Spika wa bunge Job Ndugai leo ameingia bungeni kuongoza kikao cha tano katika mkutano wa 11. Ndugai hakuwepo bungeni kwa muda mrefu baada ya kuelezwa kuwa alikuwa nje ya nchi kwa matibabu.

Wabunge wamemshangilia kwa kumpigia  makofi kutoka pande zote wakiongozwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Katika mkutano wa 10 uliofanyika kwa wiki mbili kiongozi huyo hakuonekana bungeni wakati wote.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: