Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Marehemu Ibrahimu Hussein ambaye alikuwa mfanyakazi wa Jimbo Katoliki Singida aliyefariki dunia mwanzoni mwa wiki wakati akipatiwa matibabu Hospitali ya Misheni ya Makiungu mkoani Singida.

Marehemu Ibrahimu Enzi za Uhai wake.

Askofu wa Jimbo Katoliki Singida Mhashamu Edward Mapunda (katikati) akiongoza ibada ya Misa Takatifu ya kuaga mwili wa marehemu Ibrahimu Hussein.Kulia ni Paroko Msaidizi wa Parokia ya  Moyo Mtakatifu wa Yesu, Father Kinanda.
Ibada hiyo ikiendelea.
Askofu wa Jimbo Katoliki Singida Mhashamu Edward Mapunda akinyunyuzia mafuta ya baraka kwenye jeneza la marehemu.
Ibada hiyo ikiendelea.
Huzuni katika ibada hiyo.
Vilio vikitawala katika ibada hiyo.
Vilio vikitawala katika ibada hiyo.
Ni vilio vitupu vikitawala katika ibada hiyo.
Askofu wa Jimbo Katoliki Singida Mhashamu Edward Mapunda akiongoza msafara wakati wa kuingiza jeneza la marehemu kwenye gari tayari kwenda kijijini kwao kwa mazishi.
Watawa wa Jimbo Katoliki Singida wakiwa kwenye ibada hiyo ya kuaga mwili wa marehemu.



Watawa wa Jimbo Katoliki Singida wakiaga mwili wa marehemu.

Ibada hiyo ikiendelea.
Waombolezaji wakiaga mwili wa marehemu.
Wafanyakazi wenzake na marehemu wakiwa kwenye ibada ya kumuaga mwenzao.
 


Na Dotto Mwaibale, Singida


JUMUIYA ya Waumini na Wafanyakazi wa Jimbo Katoliki Singida imepata pigo na kusababisha vilio na majonzi baada ya kumpoteza mmoja wa Wafanyakazi wake mahiri Ibrahimu Hussein ambaye amefariki dunia mwanzoni mwa wiki wakati akipatiwa matibabu Hospitali ya Misheni ya Makiungu mkoani Singida.

Akiongoza ibada ya Misa Takatifu ya kuaga mwili wa marehemu Askofu wa Jimbo Katoliki Singida Mhashamu Edward Mapunda alisema Jumuiya ya Wakatoliki Singida itamkumbuka na kuendelea kumuombea kwa namna alivyojitoa  kutekeleza matendo mema katika kipindi cha uhai wake.

"Tuendelee kumuombea.Kifo cha kimwili sawa...lakini kifo cha kiroho ni kibaya zaidi sababu ni chukizo mbele ya Mungu. Kifo cha kijana huyu ni cha baraka, neema na ni mlango wa kuingia mbinguni.. kumuona Mungu," alisema Askofu Mapunda.

Baadhi ya walioguswa na msiba huo walisema Ibrahimu alikuwa ni kijana wa aina yake kwani hata alipokuwa akitumwa hakuonesha kukataa wakati wote alikuwa akitabasamu.

Mazishi ya marehemu  Ibrahimu Hussein yalifanyika jana nyumbani kwao Mang'onyi wilayani Ikungi mkoani hapa.

Share To:

Post A Comment: