KADA ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Hamadi Shamisi Hamadi leo amechukua fomu ya kuwania Udiwani Kata ya Msambweni Jijini Tanga huku akihaidi kufanya kazi kwa uadilifu.

Hamadi aliyasema hayo leo mara baada ya kuchukua fomu katika Ofisi ya Mtendaji Kata ya Msambweni huku akiwa amesindikizwa na wanachama wa chama hicho wakiwemo wananchi.

Alisema kwamba lengo lake ni kuhakikisha anawatumikia wananchi wa kata hiyo na kuwa kiungo cha maendeleo ya wananchi na hivyo kuchochea ukuaji wa maendeleo.

“Nawaambia tutafanya kazi kwa dhati na kutanguliza uaminifu na uadilifu kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo na shahidi ni Baba yangu mzazi ambaye ananisindikiza hapa”Alisema

Awali akizungumza Mwenyekiti wa CCM kata ya Msambweni alisema kwamba hicho ni kishindo cha kwanza ila Agosti 28 wanaanza kampeni zao na wanafungua kwenye tawi la Msambweni B eneo la Komesho watakuwa na Mbunge wa Tanga Jijini kampeni za wilaya zitafunguliwa hapo.

Alisema Agosti 29 utakuwa uzinduzi wa kampeni wa Diwani wa Kata ya Msambweni na zitazinduliwa Mtaa wa Madina eneo la Mabanda ya Papa huku akiwataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi huo.

Naye kwa upande wake Mwenyekiti wa zamani wa Mtaa wa Madina Godfrey Mazimu alisema kwamba amefurahi kuona wanachama wenzake na wananchi wa Msambweni huku akiwataka kuendelea kuunganisha nguvu za pamoja mpaka mwisho na wasiachane.

Share To:

OSCAR ASSENGA

Post A Comment: