Msanii maarufu nchini katika Muziki wa bongofleva Judith Wambura a.k.a Lady J Dee katikati akishuhudia gari yake ikijazwa Mafuta ikiwa ni zawadi kutoka Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania ikiwa ni sehemu ya kampuni  hiyo kutambua mchango wa Wanawake wa Kada mbalimbali katika maendeleo ya nchi yetu katika kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa jana Machi 8,2021.

Mwanadada maarufu katika anga ya muziki wa kizazi kipya Judith Wambura a.k.a Lady Jay Dee akitoa shukurani kwa Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania kwa zawadi ya Mafuta waliompa kama sehemu ya kutambua mchango wake na mchango wa Wanawake wengine wote katika kuleta Maendeleo nchini.Zawadi hiyo inakwenda sambamba na maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo Machi 8 ya kila Mwaka

Msanii maarufu nchini katika Muziki wa bongofleva Judith Wambura a.k.a Lady Jay Dee katikati akiwa na Wafanyakazi wa Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania baada ya kumkabidhi zawadi ya kumjazia mafuta ‘full tank’ kwenye gari yake na zawadi ndogo,ikiwa ni sehemu ya kampuni hiyo kutambua mchango wa Wanawake wa Kada mbalimbali katika maendeleo ya nchi yetu katika kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa jana Machi 8,2021.

Wafanyakazi wa Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania wakiwa na Mwanamama Mwenye ulemavu wa viungo Bi.Jasmine Milanzi anaejishughulisha na utoaji wa huduma ya usafiri mkoani Dar es Salaam kwa kutumia Bajaji yake alipokuwa akijaziwa mafuta na kampuni hiyo kama zawadi kwa Wanawake katika kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa jana Machi 8,2021.

Wanawake wenye Ulemavu wa Viungo wanaojishughulisha na utoaji huduma ya kusafirisha abiria kwa Bajaji mkoani Dar es Salaam wakiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania mara baada ya kujaziwa mafuta kwenye Bajaji zao ikiwa ni zawadi kwa Wanawake wote nchini katika kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa jana Machi 8,2021.


KAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania ambayo ni namba moja katika biashara ya mafuta imeungana imeungana na wanawake wote duniania katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya mwanamke inayo adhimishwa tarehe 8 Machi kila mwaka huku ikieleza kwamba inatambua na kuthamini mchango wa makundi yote ya wanawake nchini katika kushiriki katika shughuli za ujenzi wa Taifa letu.

Aidha kampuni hiyo kwa kutambua umuhimu wa siku ya Wanawake Duniani , pamoja na mchango wao  imeamua kuitumia siku ya leo pamoja na mambo mengine kutoa zawadi ya mafuta kwa wanawake  katika makundi mbalimbali wakiwemo wanawake viongozi, mashuhuri pamoja na wanawake  wajasiriamali wadogowadogo walioko kwenye maeneo mbalimbali.

Wakizungumza wakati wa kuadhimisha siku hiyo na baada ya kutoa zawadi ya mafuta kwa wanawake  wa makundi mbalimbali wakiwemo wanawake wanaondesha Bajaji kwa ajili ya kujitafutia riziki,  maofisa wa kampuni kwa nyakati tofauti wameeleza kwamba kwa kutambua umuhimu wa Wanawake  kwenye jamii ya kitanzania na wakiwa msatari wa mbele kusheherekea mafanikio ya wanawake walioko  nchini, kampuni ya Puma Energy Tanzania Limited imeamua kuadhimisha siku hiyo kwa  kuwatambua  baadhi ya wanawake wa kupigiwa mfano kwenye jamii yetu na kuwazawadia full tank ya mafuta kwenye  magari yao pamoja bajaji.

Akielezea zaidi baada ya kuwazawadia mafuta wanawake hao wakupigiwa mfano iliyo fanyika katika  kituo cha Mafuta cha Puma Upanga, Meneja wa Operations wa Kampuni Lameck Hiliyai amesisitizia  Puma Energy Tanzania inathamini mchango wa wanawake katika kampuni na katika jamii na inafanya  kila jitihada kuhakikisha kunakuwa na uwiano unaoridhisha wa wanawake na wanaume katika kampuni.

Aidha, amewahamasisha wanawake kujitokeza zaidi kushiriki katika shughuli mbalimbali katika  biashara ya mafuta na kuachana na kasumba zilizo zoeleka kwamba hizi ni shughuli za wanaume na  kwamba kampuni hiyo ambayo ni namba moja Tanzania katika biashara ya mafuta ni wajibu wao  kuendelea kuboresha hali za wafanyakazi wao wanawake lakini zaidi  wanawake katika jamii mbalimbali  zinazowazunguka.

Awali Meneja wa Rasilimali watu wa Puma Energy kwa bara Afrika Loveness Hoyange alieleza kuwa  kampuni hiyo inatambua namna wanawake hao wanavyocharika katika harakati za ujenzi wa taifa. "Tunatambua namna gani wanawake siku hizi wanajituma, mfano hawa wenye ulemavu hawajachukulia  hali yao kuwa sababu ya kujibweteka wanafanya kazi inayowawezesha kuendesha maisha".

Ameongeza kwa kuliona hilo, kampuni yao imeamua kuwapatia mafuta ili nao waweze kusherehekea siku hii ya wanawake kwa pamoja huku akisisitiza wanatambua mchango wao katika sekta ya usafirishaji.

Kwa upande wake mwanamama Jasimin Milanzi  mwenye ulemavu wa viungo ambaye anajishughulisha na utoaji huduma ya kusafirisha abiria kwa kutumia usafiri wa bajaji, amesema anajisikia fahari kuwa miongoni mwa wanawake ambao wamepata zawadi ya kujaziwa mafuta na kampuni hiyo na imedhihirisha kumbe nao mchango wao kwenye jamii unatambulika huku akisisitiza licha ya kwamba ni walemavu wa viungo lakini wana akili kama walivyo binadamu wengine.

Share To:

Post A Comment: