wagonjwa (Ambulace) kwenye kituo cha Afya Mikanjuni ambapo limetolewa na Waziri Ummy Mwalimu ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM)

Hatua hiyo ya mbunge huyo kutoa msaada huo wa gari ni kuondosha kero ambazo zilikuwa zinawakabili wananchi hususani wagonjwa ambazo walikuwa wakikumbana nazo wakati wakihitaji kupata huduma ya dharura.

 Alisema kwa sababu Rais anataka kuwatumikia wananchi wa Tanga na watanzania wanyonge sasa kama dawa zinakuja na watu wanaambiwa hakuna na wanafanya mambo kijanjajanja wasivumiliwe hata kidogo

“Ndugu zangu Tanga Jiji haitakiwi vituo vya kutolea huduma vikakosa dawa Mkurugenzi lisimamieni tunataka dawa ziwepo kwenye vituo vya afya na zahanati na mjitathimini tusianze kutafutana uchawi Je mnakwenda sahihi na miongozo ya Serikali?Alihoji Waziri Ummy.

Alisema wanachotaka ni wahakikishe huduma bora zinapatikana lakini niwapongeze pia watumishi na wahudumu wa afya kwa kazi nzuri wanayofanya kwa kuhakikisha wananchi wanapata matibabu.

“Lakini niwaambie Rais Marehemu Magufuli amelala lakini kazi yake inaonekana na Rais Samia Suluhu ataendeleza hivyo wana Tanga tuendelee kumuunga mkono kwani amedhamini kuleta maendeleo makubwa”Alisema

Hata hivyo alisema yeye kama mbunge aliamua kutoa msaada huo baada ya kupokea kero kutoka kwa Diwani Kata ya Mabawa na wananchi kuhusu gari la kubebea Wagonjwa (Ambulance) kwa sababu mgonjwa anatakiwa kupelekwa bombo gari haiji kwa wakati na hivyo kupelekea uwepo wa changamoto”Alisema

Hata hivyo alisema aliona njia nzuri ya kuweza kuondosha kero hiyo ni kuwanunulia gari hilo kutokana na kata hiyo ni miongoni mwa kata zilizomuunga mkono .

“lakini pia niwaashe mhakikishe mnaitunza gari hii na Mkurugenzi mtafanya taratibu za kuihamisha iwe sm na tutakabidhi funguo na atatufwe dereva kwa ajili ya kuiendesha na niwaahaidi kwamba nitaenda kutafuta kwa ajili ya vituo vya afya nyengine”Alisema

Awali akizungumza Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhamani Shiloo amesema katika vituo vya afya kila mwananchi anaapopata huduma kwenye vituo vya afya au zahanati kuhakikisha anapewa risiti za kieletroni kutokana na fedha aliyopewa na hakuna lugha mbadala.

Alitoa wito kwa wananchi ili waweze kuunga mkono juhudi za mbunge ili fedha ziweze kuleta tija na maslahi mapana kwa wagonjwa ili waweze kununua vifaa tiba na dawa ili wagonjwa waweze kuhudumiwa.

“Pili niombe vifaa vitakavyokuwa vikitolewa na vinavyotolewa vitumike kwa maslai mapana na wananchi wa Jiji la Tanga ili kuunga mkono juhudi za mbunge kwa sababu yeye ameamua kushughulika na matatizo ya wananchi wa Tanga ili kuhakikisha anaondosha kero zao.

Naye Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mikanjuni Mwajame Bausy aliishukuru Serikali ya awamu ya sita na uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga kwa upanuzi mkubwa uliofanyika kwenye kituo hicho .

Alisema katika upanuzi huo majengo matatu yamejengwa kwa gharama ya sh milioni 400 na yamekamilika na yameanza kutumika na kutoa huduma kwa wananchi.

“Hali hii imeongeza ubora wa huduma zinazotolewa kwenye kituo na kuongeza mapato yatokana na huduma za afya na robo ya mwisho mwaka 2020/2021 kituo kilikusanya miloni 14.2 ukilinganisha na mapato ya robo ya mwaka ya mwaka wa fedha 2021/2022 kituo kilikiusanya kiasi cha milioni 22.2”Alisema

Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: