Na Oscar Assenga,TANGA

JUMUIYA wa Wafanyabiashara Tanzania (JWT) Mkoa wa Tanga imemshukuru Rais Dkt Samia Sukuhu kwa kutatua kero za wafanyabiashara na hivyo kuwawezesha kufanya shughuli zao kwa ufanisi kutokana kuondolewa kwa vikwazo ambavyo walikwa walikabiliana navyo awali.

Hayo yalisemwa leo na Katibu wa JWT mkoa wa Tanga Ismail Masoud wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Tanga kutoa shukrani kwa Rais Samia Suluhu na Serikali kwa mambo aliyoyafanyia wafanyabiashara Tanzania hatua ambayo imepeleka kupandisha mapato kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)

Masoud ambaye pia ni Mjumbe Bodi ya Jumuiya ya Wafnyabiashara Tanzania (JWT) alizitaja changamoto ambazo awali zilikuwa zinawakili na sasa zimepatiwa ufumbuzi ni pamoja na umeme ambapo alisema ulipelekea kutokuzalisha kisawasawa kutokana na matatizo ya umeme .

Alisema kufuatia uwepo wa changamoto hiyo,Serikali ya awamu ya sita ilitatua tatizo hilo kupitia Bwawa la Mwalimu Nyerere ambalo limekwisha na hivyo kupelekea kuondoa mgao wa umeme hivyo wanaishukuru awamu ya sita na mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) kwa makusanyo.

Akizungumza changamoto ya utoaji wa mizigo Bandarini alisema kwamba hapo awali ilikuwa ni changamoto lakini kwa sasa sio tatizo limekuwa ni historian a mizigo inatoka kwa haraka na wanalipa kodi kikamilifu na hivyo kupelekea kuchangia maendeleo.

“Lakini Mfumo wa ulipaji kodi TRA umeboresha kwa kiasi kikubwa na wafanyabiashara tunalipa kodi kwa hiari na tunavuka malengo kwenye ulipaji kodi na unajua mwezi Julai tulivuka malengo kutokana na juhudi za awamu ya sita na TRA mikoa yote na TRA imeboresha na kutimiza malengo yake kisawasawa na huo ni ushirikiano na Taasi za wafanyabiashara na tunalijenga Taifa kwa pamoja kufikia malengo ya awamu ya sita kukusanya mapato na kutoa elimu”Alisema

Akizungumza namna ambayo Serikali inawajali na kuwathamini wafanyabiashara Katibu huyo alisema kwamba kwa kipindi cha miaka minne iliunda tume tatu kwa ajili ya wafanyabiashara, kamati ya kariakoo ambayo ilizunguka nchi nzima kukusanya maoni na kuangalia changamoto za wafanyabiashara.

Alisema baada ya kuzungumza baadae ilitoa mapendekezo ambayo serikali iliyafanyia kazi na matokeo yake kwa sasa biaishara zimetulia na wanalipa kodi bila shuruti

Alisema pia Serikali iliunda kamati ya Ombeni Sefue iliundwa na Rais kufuatia mwendezo wa ulipaji kodi na matatizo ya mifumo ya ulipaji kodi Tanzania na mapendekezo yake yanafanyiwa kazi na hivyo wanategemea yatafanyiwa kazi na kuleta tija kwa ulipaji wa kodi Tanzania na kamati hiyo ilifika Tanga kutafuta kero za wafanyabiashara.

Hata hivyo alisema nyengine ni Tume ya kuchunguza biashara kwa wageni ambapo awali kulikuwa na matatizo ya wageni hasa Wachina walikuwa Tanzania wanafanyabiashara zinazofanywa na wazawa hivyo iliundwa na Waziri wa Viwanda na Baishara kwa malekezo ya Rais mwenywe na ilifanya kazi na kupeleka mapendekezo kwa Rais kwamba baadhi ya biashara zitafanywa na watanzania wenyewe huo ni upendo mkubwa sana kwa Rais anawalinda wafanyabiashara wa Tanzania kwa vitendo .

Alisema pia wanaipongeza Serikali kwa kuunda kama zote ambazo zinaonyesha Serikali inafuatilia mwendenzo wa wafanyabiashara na kwamba nini kinatakiwa katika sekta ipi ili wafanyabiashara waweze kuondokana na vikwazo walivyokuwa navyo kwa wastawi na Taifa.

“Ukipiga mahesabu utaona kwa kipindi cha miaka minne unakuta kila mwaka Serikali ilikuwa inaunda Tume ya wafanyabiashara tu pelekee inaonyesha namna inavyowajali lakini imepunguza VAT kutoka asilimia 18 mpaka 16 hapo wamsikilize kwa watanzania wanaonunua bidhaa kwa matumizi yao binafsi yatakayofanyika kwa kutumia mtandao ili kuboresha maisha ya watanzania na wafanyabaishara nchini hivyo ni hatua kubwa kwa kuwajali wananchi wa Tanzania.

Hata hivyo akizungumzia suala la Hotel Levy alisema kwamba katika upande huo Serikali ya awamu ya sita wanaipongeza kupunguza tozo ya Hotel ambapo awali ilikuwa ni asilimia 10 na sasa imeshuka mpaka asilimia 2 ambapo ni punguza kwa asilimia 80 hiyo inawasadia wafanyabaishara wa mahoteli kurekebisha hoteli zao na kuhakikisha zinakuwa bora zaidi na kuwavutia wateja na kukusanya mapato zaidi na kulipa kodi zaidi na kuendeleza taifa letu kwa ustawi wa wafanyabiashata wa hotel.

Hata hivyo alisema kwamba Jumuiya hiyo inaihakikishia Serikali watashirikiana na Taasisi za Serikali kutoa elimu ya mlipa kodi kwa wafanyabaishara wote ili walipe kodi bila shuruti ,kodi stahiki kufuati kauli tya Rais Samia kwamba hataki kodi hya dhuluma hiyo ni kauli dhabiti ina hofu ya Mungu na kamishna wa TRA anaisimamia kikamilifu.

Awali akizungumza Makamu Mwenyekiti JWT Mkoa wa Tanga Fredy Mmasy alisema kwamba wanamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kutokana na hali ya utulivu wa biashara katika Jiji la Tanga na Tanzania kwa ujumla na hata wanaona makusanyo ya kodi kazi kubwa inayosimamiwa na kufanywa na Serikali .

Alisema kutokana na makusanyo hayo makubwa imepelekea ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini ikiwemo barabara kubwa ,ujenzi wa hospitali ,shule na ununuzi wa Ambulence za kubebea wagonjwa yanayonunulwa kwa kodi na hata wigo wa mapato kwa mkoa umeongenezaka kwa hivyo wanamshukuru kwa kusimamia vizuri na hivyo wao kama wafanyabiashara wanaona mafanikio wao wafanyabishara

Naye kwa upande Mfanyabiashara wa Tanga barabara ya kumi Jijini Tanga Pateli alisema kwamba wanampongeza Rais Dkt Samia Suluhu kwa kutatua kero za wafanyabiashara na hivyo kupelekea uwepo wa mazingira ya ufanyaji wa biashara kwao jambo lililopelekea kuzifanya kwa ufanisi na kutokusumbuliwa kama ilivyokuwa awali.

Alisema kwamba hata upande wa kodi wakienda mamlaka ya Mapato TRA wanapata ushirikiano mzuri na kwa sasa hawana changamoto kama zilizokuwepo awali na hivyo kuendelea na shughuli zao.

Akizungumza kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya Mapato TRA Thomas Masese aliwashukuru wafanyabiasha na walipa kodi kwa ushirikiano mkubwa wanaoupata kutoka kwao pamoja na kuipongeza Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) Mkoa wa Tanga kwa jinsi wanavyoshirikiana.

Alisema kwamba moja ya mashirikiano hayo ni pamoja na kufanya mikutano na semina za wafanyabiashara kwa kushirikiana nao kupitia wilaya mbalimbali kuelimisha na kusikiliza kero za wananchi na hivyo namna ushirikiano huo uendele kutokana na kuwa chachu kubwa kwao .

Aidha alisema kutokana na ushirikiano huo ulipelekea mwaka jana 2024/2025 ambapo walikuwa na lengo la kukusanya Bilioni 335 na wakakusanya Bilioni 330 ambayo ni sawa na ufanisi wa asilimia 98 ukilinganisha na mwaka wa nyuma yake mwaka 2023/2024 ambayo walikusanya Bilioni 204 ukilinganisha na mwaka 2024/2025 ambazo wamekusanya Bilioni 330 imekuwa na ongezeko la Bilioni 126 ambazo ni asilimia 61.

Meneja huyo alisema kwamba mwaka huu wamepewa lengo la kukusanya bilioni 361 lakini kwa ushirikiano uliopo kati yao na Jumuiya ya Wafanyabiashara na walipa kodi wanamatumaini watalifikia lengo hilo huku akitoa wito waendelee kushirikiana ili kuweza kukusanya kiwango hicho.

Alisema lakini pia Bandari ya Tanga imefunguka kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na Serikali kwa kuongezewa uwezo wa kupokea meli kubwa mbili zinazoweza kufunga wakati mmoja.

Hata hivyo aliwataka watanzania kuendelea kupitisha shehena zao za mizigo na bidhaa katika Bandari ya Tanga na kwamba upitishaji wake wa mizigo hauchukua muda mrefu kutokana na kutokuwa na msongamano .

Naye Mfanyabiashara wa Vifaa vya Ujenzi na Umeme Jijini Tanga Alphonce Mboya alisema kwamba wana mashukuru Rais Dkt Samia Suluhu kutokana na kuzipatia ufumbuzi changamoto ambazo ilikuwa zikiwakabili ikiwemo lile la kulipishwa madeni ya nyuma ya miaka saba iliyopita ambapo alisema wasilipishwe.

“Tunamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kutokana na kuwathamini wafanyabiashara na kuwaondolea vikwazo ambavyo vilikuwa vinatukabili na sasa tunafanya shughuli zetu kwa uhuru “Alisema 

Share To:

OSCAR ASSENGA

Post A Comment: