Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi ameziagiza familia za askari waliouawa wakilinda amani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kumaliza haraka taratibu za mirathi.

Pia, amesema Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Venance Mabeyo amekwisha kuunda Baraza la Uchunguzi, kuchunguza kupotea kwa askari mmoja aliyekuwa akilinda amani DRC.

Waziri Mwinyi ameyasema hayo jana Mei 14 wakati akihitimisha hotuba ya bajeti ya wizara yake ya mwaka 2018/19 ya Sh1.9 trilioni.

Waziri Mwinyi alisema tayari baadhi ya familia za askari hao zimeshakamilisha taratibu za mirathi.

Alisema fedha za mirathi zimetolewa kwa baadhi ya familia lakini zipo baadhi hazijakamilisha taratibu.

 “Familia ambazo hazijakamilisha taratibu za mirathi zikamilishe haraka,” alisema.

Kuhusu askari mmoja aliyepotea siku hiyo ya mapigano Waziri Mwinyi alisema: “Umoja wa Mataifa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, wanaendelea kumtafuta na ikitimia miezi sita kwa Serikali ya Tanzania tutaitisha uchunguzi na Mkuu wa Majeshi ameitisha baraza la uchungizi,” alisema.

Alisema baada ya hapo Mkuu wa Majeshi atatoa taarifa ya kifo. “Lakini huyu kijana amepotea na mpaka sasa anatafutwa, hatuwezi kusema amepotea au yuko hai.” Alisema
Share To:

msumbanews

Post A Comment: