Na Eleuteri Mangi, WHUSM, Dodoma

Serikali inaendelea na zoezi la Kidemokrasia la wananchi kuboresha taarifa za wananchi kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura ambazo zitatumika kwenye Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Mdiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2020.

Msemaji Mkuu wa Serikali na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi ameongoza zoezi hilo kwa Makatibu Wakuu leo Mei 04, 2020 hapa jijini Dodoma kuhakiki na kuhuisha taarifa zao katika ikizingatiwa leo ni siku ya mwisho kwa zoezi hilo nchini kote.

“Serikali inaendelea kukamilisha kuboresha Daftari la Kudumu la Mpiga Kura, Serikali zoezi hili ni muhimu sana kwa nchi yetu ikizingatiwa ni la kidemokrasia licha ya kwamba nchi yetu na dunia nzima inapitia kwenye changamoto tuliyonayo ya COVID-19” alisema Dkt. Abbasi.

Ameongeza kuwa Demokrasia itaendelea kuheshimiwa nchini kwa sababu ni kitu muhimu sana na viongozi hao pamoja na wananchi waliojiandikisha kutumia haki yao ya Kikatiba kuchagua viongozi wao.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome amesema kuwa Wizara yake inajukumu la kuhamasisha mambo mbalimbali ikiwemo elimu ya haki ya Mpiga kura.

“Nchi yetu imepiga hatua kubwa sana katika demokrasia kiasi kwamba tunajivunia hatua tuliyofika ni nzuri na demokrasia imekuwa ni ya kweli hakuna mwaka ambao tumevuka miaka mitano hatujafanya uchaguzi na wanannchi wamekuwa wakijitokeza kwa wingi kuwachagua viongozi wao” alisema Prof. Mchome.

Lengo la elimu ya mpiga kura ni kuwahamasisha wananchi kutumia haki yao ya kikatiba katika kujitokeza na kushiriki kuchagua viongozi wao watakao waongoza ili kujenga Demokrasia na Utawala Bora nchini hatua inaanza kwa wananachi kijiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura ambalo linaratibiwa na kusimamiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). 



Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi akiwasisitiza wananchi nchini nzima kwenda kujiandikisha na kuhuisha taarifa zao kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura katika meneo yao ambapo leo Mei 04, 2020 ni siku ya mwisho kujiandiskisha na kuhuisha taarifa za wapiga kura kabla ya Uchaguzi Mkuu mwaka huu. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome akihimiza wananchi kujiandikisha na kuhuisha taarifa zao kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura ili wawe na sifa ya kutumia haki yao ya Kikatiba wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka huu kuchagua viongozi wao. Wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, (Sekta ya Mawasiliano), Dkt. Zainab Chaula na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano) Dkt. Jim Yonazi (kulia). 
Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi akiweka sahihi yake wakati wa kuhuisha taarifa zake katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura leo Mei 04, 2020 jijini Dodoma.
Katibu Mkuu mpya wa Ofisi ya Rais Ikulu Dkt. Moses Kusiluka akiweka alama za vidole wakati wa kuhakiki taarifa zake kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura leo Mei 04, 2020 jijini Dodoma. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt. John Jingu akimsikiliza Mwandishi Msaidizi Celina Kilangi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) wakati wa kuhakiki taarifa zake kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura katika leo Mei 04, 2020 jijini Dodoma
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Mbunifu Majengo, Elius Mwakalinga akiweka sahihi yake baada ya kuhuisha taarifa zake katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura leo Mei 04, 2020 jijini Dodoma. 
Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, (Sekta ya Mawasiliano), Dkt. Zainab Chaula akijaza fomu ya kuhuisha taarifa zake katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura leo Mei 04, 2020 jijini Dodoma.(Picha na Eleuteri Mangi, WHUSM, Dodoma).
Share To:

Post A Comment: