MAKAMISHNA Wasaidizi Waandamizi wa Uhifadhi wanawake kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) wapo nchini Indonesia kushiriki mkutano wa mtandao wa wanawake maafisa waandamizi wa Polisi na vyombo vingine vya usalama unaofanyika nchini humo.

Makamishna hao wanaongozwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Rasilimali Watu na Utawala, Salma Chisonga, ambapo wanatarajiwa kushiriki katika majadiliano na kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya ulinzi, uhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii.

Mkutano huo wa siku tano umewakutanisha wanawake kutoka vyombo mbalimbali vya usalama kutoka nchi tofauti duniani kwa lengo la kujadili fursa na changamoto zinazowakabili wanawake katika vyombo vya usalama pamoja na taasisi zinazolinda rasilimali za nchi.

Aidha, ushiriki wa makamishna hao unatarajiwa kutoa fursa kwa Tanzania kubadilishana uzoefu na mataifa mengine kuhusu namna ya kuimarisha ushiriki wa wanawake katika ulinzi, uhifadhi wa rasilimali na usimamizi wa maeneo ya utalii.

Mkutano huo pia unalenga kuimarisha ushirikiano na mitandao ya wanawake katika vyombo vya usalama duniani, huku ukitoa nafasi ya kujifunza mbinu na uzoefu mbalimbali katika kukabiliana na changamoto za kiusalama na uhifadhi.


Share To:
Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Post A Comment: