Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhandisi Maryprisca Mahundi, ameagiza  Chuo  cha Maendeleo ya jamii Uyole   kupitia  dhana  ya  ushirikishwaji  jamii kupinga  vitendo  vya  ukatili  wa kijinsia  na  kutaka  kazi    hiyo kuwa  endelevu ndani  na  nje ya chuo 

Mahundi  amezungumza  hayo  wakati  wa mahafali  ya kumi  na  sita  ya  chuo  cha  maendeleo  ya  jamii  CDTI uyole  yaliofanyika  viwanja  vya michezo  chuo cha maendeleo  ya jamii  Uyole  na kusema  licha  ya  siku  kumi na  sita  za kupinga ukatili  kufanyika  lazima   zoezi hilo  likawe  endelevu

Ameitaka    jamii  inayozunguka  Chuo na kila  mwanafunzi   ni  vema kila  mmoja  akawa mjumbe kupeleka  elimu  ya kupinga ukatili  hasa  wanaporudi  nyumbani  au  katika  sehemu za kazi.

Mahundi  amesema  ni  mategemeo  ya  Wizara na  Serikali  kwa  ujumla kuwa  watumishi  na wanafunzi  wa  Chuo  hicho  wataendelea  kutimiza  wajibu  kwa  kufanya  kazi  kwa  bidii na kuendelea  kuzingatia  sheria,taratibu,kanuni   na  miongozo mbalimbali  ya Kitaifa na   kama  wakifanya  hivyo  wataendelea  kutoa  wahitimu mahili na wenye maadili  mema  wanaoweza  kushindana  katika soko  la  ajira .   

Amesema  mustakabali  wa  Taifa  lolote  duniani  unategemea  sana mchango wa Taasisi  za mafunzo  katika  kuandaa wataalamu mahili na  wenye  weredi  ambao  ndio  chachu  ya kuleta mageuzi  ya kifkra na maendeleo  jumuishi  na  endelevu  katika  jamii  yoyote

Naibu  Waziri  Mahundi  ameongeza  kuwa  Wizara  inatambua  mchango  mkubwa uliotolewa  na Chuo  cha maendeleo  ya  jamii Uyole  katika  kuanda  wataalamu wa maendeleo  ya jamii ambao  wanatoa  mchango  mkubwa  katika  maendeleo  ya taifa  na  kuwapongeza wakufunzi  kwa  kufanya  kazi hiyo kwa uweledi.

Mhandisi  Mahundi  amesema  katika  kutekeleza  dhana  ya  uanagenzi ,ubunifu  na  kusema  kama   zitatekelezwa vyema zitawawezesha  wahitimu  kuajiliwa  kwa  urais  zaidi,kijiajili  na kuajili  wengine  huku  jamii  inayozunguka  Chuo hicho  ikinufaika  na mafunzo  hayo.

Kwa  upande  wake  Mkurugenzi    anayesimamia  vyuo vya Maendeleo  ya  jamii  nchi  kutoka  Wizara  ya Maendeleo  ya  jamii.jinsia   na makundi maalumu Neema Ndoboka amesema  vyuo  vya maendeleo  ya jamii nchini  vimekuwa  na mchango mkubwa  na  kwenda  maeneo mbalimbali  hapa nchini  katika  kwenda kuleta maendeleo   hasa  vijijini na mashirika mengine

Awali  akisoma  taarifa  ya  chuo   hicho  makamu  mkuu wa  chuo  anaeshughulikia  taaluma    Spay Mwangomile amesema kwa  ujumla  nidhamu ya  wanafunzi  imekuwa  ya  kuridhisha uku  wakifundishwa  maadili  mema,uadilifu   na  uwajibikaji  popote  watakapokuwa  wakiwa  kama  mabalozi  wa  chuo  hicho na kuwataka  wanafunzi  waliohitimu chuo hicho   kuwa  wabunifu

Jumla ya  wahitimu     530  wanawake  272 na  258 wanaume  wamehitimu  katika  mahafali  ya  Chuo  hicho  katika  ngazi  ya  aatashahada na  shahada.










Share To:

Post A Comment: