Yassir Simba,

Klabu ya Yanga imethibitisha kumalizana na kiungo wake mkabaji ambaye ni nahondha wa klabu hiyo raia wa Congo DRC Pappy Kabamba Tshishimbi ambaye mkataba wake ulikuwa unaelekea ukingoni mwishoni mwa msimu huu wa ligi kuu Tanzania bara.

Kiungo huyo ambaye siku za karibuni alikuwa akitajwa kuwaniwa na baadhi ya vilabu vya ligi kuu ikiwemo wekundu wa msimbazi Simba, rasmi sasa atasalia kwa wananchi hao wa jangwani mpaka 2022 kutokana na taarifa za awali kuwa ameingia kandarasi ya miaka 2 na mabingwa hao wa kihistoria.

Kupitia Mkurugenzi wa uwekezaji wa kampuni ya GSM Hersi Said amesisitiza kuwa, "Tshishimbi ni mali ya Yanga kwa sasa na haendi popote labda wanaomuhutaji wasubiri mpaka mkataba huu wa sasa utakapo malizika."
Share To:

msumbanews

Post A Comment: