NAIBU Waziri wa Maji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akizungumza wakati wa ziara yake kushoto ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly kulia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo
WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) kushoto akimsikiliza kwa umakini  Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo wakati wa ziara yake wilayani humo katika aliyevaa kofia ya kijani ni Mbunge wa Jimbo la Muheza Balozi Adadi Rajabu
 NAIBU Waziri wa Maji Jumaa Aweso ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) kushoto akimsikiliza kwa umakini Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini wakati wa ziara yake leo
 NAIBU Waziri wa Maji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM)  kushoto akiangalia chanzo cha maji cha Mto Pangani kilichopo eneo la Mandera wilayani Korogwe wakati wa ziara yake ya kukagua chanzo hicho leo
NAIBU Waziri wa Maji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) kulia akitembelea kwenye maeneo mbalimbali kwenye chanzo hicho akiwa na Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini (CCM) Mary Chatanda wakati wa ziara yake.
 NAIBU Waziri wa Maji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) kulia akikagua kwenye maeneo mbalimbali kwenye chanzo hicho akiwa na Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini (CCM) Mary Chatanda kushoto wakati wa ziara yake.
 NAIBU Waziri wa Maji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) katikati aliyevaa koti akiwa na Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini (CCM) Thimotheo Mzava na Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini (CCM) Mary Chatanda wakati wa ziara yake wakiangalia chanzo cha maji

Chanzo cha Maji cha Mto Pangani ambaho kitatumika kwenye miradi hiyo ya maji

SERIKALI imesema kwamba itatumia chanzo cha Mto Pangani kutatua tatizo la maji kwenye miji ya Handeni, Pangani, Muheza na Korogwe ili kuondosha kero hiyo ambayo imedumu kwa muda mrefu kwenye maeneo hayo

Hatua hiyo imekuja baada ya serikali kupata fedha dola milioni 500 kutoka Serikali ya India kuweza kutekeleza miradi wa maji kwenye miji 28 hapa nchini ambapo zaidi ya wananchi 600,000 watanufaika

Hayo yalisemwa leo na Naibu Waziri wa Maji Jumaa Aweso wakati alipofanya ziara yake kwenye wilaya za Muheza na Korogwe kukagua chanzo maji cha Mandera ambacho kitatumika kuchukua maji katika mradi mkubwa wa ukarabati wa mradi wa HTM kwa ufadhili wa fedha za india kwa miji minne.

Alisema kwamba kutokana na hilo changamoto ya aji kwenye miji hiyo itakuwa imepata ufumbuzi kutokana na juhudi kubwa ambazo zimefanywa na serikali kuweza kupatikana fedha hizo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi.

“Labda niwaambie kwamba Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt Magufuli imedhamiria kumaliza changamoto ya maji kwenye mji wa Muheza na maeneo mengine kwa lengo la kumtua mama ndoo kichwani “Alisema Naibu Waziri Aweso.

Alisema kwamba wakati wa utekelezaji wa mradi wa kutoka Maji Mto Pangani kwenye miji hiyo matenki makubwa na eneo la kutibu maji yatajengewa eneo la Segera na baadae kupelekea maeneo husika kwa ajili ya wananchi kupata huduma hiyo muhimu.

“Lakini chanzo hicho kitakuwa ni cha mserereko kuhakikisha wanapunguza gharama za uendeshaji wa mradi huo hivyo ni imani yangu kwamba mradi huo utakapokamilika wananchi wataondokana na adha ya maji kwa dhani ya Rais kumtua mama ndoo kichwani “Alisema

Hata hivyo alisema kwamba wahandisi wa Halmashauri wamekwisha kupita maeneo yote na hivyo hivi sasa wanasubiri kibali kitakapotoka mradi huo utaanza mara moja ikiwemo kutangaza tenda kuwapata wakandarasi ili mradi huo uanze kwa wakati.

“Labda niwaambieni kwamba sisi kama viongozi wa wizara hatutakuwa kikwazo kuhakikisha mradi huo unaanza kutekelezwa kwa wakati kuwawezesha ananchi waweze kupata maji”Alisema

Naibu Waziri huyo alisema kwamba wanatambua uwepo wa changamoto kubwa ya maji wilaya ya Muheza lakini mradi wa maji utakaotokaa Pongwe utasaidia kupunguza adha hiyo lakini mradi huo mkubwa utapunguza tatizo la maji.

Awali akizungumza wakati wa ziara hiyo Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu alisema ujio wa ziara ya Naibu Waziri huyo ni ishara kwamba wilaya ya Muheza inakaribia kufurika maji kutokana na uwepo wa chanzo hicho kikubwa cha Mto Pangani.

“Naamini Kata nyingi zitanufaika hivyo niombe wakandarasi waje mapema kazi hiyo ianze haraka kwa sababu wananchi muheza wamevumilia muda mrefu na kuna kilio cha tatizo hilo hivyo kupitia mradi huo wanaweza kuondokana na adha hiyo “Alisema Mbunge Balozi Adadi.

Awali akizungumza wakati wa ziara hiyo Mkurugenzi Mtendaji Mtendaji wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira (HTM) Mhandisi Yohana Mgaza alisema kwamba chanzo cha Mandera hicho kitatumika kuchukua maji kwenye mradi mkubwa wa ukarabati wa mradi huo wa HTM kwa ufadhili wa fedha za India kwa miji hiyo.

Alitaja miji hiyo kuwa ni Korogwe, Handeni,Pangani na Muheza na vijiji vitakavyokuwa pembeni ya bomba ambapo mradi huo ni mkubwa na utanufaisha watu zaidia ya laki sita.

Mwisho.
Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: