Kwa miezi 18 maisha yangu yalizunguka jambo moja tu kutafuta kazi. Kila asubuhi nilikuwa naamka mapema, kufungua simu au laptop yangu, na kutafuta matangazo mapya ya ajira.

Nilikuwa na ndoto ya kupata kazi nje ya nchi ili niweze kubadilisha maisha yangu na kusaidia familia yangu. Niliamini elimu na uzoefu wangu vingefungua milango mingi. Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia.

Nilituma CV kwa kampuni nyingi sana. Kila nilipoona tangazo jipya, nilihakikisha nimetuma maombi yangu kwa wakati. Wakati mwingine nilikuwa natumia saa nyingi kurekebisha CV na cover letter ili ziendane na nafasi husika.

Kilichoniumiza zaidi ni kutopata majibu. Wiki zikageuka miezi. Nilikuwa naangalia email kila siku nikitarajia mwaliko wa interview, lakini hakuna kilichokuwa kinatokea. Wakati mwingine nilipokea ujumbe wa kukataliwa, na mara nyingi sikupata jibu lolote.

Kwa kweli nilianza kukata tamaa. Nilianza kujiuliza kama kulikuwa na tatizo kwenye qualifications zangu au kama ndoto yangu ilikuwa kubwa sana. Watu wengine walinishauri niache kufikiria kazi za nje na nijikite kwenye nafasi za karibu. SOMA ZAIDI.
Share To:

Post A Comment: