Wakati Maonesho ya Nanenane yakiendelea kupamba moto katika maeneo mbalimbali nchini, Hifadhi ya Ngorongoro imeendelea kutanua mbawa zake na kuonesha vivutio vya utalii mubashara kupitia mitandao ya kijamii na luninga kubwa iliyofungwa kwenye banda la Wizara ya Maliasili na Utalii.

Watalii wanaotembelea maonesho hayo wameshuhudia vivutio vya wanyama mbalimbali kama Faru, Tembo, Pundamilia, Swala, Nyumbu, Simba wakiwa honeymoon, na makundi ya Nyati yakiwa yanajimbwafai katika maeneo yao ya asili.

Akiwa katika Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii, Meneja wa Idara ya Utalii na Masoko wa Ngorongoro SACC. Mariam Kobelo, ameeleza kuwa Ngorongoro imeendelea kuwekeza kwenye miundombinu ya utalii na kuboresha huduma ili wageni waweze kushuhudia vivutio mubashara na kufurahia huduma zinazotolewa na Ngorongoro.

“Ngorongoro ikiwa ni eneo la kipekee, tumejipanga kuendelea kutumia teknolojia za kisasa kufikia watu na kuona maajabu na simulizi adhimu za kipekee.

Share To:

Post A Comment: